Programu ya shule ya huduma ya kitheokrasi ya 2000
Maagizo
Mnamo 2000, Shule ya Huduma ya Kitheokrasi itaendeshwa kulingana na mipango ifuatayo.
VICHAPO: Migawo itatoka katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo [bi7-SW], Mnara wa Mlinzi [w-SW], “Kila Andiko Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa” (Chapa ya 1990) [si-SW], Étude perspicace des Écritures [it-1-F na it-2-F], na “Vichwa vya Biblia vya Mazungumzo” kama vinavyopatikana katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo [td-SW].
Shule ingepaswa kuanza PA WAKATI kwa wimbo, sala, na maneno mafupi ya ukaribishaji. Hakuna uhitaji wa kuonyesha kimbele yale yaliyo juu ya programu. Kadiri mwangalizi wa shule anavyotoa utangulizi wa kila sehemu, yeye atataja kichwa cha habari kitakachozungumziwa. Fuata utaratibu ufuatao:
MGAWO Na. 1: dakika 15. Huu ungepasa kutolewa na mzee au mtumishi wa huduma, na habari yake itatokana na Mnara wa Mlinzi au “Kila Andiko Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa.” Wakati unapotokana na Mnara wa Mlinzi, mgawo huu ungepasa kutolewa kama hotuba ya maagizo ya dakika 15 bila kujikumbusha kwa mdomo; wakati unapotokana na kitabu “Kila Andiko,” huo ungepasa kutolewa kama hotuba ya dakika 10 hadi 12, ikifuatwa na kujikumbusha kwa mdomo kwa dakika 3 hadi 5 kwa kutumia maulizo yaliyochapwa katika kichapo. Lengo halingepaswa kuwa kuzungumzia tu habari lakini kukaza uangalifu juu ya matumizi yenye kufaa ya habari inayozungumziwa, huku ikikazia lile litakalokuwa lenye kusaidia zaidi kwa kutaniko. Kichwa kinachoonyeshwa kingepasa kutumiwa.
Ndugu wanaogawiwa hotuba hii wangepaswa kuwa waangalifu ili kuheshimu wakati. Shauri la faraghani linaweza kutolewa ikiwa hilo lahitajiwa au ikiwa laombwa na msemaji.
MAMBO MAKUU KUTOKA USOMAJI WA BIBLIA: dakika 6. Mgawo huu ungepasa kutolewa na mzee au mtumishi wa huduma ambaye, kwa matokeo, atatumia habari kulingana na mahitaji ya kutaniko. Hakuna kichwa cha habari kinachohitajiwa. Huo haungepaswa kuwa tu kifupi cha usomaji uliotolewa kuwa mgawo. Kusema kwa kifupi muda wa sekunde 30 hadi 60 mambo yote yaliyo katika sura zilizotolewa kuwa mgawo kunaweza kutiwa ndani. Hata hivyo, lengo kubwa ni kusaidia wasikilizaji waelewe kwa nini na namna gani habari hiyo ilivyo yenye faida kwetu. Kisha, mwangalizi wa shule ataambia wanafunzi waende katika madarasa yao mbalimbali.
MGAWO Na. 2: dakika 5. Huu ni usomaji wa Biblia wa habari iliyotolewa kuwa mgawo, ambayo itatolewa na ndugu. Hilo litatumika katika shule kubwa na katika yale madarasa ya ziada. Mara nyingi, migawo ya usomaji ni mifupi vya kutosha ili kuruhusu wanafunzi watoe habari fupi ya mafasirio katika maneno ya utangulizi na ile ya umalizio. Hali ya kihistoria, maana ya kiunabii au ya kimafundisho, na matumizi ya kanuni vinaweza kutiwa ndani. Mistari yote iliyotolewa kuwa mgawo ingepasa kusomwa bila kukatizwa. Bila shaka, mistari ya kusoma inapokuwa haifuatani, mwanafunzi anaweza kutaja mstari ambako usomaji unaendelea.
MGAWO Na. 3: dakika 5. Dada atagawiwa sehemu hii. Habari kwa ajili ya utoaji huu itatokana na “Vichwa vya Biblia vya Mazungumzo” kama vinavyopatikana katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Kikao kinaweza kuwa mahubiri ya vivi hivi, ziara ya kurudia, au funzo la Biblia la nyumbani, na washiriki wanaweza kukaa au kubaki wima. Mwangalizi wa shule atapendezwa zaidi na jinsi mwanafunzi anavyozungumzia kichwa kilichotolewa kuwa mgawo na jinsi anavyosaidia mwenye-nyumba afikiri juu ya maandiko. Mwanafunzi anayegawiwa sehemu hii angepaswa kujua kusoma. Mwangalizi wa shule atapanga kuwe msaidizi mmoja, lakini msaidizi mwingine wa ziada anaweza kutumiwa. Matumizi yenye matokeo ya Biblia ingepasa kufikiriwa kwanza, si kikao.
MGAWO Na. 4: dakika 5. Habari kwa ajili ya mgawo huu itakuwa na msingi juu ya mtu wa kibiblia, au “Vichwa vya Biblia vya Mazungumzo” kama vinavyopatikana katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Wakati mgawo unapokuwa na msingi juu ya mtu wa kibiblia, habari inaweza kupatikana chini ya jina la yule mtu wa kibiblia katika kitabu Étude perspicace. Mwanafunzi angepaswa kujifunza mitajo ya Kimaandiko katika habari ili kuwa na picha iliyo wazi ya mtu wa kibiblia—matukio ya maisha yake, na utu wake, tabia zake, na mtazamo wake. Baadaye, mwanafunzi angepaswa kuzungumzia kichwa kilichotolewa kuwa mgawo na kuchagua maandiko yenye kufaa ili kuyatumia. Maandiko ya ziada yenye kukazia kanuni za Biblia, ambayo hupatana na kichwa yanaweza kutiwa ndani. Kusudi la kuzungumzia mtu wa kibiblia ni kuonyesha kile tunachoweza kujifunza kutokana na mfano wake. Vitendo vya uamanifu, ujasiri, unyenyekevu, na kutokuwa na ubinafsi vinatutolea mifano mizuri ya kufuata; vitendo vya ukosefu wa uamanifu, na tabia zisizotamanika hutumika kuwa maonyo yenye nguvu ili kuzuia Wakristo wasifuate mwendo usiofaa. Wakati sehemu hii inapokuwa na msingi juu ya “Vichwa vya Biblia vya Mazungumzo,” kichwa kilichotolewa kuwa mgawo kingepasa kutumiwa, na mwanafunzi angepaswa kujitahidi kufanya matumizi yenye kufaa ya maandiko. Ndugu au dada anaweza kugawiwa Mgawo Na. 4. Wakati ndugu anapougawiwa, huo ungepaswa sikuzote kuwa hotuba. Wakati dada anapougawiwa, huo ungepasa kutolewa kama inavyoonyeshwa kuhusu Mgawo Na. 3. Kwa kuongezea, wakati wowote ambapo kichwa cha Mgawo Na. 4 kinatanguliwa na alama #, hicho kingepasa kutolewa zaidi sana kwa ndugu.
*PROGRAMU YA ZIADA YA USOMAJI WA BIBLIA: Hii inawekwa katika vifungo vya mraba [] baada ya namba ya wimbo wa kila juma. Kwa kufuata programu hiyo, tukisoma kurasa kumi hivi kwa juma, Biblia nzima inaweza kusomwa kwa muda wa miaka mitatu. Hakuna sehemu ya programu ya shule au kujikumbusha kwa kuandika vinavyotokana na programu ya ziada ya usomaji.
TAARIFA: Ili kupata habari ya ziada na maagizo kuhusu shauri, kuheshimu wakati, kujikumbusha kwa kuandika, na kutayarisha migawo, tafadhali ona ukurasa 3 wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1996.
Programu
Jan. 3 usomaji wa Biblia: Kumbukumbu 4-6
Wimbo Na. 9 [*Yeremia 49-52]
Na. 1: Thamini Baraka za Yehova (w98-SW 1/1 kur. 22-4)
Na. 2: Kumbukumbu 6:4-19
Na. 3: td-SW 14A Kwa Nini Mungu Hakubali Kuabudu Wazazi wa Kale?
Na. 4: Simoni (Simon) (Na. 8)—Kichwa: #Tumikia Mungu Ukiwa na Nia Safi
Jan. 10 usomaji wa Biblia: Kumbukumbu 7-10
Wimbo Na. 49 [*Maombolezo 1-5]
Na. 1: Tukuzeni Mungu wa Kweli (w98-SW 1/1 kur. 30-1)
Na. 2: Kumbukumbu 8:1-18
Na. 3: td-SW 1B Wanadamu Wanaweza Kuheshimiwa, Lakini Mungu Pekee Ndiye Anayepaswa Kuabudiwa
Na. 4: Sisera (Na. 1)—Kichwa: Ushindi Ni wa Yehova
Jan. 17 usomaji wa Biblia: Kumbukumbu 11-14
Wimbo Na. 132 [*Ezekieli 1-9]
Na. 1: Kwa Nini Kupanga Mambo Kimbele kwa Ajili ya Wapendwa Wetu? (w98-SW 1/15 kur. 19-22)
Na. 2: Kumbukumbu 11:1-12
Na. 3: td-SW 7A Har–Magedoni—Vita kwa Ajili ya Kukomesha Uovu
Na. 4: Solomono (Salomon)—Kichwa: #Linda Moyo Wako
Jan. 24 usomaji wa Biblia: Kumbukumbu 15-19
Wimbo Na. 162 [*Ezekieli 10-16]
Na. 1: Nguvu ya Kugeuza na Kuunganisha ya ile Kweli (w98-SW 1/15 kur. 29-31)
Na. 2: Kumbukumbu 19:11-21
Na. 3: td-SW 7B Kwa Nini Har–Magedoni Ni Tendo la Upendo la Mungu?
