Wanaweza Kuona Kwamba Sisi Ni Tofauti
1 Mwaka uliopita, zaidi ya wapya 300 000 walijiunga nasi kwa kubatizwa. Ni mambo gani watu hao waliyoyaona katika Mashahidi wa Yehova ambayo yalifanya watake kuwa sehemu ya tengenezo la Mungu? Kwa nini sisi tunajitokeza kuwa tofauti na dini nyinginezo? Yafuatayo ni baadhi ya majibu ya waziwazi:
—Tunashikamana na Biblia badala ya maoni yetu binafsi: Tunamwabudu Yehova Mungu “kwa roho na kweli,” kama Yesu alivyotuomba kufanya. Hilo limemaanisha kutupilia mbali uwongo wa kidini na kukubali Neno la Mungu lililoandikwa.—Yn. 4:23, 24; 2 Tim. 3:15-17.
—Tunawaendea watu badala ya kungoja wao watujie: Tumekubali amri ya Kristo ya kuhubiri na kufundisha, na tunaiga kielelezo chake cha kutafuta watu wenye moyo mnyofu. Tunawatafuta nyumbani kwao, barabarani, au mahali popote wawezapo kupatikana.—Mt. 9:35; 10:11; 28:19, 20; Mdo. 10:42.
—Tunatoa mafundisho ya Biblia kwa kila mtu bila malipo: Tunatumia mali na nishati zetu bila kudai lolote, tukipitisha zaidi ya saa bilioni (miliari) moja kila mwaka katika utumishi wa Mungu. Bila upendeleo, tunajifunza Biblia na aina zote za watu.—Mt. 10:8; Mdo. 10:34, 35; Ufu. 22:17.
—Tunazoezwa vizuri kusaidia watu kiroho: Kupitia funzo letu la binafsi la Biblia na mafundisho yanayotolewa kupitia mikutano ya kutaniko, makusanyiko na mikusanyiko, tunapewa maarifa ya kitheokrasi yenye manufaa na yenye kuendelea yanayofanya iwezekane kwetu kuwapa wengine nuru ya kiroho.—Isa. 54:13; 2 Tim. 2:15; 1 Pet. 3:15.
—Tunachukua kweli kwa uzito, tukiitumia katika maisha yetu ya kila siku: Kwa sababu ya upendo wetu kwa Mungu, tunafanya mabadiliko, tukifanya maisha yetu yapatane na mapenzi yake. Utu wetu mpya ulio kama ule wa Kristo huvuta wengine kwenye kweli.—Kol. 3:9, 10; Yak. 1:22, 25; 1 Yn. 5:3.
—Tunajitahidi kuishi na kutumika na wengine kwa amani: Kusitawisha sifa za kimungu hutusaidia tujihadhari na matendo yetu na usemi wetu. Sisi ‘tunatafuta sana amani na kuifuatia’ katika mahusiano na watu wote.—1 Pet. 3:10, 11; Efe. 4:1-3.
2 Vielelezo vya maisha ya Kikristo ambavyo watu huona katika tengenezo la Yehova huchochea wengi wakubali kweli. Kielelezo chetu binafsi na kiwe na uvutano uohuo juu ya wale wanaotujua na kututazama.