Mikutano Ya Utumishi Ya Mei
Juma Toka Mei 6
Wimbo 132
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Eleza mambo yaliyoonwa yenye maana yanayohusiana na Ukumbusho ulioadhimishwa katika kutaniko lenu.
Dak. 15: “Nyakati Zinabadilika.” Kwa maulizo na majibu. Tilia mkazo ulazima wa kutoa ujumbe wa Ufalme kwa kusema juu ya kile kinachosumbua zaidi watu. Zungumza juu ya matatizo fulani fulani ya kifamilia au yanayoambatana na uhusiano wa kibinadamu unaowashughulisha watu wengi, kama hilo linavyoonyeshwa katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1994, kurasa 22-3.
Dak. 20: “Kila Andiko Lafaa kwa Kufundisha.” Zungumzia mambo yanayofanya Biblia Traduction du monde nouveau iwe ya pekee na onyesha katika njia gani inapita zile nyingine. Onyesha faida mbalimbali za usemi wake wa ki-siku-hizi. (Ona kitabu “Kila Andiko,” ukurasa 328, mafungu 4-6.) Maonyesho mawili kutokana na vielelezo vinavyodokezwa.
Wimbo 20 na sala ya mwisho.
Juma Toka Mei 13
Wimbo 72
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Hali ya akaunti.
Dak. 20: “Tutoe Utumishi Mtakatifu Mchana na Usiku.” Kwa maulizo na majibu. Someni mafungu 5 na 6.
Dak. 15: “Tuwasaidie Majirani Zetu Kutambua Thamani ya Biblia.” Mzee mmoja anazungumza na wahubiri wawili au watatu juu ya sababu za kufanya ziara za kurudia pamoja na kusudi la kuanzisha mafunzo ya Biblia. Chunguzeni vielelezo vinavyodokezwa kwa ajili ya ziara za kurudia na fanyeni maonyesho kwa mfano wa vipindi vya mazoezi.
Wimbo 113 na sala ya mwisho.
Juma Toka Mei 20
Wimbo 133
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Je! Programu ya Mikutano Itabadilika?” Mwangalizi-msimamizi anazungumzia sehemu hiyo pamoja na wasikilizaji. Kwa kadiri wakati utakavyoruhusu, chunguza mawazo ya Mnara wa Mlinzi wa Agosti 15, 1988, ukurasa 19, fungu 15 na wa Oktoba 1, 1988, ukurasa 17, fungu 13.
Dak. 20: “Tujiendeshe kwa Namna Yenye Kustahili ile Habari Njema.” Kwa maulizo na majibu. Rudilia mawazo fulani fulani kutokana na Mnara wa Mlinzi wa Juni 15, 1989, kurasa 16-17, mafungu 5-9.
Wimbo 204 na sala ya mwisho.
Juma Toka Mei 27
Wimbo 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kumbusha mawazo fulani fulani ya maana ya hotuba ya pekee na sema jinsi yanavyoweza kuchochea watu wenye kupendezwa kuchukua msimamo imara kwa ajili ya ibada ya kweli. Vutia pia uangalifu juu ya kisanduku “Tuendelee Kukomaa Katika Ujuzi Sahihi” na tilia mkazo ulazima wa kuhudhuria kikawaida funzo la Biblia.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko. (Au hotuba yenye msingi wa makala “Je! Wewe Hufurahia Funzo la Kibinafsi?” iliyotolewa katika Mnara wa Mlinzi wa Juni 15, 1994, kurasa 8-11.)
Dak. 20: Tutolee kitabu kipya Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele mnamo Juni. Chunguza upya mambo ya pekee yanayovutia ya kitabu: vichwa vya habari vyenye kuvutia vya sura, picha zinazosema zenyewe na pia maelezo mepesi, udogo wa kitabu na matumizi yenye akili ya maulizo. Chagua vichwa fulani fulani vya mazungumzo vinavyoweza kupendeza watu wa eneo. Kitabu Ujuzi kimetengezwa kipekee kwa ajili ya kuongoza tu mafunzo ya Biblia yenye kuzaa matunda. Bidii ya pekee ingepaswa kufanywa ili kurudilia kuwaona wote wale waliokikubali, pamoja na kusudi la kuanzisha mafunzo ya Biblia. Onyesho moja au mawili mafupi na mhubiri mwenye uwezo. Tia kila mmoja moyo kufanya matumizi mazuri ya kitabu hicho kipya katika mahubiri tangu Juni.
Wimbo 195 na sala ya mwisho.