Tumheshimu Yehova Kwa Michango Yetu Ya Kujipendea
1 “Alaaniwe mudanganyifu aliye na ndume katika kundi lake, anayeapa na kutoa kwa [Yehova] kitu kilicho kilema; kwa maana mimi ni Mufalme mukubwa, [Yehova] wa majeshi anasema.” (Malaki 1:14) Je! tunaona ni jambo geni kwamba wanadamu wasiokamilika waweze kutoa kitu fulani kwa Muumba? Hakuna kitu katika ulimwengu mzima kisichokuwa tayari chake. Mungu mwenyewe anasema katika Neno lake: “Feza ni yangu, na zahabu ni yangu.” (Hagai 2:8) Mungu haitaji zawadi zetu kwa kuwa anajitosheleza mwenyewe. Mfalme Daudi alitambua kwamba sisi kama wanadamu hatuwezi kwa vyovyote kumtajirisha Mweza-Yote. Kwa hiyo, iwe tungempa nini, tunamrudishia tu sehemu ndogo ya yale tuliyopokea kutoka kwake, chanzo cha “kila zawadi njema na kila upaji mkamilifu.” Je! tufikie hivyo uamuzi wa kwamba michango yetu tunayotoa kwa ajili ya ibada ya Yehova haina thamani yoyote machoni pake? Je! Mungu anadharau michango yetu ya kujipendea? Mtunga zaburi anajibu: “Leteni sadaka na ingieni katika viwanja vyake.”—Zab. 96:8.
2 Jinsi gani mahubiri ya habari njema ya Ufalme yanategemezwa kifedha katika nchi yetu? Kupitia michango ya kujipendea inayotolewa na watumishi wa Yehova na watu wenye mioyo tayari. Kwa msaada wa michango hiyo tengenezo la Yehova linawatunza mapainia wa pekee, wamishonari na waangalizi wasafiri, na pia familia ya Betheli. Tufikirie kidogo gharama kubwa zinazofanyika kwa usafirishaji wa vitabu na magazeti katika makutaniko zaidi ya 2 200 ya Burundi, Congo na Zaïre. Je! tunafikiria fedha zinazotumiwa juu ya matayarisho ya makusanyiko ya wilaya, kwa mfano? Na tuseme nini juu ya uandikaji na uchapaji kwa vichapo vyetu? Kwa kweli fedha hizo hutoka hivyo wapi? Mpaka sasa, tutasema, gharama zote hizo zimelipiwa kwa kadiri kubwa na michango ya kujipendea ya ndugu na dada zetu wa nchi kama vile Ubeljiji, Ufaransa, n.k. Wale wanaotoa michango katika nchi hizo kwa kawaida si watu matajiri. La hasha! Badala yake ni waabudu wa Yehova wanaoonyesha uthamini wao kwa ajili ya mambo ya kiroho. Wanakumbuka ibada ya Yehova kwa kutayarisha kikawaida mchango fulani kwa ajili ya nyumba ya Yehova. (Ona 1 Kor. 16:2.) Ni wanaume na wanawake, watoto, vijana na watu wazee-wazee, kama wale wanaopatikana hapa kwetu.
3 Katika karne ya kwanza ya wakati wetu wa kawaida, mtume Paulo alilisifu kutaniko la Wafilipi katika maneno yafuatayo: “Hata hivyo, mlitenda vema kuwa washiriki pamoja nami katika dhiki yangu. . . . Kwa sababu, hata katika Thesalonike, nyinyi mlinipelekea kitu fulani mara moja na mara ya pili kwa ajili ya uhitaji wangu.” (Flp. 4:14, 16, NW) Je! tunaweza kusema vivyohivyo juu ya eneo letu? Je! tunaonyesha pia hali ya akili bora kama hiyo? Je! kila mmoja wetu, anatamani kuonyesha uthamini wake kwa ajili ya mambo ya kiroho kwa kutoa michango ya kujipendea? Mnamo miezi ya nyuma, michango iliyopokelewa Zaïre kwa mfano ilifikia kwa wastani 180 NZ kwa kila mhubiri. Hata hivyo, ili kulipia gharama zetu zinazoambatana na utangazaji wa habari njema nchini, michango ya kujipendea ingepaswa kila mwezi kuwa, kwa wastani ya dola 4.45 kwa kila mhubiri.
4 Kutokana na hilo, inaonekana kwamba tunapaswa kujichunguza ili kuona ni uwezekano gani mbalimbali wa eneo letu, kuhusu kulipia gharama zinazoambatana na kazi ya Ufalme. Kanuni bora tunayopata katika barua ya pili ya Paulo kwa Wakorintho, kwenye sura ya nane, inastahili uangalifu wetu. Ikiwa tunathamini pendeleo letu la kumtumikia Yehova, tutatoa michango pia “kulingana na uwezo wetu halisi.” (mstari 3, NW) Tunapaswa kila mmoja kufanya uchunguzi wa kibinafsi, “kwa maana ikiwa utayari upo kwanza, hukubaliwa hasa kulingana na alicho nacho mtu, si kulingana na kile ambacho mtu hana.”
5 Je! tunaweza kuondoa juu ya “kidogo tuliyo nayo,” ili kutoa kwa faida ya ibada safi? Mtu anaweza kusema: “Mimi, ninapenda kutoa lakini sina kitu.” Labda hilo litakuwa jambo gumu zaidi kwa wamoja kuliko wengine. Vijana na wazee, wanaume na wanawake, watoto na wakubwa, sote tunaweza kujichunguza kwa makini ili kuona yale tunayoweza kutoa kikawaida kulingana na uwezo wetu. Tusijisikie kamwe hoi ati kwa kuwa kile tunachoweza kutoa ni kidogo sana. (Ona Luka 21:2-4.) Ikiwa kila mmoja anafanya hivyo kwa kujipendea, kwa moyo wake wote na kwa furaha, na ikiwa wale walio na uwezo wa kuzidi wengine wanatoa zaidi, kutakuwa na usawa-sawa unaojazia kile kinachokosa kwa wengine.—2 Kor. 8: 13, 14; 9:7.
6 Baraza la wazee la kutaniko linaweza kutimiza mengi ili kwamba uthamini huo ukue na ukomae katika kutaniko. [Ona pia mawazo ya Mnara wa Mlinzi wa Desemba 1, 1992, kurasa 8 na 9, mafungu 8 mpaka 10 na ukurasa 16, mafungu 16 na 17, juu ya zaka.] Enyi wazee, je! mngependa kutolea kutaniko azimio ili kutuma kwa ukawaida kila mwezi mchango wa kujipendea kwenye tawi? (Chunguzeni Huduma Yetu ya Ufalme ya Agosti 1994 juu ya utaratibu wa kufuata ili kutoa maazimio kutanikoni) Hesabu ya fedha inaweza kubadilika toka mwezi mmoja hadi mwingine, kwa kadiri kutaniko linavyofanikiwa kiroho na kwamba Yehova anabariki jitihada njema yalo.—Mit. 10:22.
7 Ikiwa tunatoa kwa furaha na ukarimu katika kusudi la kutegemeza ibada ya kweli, tutafanikiwa. Tutege sikio kwa kitia-moyo hiki katika Mezali 3:9, 10: “Heshimu [Yehova] kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazidio yako yote. Hivi gala zako zitajazwa kwa wingi.” Tunaweza hivyo kuonyesha shukrani yetu kwa ajili ya pendeleo ambalo Yehova anatutolea la kumtumikia kwa utumishi mtakatifu. Kwa michango ya kujipendea ambayo kila mmoja wetu atatoa, tunaleta msaada wetu bora ili kuendeleza mbele ibada safi katika eneo. Hasa zaidi tukumbuke: kwamba kwa kufanya hivyo, tunamheshimu Yehova kwa mali zetu.