Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea mnamo Septemba: Broshua moja ya kurasa 32 kati ya zifuatazo: Je! Kweli Mungu Anatujali?; Je! Uamini Utatu?; Serikali Itakayoleta Paradiso; Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa . . ..; Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?; Kuishi Milele Duniani Katika Furaha! Oktoba: Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Novemba: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ikiwa mtu anaonyesha kupendezwa wakati wa ziara za kurudia, itawezekana kumtolea uandikisho. Desemba: Ugawaji wa trakti Habari ya Ufalme Na. 35. Makutaniko ambayo yametembelea eneo lote na kuangusha Habari za Ufalme Na. 35 kwa washiriki wa kila familia au nyumba wanaweza kutolea kitabu Ujuzi.
◼ Katika kila mji, kwa nyakati tofauti mwakani, kuna siku zisizo za kazi muda wazo watoto hawaendi shuleni na watu wazima hawatumiki. Ni nafasi bora kwa kutaniko kuwa na utendaji mwingi katika mahubiri. Ili kuarifu kutaniko mapema zaidi juu ya mipango iliyochukuliwa kwa ajili ya mahubiri ya kikundi muda wa siku hizo zisizo za kazi, wazee wangepaswa kujua tarehe ya siku hizo.
◼ Kila kutaniko lilipokea, kulingana na mahitaji yalo, fomu kwa mwaka wa utumishi 1998. Tafadhali zitumieni kwa busara. Zitalindwa tu kwa matumizi kwa ajili ya hayo zinatumwa.
◼ Akaunti za kutaniko zinapaswa kuchunguzwa Septemba 1, au mapema zaidi iwezekanavyo kisha tarehe hiyo, na mwangalizi-msimamizi au na mtu mwingine atakayechaguliwa naye. Kutaniko litatangaziwa baadaye kwamba uchunguzi ulifanywa. cf km 9/95
◼ Wahubiri wanaotazamia kuwa mapainia wasaidizi mnamo Oktoba wangepaswa kutoa haraka ombi. Wazee wataweza hivyo kuchukua mipango kuhusu magazeti, vitabu na maeneo.cf km 9/95
◼ Wazee watafanya uangalifu kufuata mashauri ya Mnara wa Mlinzi wa Aprili 15, 1991, kurasa 21-3, kuelekea kila mtu aliyetengwa au aliyejitenga na ushirika na ambaye angeweza kuonyesha nia ya kurudi.