Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/98 uku. 2-5
  • Matangazo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 1/98 uku. 2-5

Matangazo

◼ Vichapo vya kutolea katika Januari: Tafsiri ya Ulimwengu Mpya na kitabu Biblia: Neno la Mungu au la Binadamu? Februari: Kila kitabu chenye kurasa 192 kilichotangazwa kabla ya 1985 kilicho katika stoki ya kutaniko. Makutaniko yasiyokuwa nacho yataweza kutolea kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Machi: Ufunuo: Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Aprili: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada za pekee zitafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia.

◼ Makutaniko yangepaswa kuanza kufanya ombi la mabuku ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! 1997 kwenye ombi lao la vichapo. Mabuku yatapatikana katika Kiingereza, Kifaransa na Kireno. Mabuku ni bidhaa vinavyofanyiwa ombi la pekee.

◼ Akaunti ya kutaniko inapaswa kuchunguzwa na mwangalizi msimamizi au mtu mwingine atakayechaguliwa naye mnamo Machi 1, au mapema zaidi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Itatangazwa baadaye kutanikikoni kwamba uchunguzi huo umefanywa.

◼ Katika 1999, Ukumbusho utasherehekewa Siku ya Nne, Aprili 1, baada ya jua kutua. Tarehe hiyo inatangazwa mapema ili kuwezesha kulinda au kukodisha majumba mahali ambapo makutaniko mengi yanatumia Jumba la Ufalme moja, jambo linalowalazimisha kupata majumba mengine wakati huo. Wazee wanapaswa kupata kibali cha afisi yenye kushughulika na jumba linalokodiwa kwamba tukio lingine lolote katika makao hayo halitavuruga sherehe ya Ukumbusho. Kwa sababu ya umaana wa tukio hilo, baraza la wazee lingepaswa kuchagua kama msemaji kwa ajili ya Ukumbusho mmoja wa wazee wenye uwezo zaidi, badala ya kutosheka na kuchagua msemaji mmoja baada ya mwingine kwa kuachiana zamu au kutumia ndugu yule yule kila mwaka.

◼ Mara moja kwa mwaka, tawi la Ufaransa huchapa fomu tunazohitaji kwa ajili ya mwaka mzima, kulingana na ombi letu na kuhusiana na hesabu ya wahubiri. Hivyo, tunakumbusha makutaniko kutumia stoki yao vizuri ili isimalizike kabla ya kutolewa zingine kunakopangwa mwaka ujao. Haikupangwa kuhudumia ombi la fomu katikati ya mwaka, isipokuwa kwa makutaniko mapya. Namna ya kutumia fomu zenu ili zimalize mwaka wote:

◆ Za kutumiwa kila juma: M-1, M-101, M-203, S-24. Tumeni tu nakala ya kwanza kwenye afisi; nakala ya pili inabaki katika fahili ya kutaniko. Hamtatuma zote mbili. S-8, S-48, S-61a, ­S-61b na S-88 zinaweza kutumiwa kila juma lakini hazitumwi kwenye afisi ya tawi. Zinabaki katika kutaniko.

◆ Za kutumiwa mara moja kwa mwezi: ­S-14, S-20. Hapo pia, nakala moja tu ndio hutumwa kwenye tawi, nakala ya pili huchungwa katika fahili ya kutaniko. Kwa upande mwingine, S-3, S-4, S-26, S-28, S-30 na S-89 zinajazwa kila mwezi, lakini hazitumwi kwenye afisi. Kila kutaniko litapokea nakala 13 za S-1 kwa ajili ya uhitaji wa mwaka. Nakala moja hujazwa kila mwezi na kutumwa kwenye afisi. S-1 haifanyiwi nakala ya pili. Badala yake, munaweza kujaza S-21 tatu: moja kwa ajili ya utendaji wa wahubiri, moja kwa ajili ya mapainia wasaidizi na ingine kwa ajili ya mapainia wa kawaida.

◆ Za kutumiwa kikawaida: ­M-202, S-12, S-13, S-19, S-9.

◼ Kosa linapofanywa wakati wa kujaza fomu, ni vizuri zaidi kulisahihisha kwenye fomu ileile. Fomu hazipaswi kutumiwa kwa kutuma barua au kama karatasi ya ovyo. Makutaniko ambayo bado hayajapata stoki yazo ya mwaka ya fomu yanaombwa kuendelea kusubiri. Watatumiwa stoki hiyo karibuni.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine