Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/98 uku. 7
  • “Yehova Ni Msaidiaji Wangu”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Yehova Ni Msaidiaji Wangu”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Uwe Hodari na Mwenye Nguvu Sana”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Kuwa Hodari Haiko Nguvu Sana
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
  • “Upendo Wenye Kristo Iko nao Unatulazimisha”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Tufuate Mufano wa Yesu: Tukuwe na Uhodari na Utambuzi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 3/98 uku. 7

“Yehova Ni Msaidiaji Wangu”

1 Yesu alipowapa wanafunzi wake wa kwanza kazi ya kuhubiri, aliwaambia: “Tazama! Mimi ninawatuma nyinyi kama kondoo katikati ya mbwa-mwitu.” (Mt. 10:16) Je! hata hivyo walikuwa waoga na kujizuiza kuhubiri? Hapana. Walitenda kwa njia ambayo mtume Paulo alieleza baadaye kwa Wakristo wenzake: “Tupate kuwa wenye moyo mkuu na kusema: ‘Yehova ni msaidiaji wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunifanya nini?’ ” (Ebr. 13:6) Walishangilia kwa kuwa walihesabiwa wenye kustahili kuvunjiwa heshima kwa ajili ya jina la Yesu, na waliendelea bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema.​—Mdo. 5:41, 42.

2 Leo, kazi ya kuhubiri inayofanywa katika dunia nzima inakuwa katika sehemu yake ya umalizio. Sawasawa kama Yesu alivyotangaza, sisi ni vitu vya kuchukiwa na mataifa yote. (Mat. 24:9) Mahubiri yanapambana na upinzani, yanadhihakiwa na hata kupigwa marufuku katika mahali fulani duniani. Ikiwa tungekosa imani, tungeweza kuogopeshwa. Hata hivyo, jambo la kujua kwamba Yehova ni msaidiaji wetu na kwamba anatutolea nguvu linatia nguvu azimio letu la kudumu.

3 Kuwa hodari ni kuwa mwenye nguvu, kuwa jasiri na shujaa. Ni kinyume cha hofu, haya na woga. Wanafunzi wa Yesu walihitaji sikuzote uhodari ili kuvumilia. Ni jambo la muhimu kwamba tuwe hodari ili kwamba tusijiache kushindwa na mienendo na matendo ya ulimwengu ulio adui wa Mungu. Ni jambo lenye kutia moyo kama nini kutafakari juu ya kielelezo cha Yesu, ambaye alishinda Ulimwengu! (Yn. 16:33) Acheni pia tukumbuke mitume ambao, walipokabili majaribu makali, walisema kwa ujasiri: “Lazima sisi tumtii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.”​—Mdo. 5:29.

4 Sisi Si Namna ya Wale Warudiao Nyuma: Tunapaswa kujitahidi kulinda maoni yenye kutazamia mema ya kazi yetu. (Ebr. 10:39) Tusisahau kwamba ni Yehova anayetutuma katika upendo wake na rehema yake kwa wanadamu wote kwa ujumla. Yeye haombi kamwe watumishi wake kufanya jambo lolote lisilotumikia kusudi lenye mafaa. Yote tuliyo nayo ya kufanya itakuwa mwishowe kwa faida ya wale wanaompenda Mungu.​—Rom. 8:28.

5 Maoni yenye kutazamia mema yatatusaidia tuendelee kutafuta watu wenye mfano wa kondoo katika eneo letu. Tungeweza kuona ubaridi wa watu kuwa uthibitisho wa kuvunjika kwao moyo na kukosa kwao tumaini. Upendo na utufanye kuwa wasikivu na wenye subira! Kila wakati tunapoacha kichapo au tunapotambua kupendezwa kwa kiasi fulani, tungepaswa kuwa na mradi wa kufanya haraka ziara ya kurudia ili kukomaza kupendezwa huko. Hatupaswi kamwe kushakia uwezo wetu wa kuanzisha funzo la Biblia au kuongoza moja. Badala yake, inatuomba kutafuta kwa ukawaida katika sala tegemezo na mwongozo wa Yehova, tukiwa hakika kwamba atatusaidia.

6 Tuna uhakika kwamba Yehova ataongoza kazi kwenye umalizio wake. (Ona Wafilipi 1:6.) Yehova ni msaidiaji wetu, tumaini letu kamili katika yeye linatutia nguvu ili kwamba ‘tusife moyo katika kufanya lililo bora.’​—Gal. 6:9.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine