Mikutano Ya Utumishi Ya Novemba
Juma Toka Novemba 3
Wimbo 39
Dak. 10: Matangazo. Matangazo yaliyochaguliwa ya Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 15: “Je! Kuna Wakati Ambao Watu Wataweza Kupendana?” Kwa maulizo na majibu. Chunguza nukta kuu za trakti Habari za Ufalme Na. 35. Kazia sababu kutokana na hizo watu wa eneo watafaidika na habari hizo. Sisitiza juu ya ulazima wa kuchukua mipango tangu sasa kwa ajili ya kushiriki kikamilifu katika ugawaji wa trakti Habari za Ufalme na kufuatia kwa juhudi kila kupendezwa ambako itaamsha.
Dak. 20: “Tugawe kwa Uwingi Trakti Habari za Ufalme Na. 35.” Hotuba ya utangulizi inayotolewa na mwangalizi wa utumishi. Chunguza mafungu 5-8 kwa maulizo na majibu. Onyesha ni mipango gani iliyochukuliwa kwa ajili ya utendaji wetu wenye kuongezeka. Zungumza juu ya njia mbalimbali za kuangalia ili kwamba eneo liwe limetembelewa kikamilifu. Wahubiri wanaweza kutumikisha trakti Habari za Ufalme Na. 35 ili kutoa ushuhuda kwenye vituo vya basi, katika maduka madogo-madogo, nafasi za kuegeshea magari na mahali penginepo. Toa madokezo juu ya namna ya kuwasaidia wapya wanaotamani kuanza kuhubiri. Katika maeneo fulani, litakuwa labda jambo la akili kuhubiri mwenyewe na kutokutumia mfuko wa mahubiri ili kugawa trakti Habari za Ufalme. Maonyesho mawili au matatu mafupi.
Wimbo 126 na sala ya mwisho.
Juma Toka Novemba 10
Wimbo 41
Dak. 12: Matangazo. Hali ya akaunti. Kazia mawazo kutokana na namba za mwisho mwisho za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ambayo tunaweza kutumia ili kuanzisha mazungumzo. Kumbusha wahudhuriaji wote kwamba tutatolea magazeti pamoja na trakti Habari za Ufalme Na. 35 mnamo mwisho-juma. Tunapaswa kufuata kupendezwa. Omba wahudhuriaji kuleta broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote kwenye mkutano wa juma lijalo.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 18: “Jinsi Gani Tunaitikia Kuelekea Ubaridi?” Mazungumzo kati ya wazee wawili. Ingizeni maelezo kutokana na habari zinazopatikana chini ya kichwa kidogo cha habari “Jinsi ya Kupambana na Ubaridi”, katika Mnara wa Mlinzi wa Novemba 1, 1974, ku. 669-70 (kifaransa)
Wimbo 130 na sala ya mwisho.
Juma Toka Novemba 17
Wimbo 42
Dak. 15: Matangazo. Taja mambo yaliyoonwa ya Kitabu-Mwaka 1996, kur. 6-8, chini ya kichwa kidogo cha habari “Ugawaji wa Ulimwenguni Pote wa Trakti Habari ya Ufalme.” Kazia jitihada za kibinafsi zilizofanywa na wahubiri wakati wa ugawaji wa mwisho wa trakti Habari za Ufalme. Tia kila mmoja moyo kujitoa kikamilifu katika ugawaji wa trakti Habari za Ufalme Na. 35.
Dak. 15: Nukta Kubwa Kutokana na Broshua Mpya Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji juu ya sababu kutokana na hizo Biblia inastahili kuchunguzwa. Broshua hiyo imetayarishwa ili kuwasaidia watu walio labda na elimu ya kutosha, lakini wanaojua mambo madogo tu juu ya Biblia. Haijaribu kuwasadikisha kwamba Biblia iliongozwa na Mungu; badala yake, inaacha mambo ya kweli yajisemee yenyewe. Tungepaswa kuisoma na kuijulisha kwa wengine, hasa kwa wale tunaojifunza nao.
Dak. 15: “Je! Sisi ni Mashahidi wa Wakati Wote?” Hotuba inayotolewa na mzee.
Wimbo 133 na sala ya mwisho.
Juma Toka Novemba 24
Wimbo 43
Dak. 12: Matangazo. Sema mnafikia wapi katika ugawaji wa trakti Habari za Ufalme Na. 35. Alika wasikilizaji kuripoti mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo. Onyesha ni kwa kadiri gani eneo limetembelewa mpaka sasa na yale yanayobaki kufanya ili kulitembelea kikamilifu tangu sasa hadi Desemba 14. Wakati eneo lote litakuwa limekwisha kutembelewa, tutatolea kitabu Ujuzi mpaka mwisho wa Desemba. Sisitiza juu ya mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia wakati wa ziara za kurudia kwa watu walioitikia vizuri wakati tulipowatolea trakti Habari za Ufalme.
Dak. 15: Kupata Tumaini Katikati ya Hali ya Kukata Tumaini. Hotuba inayotolewa na mzee, kutokana na Mnara wa Mlinzi wa Mei 15, 1997, kur. 22-5.
Dak. 18: Nuru Yenu na Iangaze. Hotuba na mazungumzo juu ya kurasa 84-8 za kitabu Huduma Yetu. Omba mapema kwa wahubiri fulani kutayarisha maelezo juu ya maulizo yafuatayo: (1) Kwa nini Mashahidi wa Yehova wanahubiri nyumba kwa nyumba? (2) Ni kwa kadiri gani ufundi huo ulikuwa ukitumiwa kwenye karne ya kwanza? (3) Kwa nini leo ni lazima hasa kuendelea kuhubiri nyumba kwa nyumba? (4) Ni nini leo kinachofanya iwe vigumu kushiriki kikawaida katika mahubiri? (5) Ni msaada gani tunaweza kufaidika nao ili kudumu? (6) Tunabarikiwa namna gani ikiwa tunafanya nuru yetu ingae? (7) Tunaweza kufanya nini ili kuwa wenye matokeo zaidi kwa kuwafikia watu? Toa mfano kwa kuomba wahubiri watatu au wanne kuripoti mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo yaliyotokea wakati wa mahubiri katika maduka na barabarani.
Wimbo 136 na sala ya mwisho.