Matangazo
◼ Toleo la Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichotangazwa kabla ya 1985 ambacho huenda kutaniko likawa nacho katika stoki. Makutaniko yasiyokuwa na vitabu hivyo yatatolea watu La paix et la sécurité véritables: comment est-ce possible? au Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Februari: Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Aprili: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Iweni na akiba ya broshua Anataka kwa ajili ya wale wenye kupendezwa, na jitahidini kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani.
◼ Nyongeza ya toleo hili la Huduma Yetu ya Ufalme kuhusu kusanyiko la wilaya 1999 itachunguzwa katika Mkutano wa Utumishi juma toka Desemba 28, 1998.
◼ Wahubiri wote wenye kubatizwa watakaokuwako kwenye Mkutano wa Utumishi juma toka Januari 4 watapewa “Instructions médicales/Pas de sang” na kadi ya utambulisho kwa ajili ya watoto wao.
◼ Kuanzia Februari, na ikiwa ni kuchelewa Machi 1, hotuba mpya ya watu wote itakayotolewa na waangalizi wa mzunguko itakuwa “Mungu Ni Halisi Kadiri Gani Kwako?”
◼ Makutaniko yanapaswa kufanya mipango ili yaadhimishe Ukumbusho mwaka huu Siku ya Nne, Aprili 1, baada ya jua kutua. Ingawa hotuba inaweza kuanza mapema, kupitishwa kwa mifano ya Ukumbusho hakupaswi kuanza isipokuwa baada ya jua kutua. Chunguzeni pamoja na wapasha-habari wa hapo kwenu kusudi mwamue ni wakati gani jua linapotua huko. Ingawa ni vizuri kwamba kila kutaniko lifanye mwadhimisho wake wa Ukumbusho, jambo hilo haliwezekani sikuzote. Mahali ambapo makutaniko mengi hutumia kwa kawaida Jumba la Ufalme lilelile, labda kutaniko moja au mengi yanaweza kutumia nyumba nyingine jioni hiyo. Mahali ambapo hili lawezekana, tunashauri kwamba kuweko kipindi cha angalau dakika 40 kati ya programu mbalimbali ili kutoa nafasi ya kusalimia wageni, kutia moyo wale waliopendezwa karibuni, na kufaidika kikamili na tukio hilo. Tatizo la kufika na kuegeshwa kwa magari, kutia ndani kushushwa na kupakiwa kwa wasafiri lapaswa pia liangaliwe. Baraza la wazee lingepaswa kuamua juu ya mipango ambayo ingekuwa bora zaidi katika kutaniko lenu. Kwa kuwa Ukumbusho ni jioni ya pekee kwa ajili ya kutafakari yale ambayo Yehova na Yesu wametufanyia, lingekuwa jambo lisilofaa kuugeuza kuwa wakati wa sikukuu ya kula na kunywa.
◼ Hotuba ya pekee ya watu wote katika majira ya Ukumbusho wa 1999 itatolewa Siku ya Yenga, Aprili 18. Kichwa cha hotuba kitakuwa “Urafiki Pamoja na Mungu na Jirani.” Mtapata muhtasari. Makutaniko yatakayokuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko, mkusanyiko wa mzunguko, au mkusanyiko wa pekee wa siku moja mwisho-juma huo yatafanya hotuba ya pekee juma lenye kufuata. Hakuna kutaniko ambalo litafanya hotuba hiyo kabla ya Aprili 18, 1999.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Kifaransa: Index des publications de la Société 1996.