Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/99 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Ya Februari

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mikutano Ya Utumishi Ya Februari
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 2/99 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Ya Februari

Juma Toka Februari 1

Wimbo 154

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Kumbusha wote watoe ripoti ya utumishi ya Januari.

Dak. 17: “Toleeni Watu wa Umri Zote Kitabu Furaha ya Familia.” Mzee mmoja na wahubiri wawili au watatu wenye uwezo wanazungumzia makala. Tia mkazo juu ya mradi wa kusaidia wengine watambue kwamba siri ya kupata furaha ya familia hupatikana katika kufuata shauri la Biblia. (Ona Furaha ya Familia, kur. 9-​12.) Fanyeni onyesho la moja kati ya utoaji mbalimbali uliopendekezwa. Onyesha jinsi ya kusema juu ya bei adaptation RDC na jinsi ya kufanya mipango [W set up vt 11] kwa ajili ya ziara ya kurudia.

Dak. 18: “Kuvaa Utu Mpya.” Hotuba inayochanganua Waefeso 4:​20-​24. (Ona Mnara wa Mlinzi wa Machi 1, 1993, kur. 14-​18, maf. 4-​17.) Fasiria jinsi tunavyovua utu wa hapo zamani na kuvaa utu mpya.

Wimbo 4 na sala ya mwisho.

Juma Toka Februari 8

Wimbo 12

Dak. 10: Matangazo. Hali ya akaunti.

Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.

Dak. 20: “Muumba Wetu Mtukufu Anatujali!” Maulizo na majibu. Fasiria jinsi kitabu Muumba kinavyoweza kutumiwa ili kusaidia wale wanaoshakia au wanaokana kuwako kwa Mungu. Ingawa hicho si kitabu cha kuongoza mafunzo ya Biblia, kinaweza kutumika kama kifaa chenye matokeo katika kuchochea watu wachunguze yale yote ambayo Biblia husema. (Ona kitabu Muumba, kur. 189-​91.) Alika wahubiri washiriki hisia zao binafsi kuhusu kichapo hicho na waeleze mambo yoyote yaliyoonwa ambayo wamepata katika kukiangushia wengine.

Wimbo 173 na sala ya mwisho.

Juma Toka Februari 15

Wimbo 40

Dak. 10: Matangazo.

Dak. 18: Tunafaidikaje kwa Kujiandikisha Katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji, yakiongozwa na mwangalizi wa shule. Shule haina kusudi tu la kuzoeza watu katika kusema peupe. Tunafaidika moja kwa moja katika njia nyinginezo pia. (Ona Kiongozi cha Shule, kur. 12-​13.) Tunajifunza jinsi ya kuwasiliana vizuri zaidi na watu wengine. Tunafundishwa kusema wazi, kwa utulivu na kwa uhakika. Tunakuwa wenye ustadi zaidi katika kujibu maulizo kuhusu imani yetu na katika kufasiria maamuzi yetu yenye msingi katika Biblia. Ujuzi wetu wa Biblia huongezeka, jambo linalotusaidia tuwe wenye matokeo zaidi katika kutoa ushahidi kwa wengine. Tunajifunza kutambua makosa yetu na kukubali shauri, jambo linalotuzoeza kushughulika na wengine kwa upole zaidi. Mazoezi yote ambayo shule huandaa yanatusaidia tubaki wenye ‘kustahilishwa vya kutosha’ kuwa wahudumu wa Mungu.​—2 Kor. 3:​5, 6.

Dak. 17: “Jinsi Washiriki wa Familia Wanavyofanya Kazi Pamoja ili Kushiriki Kikamili​—Katika Funzo la Biblia.” Mazungumzo yatakayofanywa na kikundi cha familia. Wanachanganua jinsi wanavyotumia madokezo kuhusu usomaji wa Biblia na funzo katika familia, madokezo yanayopatikana katika Mnara wa Mlinzi wa Mei 15, 1996, kur. 14-15, na Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 15, 1992, kur. 16-17.

Wimbo 57 na sala ya mwisho.

Juma Toka Februari 22

Wimbo 170

Dak. 10: Matangazo.

Dak. 15: “Majibu ya Maulizo Yenu.” Maulizo na majibu. Onyesha kwamba Ukumbusho ni sherehe ya kuadhimisha kwa heshima na kwa furaha. Haifai kuiga sikukuu za Jumuiya ya Wakristo.

Dak. 20: Jinsi ya Kupata Shangwe Katika Kufanya Wanafunzi. Hotuba iliyo na msingi juu ya Mnara wa Mlinzi wa Februari 15, 1996, kur. 19-​22.

Wimbo 91 na sala ya mwisho.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine