Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea mnamo Oktoba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Novemba: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ikiwa mtu anaonyesha kupendezwa wakati wa ziara za kurudia, itawezekana kumtolea uandikishaji.adaptation RDC Desemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.
◼ Wazee watakuwa macho ili kufuata maagizo ya Mnara wa Mlinzi wa Aprili 1, 1991, kurasa 21-3, kuhusiana na mtu aliyetengwa au aliyejitenga na ambaye anataka kurudishwa.
◼ Watu wanaoshirikiana na kutaniko wanapaswa kutuma kupitia hili uandikishaji au uandikishaji wa kurudilia wowote kwa Mnara wa Mlinzi au Amkeni!, kutia ndani uandikishaji wao wenyeewe.
◼ Sosaiti haishughulikii maombi ya binafsi ya wahubiri wanaoomba vichapo. Mwangalizi-msimamizi atapanga kwamba tangazo lifanywe kila mwezi kabla ya kutuma ombi la vichapo la kutaniko kila mwezi kwenye Ofisi. Jambo hilo litafanya iwezekane kwa wote wanaotaka kupata vichapo kumjulisha ndugu anayeshughulika na vichapo. Tafadhali, kumbukeni ni vichapo gani vinavyofanyiwa ombi la pekee.
◼ Katika stoki, Sosaiti inayo mabuku ya Mnara wa Mlinzi katika Kifaransa ya 1950-55, 57, 61, 63, 64, 67, 75-81, 83-89, 91, 96 na pia mabuku ya Amkeni! katika Kifaransa ya 90, 92-96. Vilevile, Vitabu-Mwaka katika Kifaransa vya miaka ifuatayo: 77, 88, 93, 95-98. Wahubiri au makutaniko mapya wanaotaka kuyapata wanaweza kuyaomba tangu sasa kwa ndugu anayeshughulika na vichapo. (Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 1997, Majibu kwa Maulizo Yenu; Mnara wa Mlinzi wa Novemba 1, 1994, kur. 28-31.)
◼ Tunataka kuwajulisha kwamba mtahudumiwa kwa kupelekewa trakti mlizoagiza zikiwa pamoja na bei inayolingana na pakiti ya trakti mia moja moja, zikiwa chache. (Ona S-15) Ikiwa kiwango si barabara, labda kinapozidi au kupungua, tafadhali msitume malalamiko. Hilo litarahisisha kazi ya idara ya usafirishaji.
◼ Tunataka kuvuta uangalifu wenu juu ya jinsi ya kufanya kuhusiana na matumizi mazuri ya hotuba za watu wote mnazoandaliwa: (1) Mwangalizi-msimamizi anapaswa kuweka faili ya wakati wote ya mihtasari yote. (2) Anapaswa kutoa nakala ya muhtasari kwa msemaji. (3) Hotuba ileile moja inaweza kutolewa na wasemaji tofauti. (4) Tieni, tafadhali, katika faili yenu mihtasari mipya inayotumwa kwenu kama ilivyopangwa na Sosaiti.