‘Tuendelee Kukomaa Katika Ujuzi Sahihi’
Ujuzi sahihi wa Mungu unaongoza kwenye uhai udumuo milele. (Yn. 17:3) Tungepaswa kufanya yote tuwezayo ili kukomaa katika ujuzi sahihi wa Yehova. (Kol. 1:9, 10) Ni tangu Aprili 29 tunajifunza kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele katika mpango wa mafunzo ya kitabu. Si tu kwamba tutaongeza wenyewe uelewevu wetu wa Neno la Mungu, lakini pia tutatayarishwa vizuri kufundisha wengine. Tutabarikiwa, na pia familia yetu, ikiwa tunajitayarisha, ikiwa tunahudhuria na kushiriki kila juma, na ikiwa tunatumia yale tunayojifunza katika huduma.