Mikutano Ya Utumishi Ya Julai
Juma Toka Julai 7
Wimbo 181
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa ya Huduma Yetu ya Ufalme. Eleza ripoti ya kutaniko ya mwezi wa Juni.
Dak. 15: “Fanya Yote Uwezayo Kabisa.” Kwa maulizo na majibu.—Ona Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1993, kur. 28-30.
Dak. 22: “Ujuzi Utokao kwa Mungu Unajibu kwa Maulizo Mengi.” Ndugu mmoja anaongoza uchunguzi wa makala pamoja na wahubiri wawili au watatu, kati yao kukiwa kijana. Eleza fungu la 1 kwa kukazia kwa nini kitabu Ujuzi ni chenye matokeo sana ili kusaidia kujibu kwa maulizo. Onyesho: fanyeni tamasha moja ya mazoezi na toeni madokezo ili kuboresha kila utoaji uliofanywa.
Wimbo 200 na sala ya mwisho.
Juma Toka Julai 14
Wimbo 189
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Hali ya akaunti.
Dak. 15: “Vijana, Miradi Yenu ya Kiroho Ni Gani?” Baba wawili wa familia wanachunguza pamoja makala. Wanapanga njia za kuwasaidia watoto wao kuelewa kwa nini ni lazima kujiwekea miradi ya kitheokrasi, jambo ambalo litawaletea baraka za kiroho, badala ya kufuatia faida za kimwili.—Ona kitabu Huduma Yetu, kur. 116-118.
Dak. 20: Kufundisha Wengine: Uhitaji wa Lazima. Hotuba inayotolewa na mzee. Chunguza ripoti ya utumishi ya ulimwengu ya 1996 katika Kitabu-Mwaka 1997, uku. 33. Bidii nyingi kwa ajili ya kutoa ushuhuda mahali ambapo watu wengi hupatikana inazaa matunda. Sasa, kuna uhitaji wa haraka wa kuwaona watu ambao tuliachia kichapo na kuwafundisha ukweli. Tunapokutana nao katika mahali pa watu wengi, tuwaulize kwa busara jina na anwani yao ili kwamba ziara ya kurudia ifanywe kwao. Imetupasa kufanya mengi zaidi ya kupanda tu mbegu ya Ufalme; tunapaswa pia kutilia maji. (1 Kor. 3:6-8) Wakati mbegu inapopandwa juu ya udongo mzuri, mafundisho yenye matokeo yanaweza kusaidia mtu kuelewa maana yake. (Mt. 13:23) Tunapaswa kushiriki katika kazi ya kufundisha kikamilifu na kwa ustadi iwezekanavyo. (Ebr. 5:12a) Tumia mawazo yanayotolewa katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996, mafungu 25-6. Kazia bidii ambayo inafaa kufanya ili kuanzisha mafunzo pamoja na broshua Anataka au kitabu Ujuzi.
Wimbo 204 na sala ya mwisho.
Juma Toka Julai 21
Wimbo 192
Dak. 10: Matangazo. Tokeza mawazo yenye kupendeza ya magazeti ya mwisho mwisho.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 20: Je! Mimi Nimo Katika Dini ya Kweli? Mzee mmoja anaongoza mazungumzo pamoja na wahubiri wawili au watatu wenye uwezo juu ya msingi wa Amkeni! (kifaransa) ya Desemba 22, 1989, uku. 18. Tunawatembea kwa uwingi watu wanaoonekana kuwa wanyofu. Hata hivyo, hawajawai kamwe kukubali funzo la Biblia. Chunguza mawazo ya makala hayo ya Amkeni! yanayoweza kuwasaidia kutambua ulazima wa kutenda kulingana na ujuzi sahihi. Taja nukta kubwa za sura ya 5 ya kitabu Ujuzi, yenye kichwa “Ni Ibada ya Nani Anayoikubali Mungu?” Soma fungu 20. Tunaweza kufanya ziara za kurudia kwa watu hao ili kuwatia moyo kwa upole na kwa busara kukubali funzo na kuhudhuria kwenye mikutano.
Wimbo 201 na sala ya mwisho.
Juma Toka Julai 28
Wimbo 193
Dak. 10: Matangazo. “Habari za Kitheokrasi.”
Dak. 15: “Wazazi—Muwazoeze Watoto Wenu Katika Mahubiri.” Kwa maulizo na majibu. Zungumzia pia maagizo yanayotolewa katika kitabu Huduma Yetu kwenye kichwa kidogo cha habari “Kusaidia Vijana,” kur. 99-100.
Dak. 20: Tujitayarishe kwa Ajili ya Toleo la Agosti. Chagua broshua moja au mbili zinazopatana na eneo la kutaniko na chunguza upya nukta fulani za lazima katika kila mojawapo yazo. Sema jinsi zinavyoweza kutumiwa katika utoaji.
Wimbo 211 na sala ya mwisho.