Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea mnamo Februari: Kila kitabu chenye kurasa 192 kilichotangazwa kabla ya 1985 kilicho katika stoki ya kutaniko. Makutaniko yasiyokuwa nacho katika stoki yataweza kutolea kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Machi: Ufunuo: Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Aprili: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada za pekee zitafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Mei: Mnara wa Mlinzi na Amkeni!
◼ Kwa wahubiri wote waliobatizwa watakaokuwako wakati wa mkutano wa utumishi wa juma toka Februari 2, hati “Instructions médicales/Pas de sang” na kadi za utambulisho kwa ajili ya watoto wao zitatolewa.
◼ Mapainia wasaidizi wasiofikisha kiwango cha saa kinachoombwa hawataweza kuhesabiwa kwa vyovyote juu ya ripoti ya kutaniko inayotumwa kwenye afisi. Ikiwa wazo hili halifuatwi, wastani ya nchi yote utakuwa chini ya saa 60.
◼ Kuanzia Februari au Machi 1 ikiwa ni nyuma, waangalizi wasafiri watatoa hotuba mpya ya watu wote yenye kichwa: “Je! Wewe Unalo Wazo la Mungu Juu ya Uhai?”
◼ Makutaniko yatachukua mipango yenye kutenda kazi kwa ajili ya Ukumbusho utakaoazimishwa mwaka huu Siku ya Posho, Aprili 11, baada ya jua kutua. Kupitishwa kwa mifano hakupaswi kuanza isipokuwa baada ya jua kutua, ingawa hotuba inaweza kuanza mapema. Chunguzeni saa ya kutua kwa jua katika eneo lenu. Ni vizuri kwamba makutaniko yaadhimishe Ukumbusho katika mahali tofauti, ijapokuwa hilo halifanyiki sikuzote. Mahali ambapo makutaniko mengi hufanya mikutano katika Jumba la Ufalme moja, itawezekana labda kwamba moja au mengi ya makutaniko hayo yaweze kutumia majengo mengine jioni hiyo. Ukumbusho haungepaswa kuanza nyuma kwa kiasi cha kuvunja moyo watu ambao wanapendezwa na ukweli tangu hivi karibuni. Kwa upande mwingine, haingefaa kwamba programu iwe yenye kusongwa sana hivi kwamba hakungekuwa wakati wa kutosha kabla na baada ya mwadhimisho ili kusalimu waalikwa, kutolea wamoja msaada wa kiroho wenye kufuatishwa, na kutiana moyo wamoja na wengine. Baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote yanayohusika, wazee wataamua jambo linalostahili kufanya ili kuwezesha wote watakaokuja kwenye Ukumbusho kupata faida zote iwezekanavyo kutokana na huo.
◼ Hotuba ya pekee inayopangwa wakati wa Ukumbusho itatolewa Siku ya Yenga, Machi 29. Muhtasari utatolewa. Makutaniko yaliyo na ziara ya mwangalizi wa mzunguko, mkusanyiko wao wa mzunguko au mkusanyiko wao wa pekee wa siku moja juma hilo yataweza kusikiliza hotuba ya pekee juma lifuatalo. Hakuna kutaniko litakalopanga hotuba hiyo kabla ya Machi 29, 1998.
◼ Baraza la wazee lingepaswa kutambua kwamba ni jambo la lazima kufanya mabadiliko yafuatayo wakati kutaniko linahudhuria kwenye kusanyiko: juma la mkusanyiko wa pekee wa siku moja, mikutano ya kutaniko ingepaswa kufanyika kama kawaida, isipokuwa mkutano wa watu wote na funzo la Mnara wa Mlinzi itakayoondolewa. Juma la mkusanyiko wa mzunguko, kutaniko litaondoa pia Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na mkutano wa utumishi; funzo la kitabu tu ndilo litakalofanyika juma hilo.
◼ Kuanzia juma toka Mei 4, 1998, na kufikia lile toka Septemba 14, 1998, kitabu Biblia: Neno la Mungu au la Binadamu? kitachunguzwa katika mafunzo ya kitabu ya makutaniko yanayozungumza Kifaransa.