Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/99 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Ya Machi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mikutano Ya Utumishi Ya Machi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 3/99 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Ya Machi

Juma Toka Machi 1

Wimbo 33

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme.

Dak. 17: “Mwadhimisho wa Ulimwenguni Pote wa Kifo cha Kristo.” Maulizo na majibu. Tia ndani maelezo juu ya Mnara wa Mlinzi wa Februari 1, 1997, kur. 11-12, maf. 10-14. Tia mkazo juu ya jinsi upendo mkubwa wa Yehova ulivyomsukuma aandae fidia kwa ajili yetu.

Dak. 20: Sababu Zenye Kushurutisha Kuwa Mapainia Wasaidizi Mnamo Aprili na Mei. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji, yanayoongozwa na mwangalizi wa utumishi na yanayosihi wote wafikirie kwa uzito kuwa mapainia wasaidizi. Rudilieni marekebisho ya saa zinazoombwa kwa mapainia wa kawaida na wasaidizi, kama yanavyoonyeshwa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 1999, ukurasa 7. Marekebisho hayo yangepaswa kuwezesha wengi zaidi wafurahie pendeleo la utumishi wa wakati wote. Fasiria jinsi uthamini wetu kuhusu dhabihu ya Kristo unavyotushurutisha tujikakamue katika kuhubiria wengine. (2 Kor. 5:​14, 15) Mwaka huu, Ukumbusho utafanyika tarehe ya kwanza ya Aprili. Ni kichocheo kizuri kama nini kwa wahubiri wote wa Ufalme kutoa mwezi mzima katika utendaji wa utumishi wenye kuzidishwa! Rudilia mambo makuu yaliyochaguliwa kutoka nyongeza za Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1997 na Aprili 1998, zinazozungumzia utumishi wa painia msaidizi. Fikiria njia za kufanya programu za kielelezo tulizotolewa zipatane na hali. Rudilia mipango ya utumishi katika kutaniko lenu, mipango inayotoa nafasi kubwa ya kushiriki katika huduma pamoja na wengine. Tia moyo wahubiri wachukue fomu za maombi ya utumishi wa painia msaidizi baada ya mkutano.

Wimbo 44 na sala ya mwisho.

Juma Toka Machi 8

Wimbo 52

Dak. 10: Matangazo. Hali ya akaunti.

Dak. 20: “Waalikeni Waje.” Maulizo na majibu. Tia mkazo juu ya uhitaji wa sikuzote wa kuongoza kwenye mikutano ya kutaniko wale waliopendezwa hivi karibuni. Fanyeni onyesho la mazungumzo pamoja na mtu mwenye kupendezwa, mkitumia habari katika kitabu Ujuzi, uku. 159, fu. 20, na kur. 162-3, maf. 5-8. Tia moyo kila mmoja afanye jitihada ya pekee ili kusaidia wanafunzi wa Biblia na wengine wanaopendezwa wahudhurie Ukumbusho mnamo Aprili 1. Onyesha nakala ya mwaliko, na ufasirie jinsi huo unavyoweza kutumiwa kwa matokeo. Wote wangepaswa kuanza kugawa mialiko kwa ajili ya Ukumbusho juma hili.

Dak. 15: “Jinsi Washiriki wa Familia Wanavyofanya Kazi Pamoja ili Kushiriki Kikamili​—Katika Mikutano ya Kutaniko.” Mazungumzo yanayofanywa na kikundi cha familia. Huku wakitoa maelezo juu ya mambo makuu ya makala, wanazungumzia jinsi wanavyoweza kujitayarisha kwa ajili ya mikutano wakiwa familia. Wanazungumzia njia wanazoweza kutumia ili wasaidiane kushiriki na kile kinachapasa kufanywa ili familia ifike kwenye mikutano pa wakati.

Wimbo 62 na sala ya mwisho.

Juma Toka Machi 15

Wimbo 56

Dak. 10: Matangazo. Chunguza “Je! Utahudhuria?”

Dak. 15: “Watumishi wa Huduma Hutoa Utumishi Wenye Thamani.” Hotuba inayotolewa na mtumishi wa huduma mwenye ustadi. Rudilia mambo makuu yanayozungumziwa katika kitabu Huduma Yetu, kur. 57-9. Fasiria jinsi watumishi wa huduma wanavyotumiwa kwenu ili kusaidia kutaniko.

Dak. 20: Tufurahie Kitabu-Mwaka 1999. Mazungumzo kati ya mume na mke. Mume afasiria kwamba Kitabu-Mwaka kilitangazwa katika umbo la kitabu kwa mara ya kwanza mnamo 1927 na kwamba kwa zaidi ya miaka 70, ripoti ya ulimwenguni pote ya Mashahidi wa Yehova imekuwa ikitiwa ndani. Wanarudilia mambo makuu ya “Jumla Kuu za 1998,” kwenye ukurasa 31. Kisha wanazungumzia “Barua Kutoka Baraza Linaloongoza,” kwenye kurasa 3-5, na wanatoa maelezo juu ya jinsi watakavyotenda kuhusiana na kitia-moyo kinachotolewa.

Wimbo 68 na sala ya mwisho.

Juma Toka Machi 22

Wimbo 162

Dak. 10: Matangazo. Tangaza majina ya wale watakaokuwa mapainia wasaidizi mnamo Aprili. Fasiria kwamba haijakuwa nyuma mno kujaza ombi. Onyesha programu nzima ya mikutano kwa ajili ya utumishi, mikutano inayopangwa kufanywa mnamo Aprili. Tia moyo wote wafuate usomaji wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho, usomaji unaopangwa toka Machi 27-Aprili 1, kama inavyoonyeshwa katika Kuyachunguza Maandiko Kila Siku​—1999 na kwenye kalenda ya 1999.

Dak. 15: Jitayarisheni kwa Ajili ya Ukumbusho. Hotuba. Wote wangepaswa kufanya mipango ili kusaidia wanafunzi wa Biblia na wengine wanaopendezwa wahudhurie Ukumbusho. Huenda wapya wanaohudhuria wasielewe ni nani anayeweza kushiriki mifano au maana ya mwadhimisho huo. Rudilia yale yanayosemwa katika Mnara wa Mlinzi wa Aprili 1, 1996, kur. 6-8, na uonyeshe jinsi tunavyoweza kusaidia mtu aliyependezwa hivi karibuni aelewe maana na kusudi la mwadhimisho huo. Malizia kwa kurudilia “Mambo ya Kutosahau kwa Ajili ya Ukumbusho” na kuonyesha mipango mliyoifanya kwa ajili ya Ukumbusho.

Dak. 20: Jambo Gani Hutufikia Tunapokufa? Mzee mmoja na wahubiri wawili au watatu wenye ustadi wanazungumzia manufaa na matumizi ya broshua hiyo. Tulijua broshua hiyo vizuri zaidi tulipojifunza hiyo kwenye Funzo la Kitabu. Je! tunaitumia kwa matokeo katika utumishi wa shambani? Ndugu wanaoshiriki mazungumzo wanahojiana: Kwa nini watu wengi ni wenye kupendezwa na habari hiyo? Kinyume na fundisho la kidini la uwongo, broshua hiyo yakazia tumaini gani? Tunawezaje kutumia maulizo kwenye jalada ya mwisho ili kuamsha kupendezwa? Ni fursa gani zinazopatikana ili kutolea watu broshua hiyo. Fanyeni onyesho moja la utoaji kwa kutumia maandiko katika fungu 14 kwenye ukurasa 27. Tia moyo wote wawe tayari kufanya matumizi mazuri ya broshua hiyo.

Wimbo 92 na sala ya mwisho.

Juma Toka Machi 29

Wimbo 111

Dak. 12: Matangazo. Kumbusha wote watoe ripoti zao za utumishi za Machi. Mnamo Aprili, tutatolea watu Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Onyesha namba za karibuni za magazeti hayo, toa dokezo la makala yanayoweza kukaziwa, na utaje baadhi ya mambo ya pekee yenye kupendeza. Wote wangepaswa kuchukua broshua Anataka na kuitumia ili kuanzisha mafunzo ya Biblia pamoja na watu wenye kupendezwa

Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.

Dak. 18: Tunapaswa Kuitikiaje Shauri? Hotuba inayotolewa na mzee. Sisi sote twatolewa shauri kuhusu mwelekeo wetu, mwenendo wetu, mashirika yetu au kushiriki katika utendaji wa kutaniko. Mara kwa mara, twaelekea kupinga shauri au kuhuzunishwa. Kuwa tayari kukubali na kutumia shauri kwaweza kuwa jambo la maana katika hali yetu njema ya kiroho. Rudilia mambo ya lazima yanayotia mkazo juu ya sababu ambazo zingepaswa kutuchochea tukubali na kuthamini shauri.​—Ona Mnara wa Mlinzi wa Aprili 1, 1987, kurasa 27-30.

Wimbo 118 na sala ya mwisho.

[DO NOT SET] References

1. jp 112

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine