Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea mnamo Septemba: Broshua yoyote yenye kurasa 32 kati ya zifuatazo: Je! Kweli Mungu Anatujali?; Doit-on croire à la Trinité ?; Serikali Itakayoleta Paradiso; Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. . . ; Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?; Kuishi Milele Duniani Katika Furaha! Ikiwa hilo linafaa, broshua zifuatazo zinaweza kutumiwa: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?; Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?; Nos problèmes — Qui nous aidera à les résoudre?; Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote. Oktoba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Novemba: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ikiwa mtu anaonyesha kupendezwa wakati wa ziara za kurudia, itawezekana kumtolea uandikishaji. Desemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.
◼ Kila kutaniko lilipokea fomu tatu Inventaire des publications (S(d)-18). Je! mmekwisha kurudisha nakala kwenye ofisi?
◼ Makutaniko yataanza kutoa maombi ya Kalenda ya Mashahidi wa Yehova 1999 kwenye ombi la vichapo la Septemba.
◼ Halmashauri ya Utumishi ya kutaniko itachunguza bila kukawia Maombi yote ya kukubaliwa katika utumishi wa painia wa kawaida. Halmashauri hiyo haitachunga ombi ili kuangalia ikiwa mwenye kutaka kuwa painia anao uwezo wa kufikia mradi wa saa. Tarehe ya kuwekwa yaweza kubadilishwa mara moja ikiwa ombi lapokewa baada ya tarehe iliyoombwa na mwenye kutaka kuwa painia. Kuwekwa kunakoanzia kwenye tarehe ambayo imekwisha kupita hakufanywi, isipokuwa kama hali za pekee zinaomba hivyo. Wakati huo, barua inapaswa kuongezwa kwenye ombi.
◼ Kitabu Biblia: Neno la Mungu au la Binadamu? kitakapomalizwa, broshua zitachunguzwa mfululizo kwenye mafunzo ya kitabu ya kutaniko. Tangazo la Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 1998 lilisema kwamba tungeanza kujifunza broshua Anataka kuanzia juma la Septemba 21. Hiyo itafuatwa na uchunguzi wa broshua ambazo mtajulishwa kupitia barua.