Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea mnamo Juni: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! na broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? Julai: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Tutajikaza hasa kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Agosti na Septemba: Broshua moja ya kurasa 32 kati ya zifuatazo: Je! Kweli Mungu Anatujali?; Je! Uamini Utatu?; Serikali Itakayoleta Paradiso; Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. . . ; Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?; Kuishi Milele Duniani Katika Furaha!
◼ Vichapo vinavyopatikana tena katika stoki:
Kiingereza: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!; Mwimbieni Yehova Sifa (sahani ya santuri kompakti—musiki wa piano); Kuishi Milele Duniani Katika Furaha! Mungu Anataka Nini Kwetu? Kiarabu: Kuishi Milele Duniani Katika Furaha! Trakti Na. 13, 14, 15, 16, 19, 20, 21, 22. Kifaransa: Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu; Mwimbieni Yehova Sifa (aina ndogo); Vijana Huuliza; Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi; Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia; Fahirisi 1986-1990. Lingala : Vijana Huuliza; Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Otetela : Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi; Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Kireno: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi; Maisha ya Furaha ya Jamaa; Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu Pekee wa Kweli. Swahili : Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Tshiluba: Siri ya Kupata Furaha ya Familia; Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
◼ Tuna aina mbalimbali ya kaseti za kusikiliza katika stoki. Wahubiri wanatiwa moyo kujipatia zenyewe kwa matumizi yao wenyewe. Kaseti za vitabu vya Biblia ni za lazima sana. Tunaweza kuzisikiliza tunapokuwa tukila chakula au wakati tunaposhughulika na kazi mbalimbali nyumbani.
◼ Kila kutaniko linatiwa moyo kuongeza agizo lake la magazeti, kulingana na mahitaji ya kila mhubiri, na kurekodi maandikisho mapya. Inafaa kungoja miezi mitatu ili kufaidika na mabadiliko hayo na kupokea namba za maandikisho, hilo kuhesabu kuanzia tarehe ambayo maelezo yalipotumwa kwenye afisi. Lalamiko lolote kwa upande huo haliwezi kufanywa kabla ya muda wa miezi mitatu.
◼ Tangu mwezi wa Februari 1997, kwa sababu zenye kutenda kazi, afisi inatumia tangu hapo hesabu fupi zaidi katika akaunti za makutaniko ya Zaïre. Ili kupata tarakimu au hesabu halisi, inafaa kuongeza sufuri tatu upande wa mkono wa kulia wa hesabu hiyo. Kwa mfano: NZ 1,800 maana yake NZ 1,800,000. Lakini, wakati wa kutuma fedha zenu kwa njia ya fomu S-20, tunawaomba kuandika hesabu zote hizo bila kuzikata. Kwa mfano, NZ 1,800,000 kuandika NZ 1,800,000 na hapana NZ 1,800.
◼ Tunawajulisha, kwa huzuni, kwamba kuanzia mwezi wa Juni, afisi haitapokea tena hesabu za mwaka za Septemba 1996. Makutaniko ambayo, mpaka hivi hayakuzituma kwenye afisi, hayatahudumiwa vichapo.
◼ Ikiwa ndugu fulani ana barua ya kutuma toka mji mmoja kwenda mji mwingine wa nchi, atapaswa kushughulika nayo mwenyewe. Ni vivyo hivyo na barua zinazotumwa kwa watu binafsi au kwenye makutaniko katika nchi nyingine. Barua kama hizo hazipaswi kutolewa kwa ndugu anayehusika na bohari ya Sosaiti ili kuzituma kwenye Betheli ya Kinshasa tukifikiria kwamba Betheli itazituma hadi mahali zinapokwenda. Ni kweli kwamba kuchagua na pia kutuma (na wakati mwingine kutuma tena) barua hizo za kibinafsi hufanyika kwa bei ghali; zaidi ya hayo, hilo linatokeza kazi kubwa ya ziada kwa akina ndugu wanaotumika kwenye Betheli.