Yehova Hutoa Nguvu Ipitayo Iliyo Ya Kawaida
1 Wanafunzi wote wa Yesu walijikuta wamekabiziwa pendeleo lenye thamani linalotokana na utumishi mtakatifu: huduma ya Kikristo. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Hata hivyo, kwa sababu ya kutokukamilika kwa kibinadamu na magumu yaliyo sehemu ya mfumo wa sasa wa mambo, inaweza kufikia kutokujisikia kuwa wenye uwezo.
2 Hilo linapotufikia, tunaweza kupata burudisho katika barua ambayo mtume Paulo aliandikia Wakristo wapakwa-mafuta wa Korintho. Aliandika: “Sisi tuna hazina hii katika vyombo vya udongo.” (2 Kor. 4:7) Paulo alikuwa hakika: “Kwa kuwa sisi tuna huduma hii [...], hatufi moyo.” (2 Kor. 4:1) Tutambue kwamba si jambo rahisi kwa mtu awaye yote, tuwe Wakristo wapakwa-mafuta au washiriki wa “kondoo wengine,” kuendelea kutangaza habari njema na ‘kutokufa moyo.’ Tunahitaji kwamba Mungu atutolee uwezo, “nguvu ipitayo iliyo ya kawaida.”—Yn. 10:16; 2 Kor. 4:7b.
3 Ni jambo lenye kutia moyo kuona kwamba ijapokuwa upinzani mkali, matatizo makubwa ya afya au hali mbaya ya kiuchumi Mashahidi wengi ni waeneza-evanjeli wenye bidii. Tunapaswa sisi sote kutambua kwamba utendaji wetu wa kuhubiri una utegemezo wa Yehova. Pia, tusiruhusu kuvunjika moyo au hofu vidhoofishe azimio letu, lakini ‘tuendelee kujipatia nguvu katika Bwana na katika uwezaji wa nguvu yake.’—Efe. 6:10; Mit. 24:10.
4 Namna Gani Kujipatia Nguvu ya Mungu: Tusali Mungu kwa kudumu tukimwomba utegemezo wake na uweza wake. (Rom. 12:12; Phil. 4:6, 7) Kisha, kwa moyo wetu wote, tuweke tumaini letu katika Yehova, tukiwa hakika kwamba atatutolea nguvu ipitayo iliyo ya kawaida. (Mit. 3:5) Tusome maandishi ya maisha ya watu yanayotangazwa katika magazeti yetu; yanatoa uthibitisho kwamba Yehova anasaidia watumishi wake kushindana na majaribu. Tushirikiane kwa ukaribu na ndugu na dada wa kutaniko, na tusiache mikutano.—Rum. 1:11, 12; Ebr. 10:24, 25.
5 Tufanye yote tuwezayo ili kuweza kupokea nguvu ya Yehova, nguvu ipitayo iliyo ya kawaida na itakayotuwezesha kutokufa moyo katika kazi ya maana sana ya kuhubiri Ufalme.