Habari Zenye Kuwa Ndani
3 Walijitoa Kwa Kujipendea—Katika Uturuki
JUMA LA TAREHE 28/08–3/09/2017
Habari hii inazungumuzia namna tunaweza kutumia mali zetu za kimwili ili ‘kujifanyia marafiki’ mbinguni. (Lu. 16:9) Inazungumuzia pia namna tunaweza kuepuka kuwa watumwa wa mambo ya biashara yenye pupa ya ulimwengu huu, na namna gani tunaweza kufanya mengi zaidi katika kazi ya Yehova.
JUMA LA TAREHE 4-10/09/2017
12 ‘Mulie Pamoja na Watu Wanaolia’
Namna gani Mukristo anaweza kupambana na huzuni ya kupoteza mupendwa wake katika kifo? Yehova anatutolea faraja nyingi yenye tuko nayo lazima kupitia Yesu Kristo, Maandiko, na kupitia kutaniko la Kikristo. Habari hii itatuonyesha namna sisi na wengine wenye kuomboleza tunaweza kupata faraja.
JUMA LA TAREHE 11-17/09/2017
17 ‘Musifu Yah!’—Sababu Gani?
Zaburi ya 147 inatia moyo watu wa Mungu tena na tena wamusifu Yehova. Ni jambo gani lenye kumuhusu Yehova lenye lilishangaza sana muandikaji wa zaburi hivi kwamba alipenda Mungu asifiwe? Habari hii inatoa jibu, na inaonyesha sababu gani tunapaswa kuwa na hamu kama hiyo ya kumusifu Mungu wetu.
JUMA LA TAREHE 18-24/09/2017
22 Na Atimize Mipango Yako Yote
Ndugu na dada wengi vijana wanaendelea kuingia kwa bidii katika utumishi wa wakati wote. Unatamani kufanya hivyo? Habari hii inatoa mashauri ya muzuri kutoka katika Maandiko yenye yatakusaidia ili ufanye mipango kwa ajili ya wakati unaokuja wa muzuri na wenye furaha.