Na. 4: Sosthenesi (Sosthène)—Kichwa: Hubiria Watu wa Namna Zote
Jan. 31 usomaji wa Biblia: Kumbukumbu 20-23
Wimbo Na. 13 [*Ezekieli 17-21]
Na. 1: Maoni ya Kimaandiko juu ya Kusifu na Kurai (w98-SW 2/1 kur. 29-31)
Na. 2: Kumbukumbu 20:10-20
Na. 3: td-SW 33A Ubatizo Ni Takwa la Kikristo
Na. 4: Stefanasi (Stéphanas)—Kichwa: #Uwe Thabiti Katika Kweli
Feb. 7 usomaji wa Biblia: Kumbukumbu 24-27
Wimbo Na. 222 [*Ezekieli 22-27]
Na. 1: Msingi wa Kutazamia Mema kwa Kweli (w98-SW 2/1 kur. 4-6)
Na. 2: Kumbukumbu 25:5-16
Na. 3: td-SW 33B Ubatizo Hauoshei Mbali Dhambi
Na. 4: Stefano (Étienne)—Kichwa: #Onyesha Kwamba Unajaa Roho na Hekima
Feb. 14 usomaji wa Biblia: Kumbukumbu 28-30
Wimbo Na. 180 [*Ezekieli 28-33]
Na. 1: Sitawisha Roho ya Shukrani (w98-SW 2/15 kur. 4-7)
Na. 2: Kumbukumbu 28:1-14
Na. 3: td-SW 1A Biblia Ni Neno la Mungu Lililopuliziwa
Na. 4: Susana (Suzanne)—Kichwa: Tumia Mali Zako ili Kusaidia Wengine
Feb. 21 usomaji wa Biblia: Kumbukumbu 31-34
Wimbo Na. 46 [*Ezekieli 34-39]
Na. 1: Kumbukumbu la Torati—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si-SW kur. 40-1 maf. 30-4)
Na. 2: Kumbukumbu 32:35-43
Na. 3: td-SW 1B Biblia Ni Mwongozo Wenye Kutumika kwa Siku Yetu
Na. 4: Sintike (Syntyche)—Kichwa: Endeleeni Kuishi Pamoja kwa Amani
Feb. 28 usomaji wa Biblia: Yoshua 1-5
Wimbo Na. 40 [*Ezekieli 40-45]
Na. 1: Yoshua—Utangulizi (si-SW uku. 42 maf. 1-5)
Na. 2: Yoshua 2:8-16
Na. 3: td-SW 1C Biblia Ni Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote
Na. 4: Tamari (Tamar) (Na. 1)—Kichwa: Usiwe Haraka Kuhukumu
Machi 6 usomaji wa Biblia: Yoshua 6-9
Wimbo Na. 164 [*Ezekieli 46–Danieli 2]
Na. 1: Wazazi—Walindeni Salama Watoto Wenu! (w98-SW 2/15 kur. 8-11)
Na. 2: Yoshua 7:1, 10-19
Na. 3: td-SW 2A Kutiwa Damu Mishipani Huvunja Utakatifu wa Damu
Na. 4: Tera (Térah) (Na. 1)—Kichwa: Je! Dini ya Wazazi wa Mtu Ni ya Kweli Sikuzote?
Machi 13 usomaji wa Biblia: Yoshua 10-13
Wimbo Na. 138 [*Danieli 3-7]
Na. 1: Kile Ambacho Biblia Husema Kuhusu Kipawa (w98-SW 2/15 kur. 23-7)
Na. 2: Yoshua 11:6-15
Na. 3: td-SW 2B Je! Inafaa Kuokoa Uhai wa Mtu Bila Kujali Gharama?
Na. 4: Teresi (Téresh)—Kichwa: Matokeo ya Ukosefu wa Uaminifu
Machi 20 usomaji wa Biblia: Yoshua 14-17
Wimbo Na. 10 [*Danieli 8–Hosea 2]
Na. 1: Wanaume Waaminifu ‘Wenye Hisia Kama Zetu’ (w98-SW 3/1 kur. 26-9)
Na. 2: Yoshua 15:1-12
Na. 3: td-SW 32 Nyakati za Mataifa Zilikwisha Wakati Gani?
Na. 4: Tomasi (Thomas)—Kichwa: #Kwa Nini Tungepaswa Kufikiri Kabla ya Kusema
Machi 27 usomaji wa Biblia: Yoshua 18-20
Wimbo Na. 105 [*Hosea 3-14]
Na. 1: Kuzikumbuka Siku za Mwisho za Yesu Duniani (w98-SW 3/15 kur. 3-9)
Na. 2: Yoshua 18:1-10
Na. 3: td-SW 12A Kanisa la Kikristo Ni Nini?
Na. 4: Tiberio (Tibère)—Kichwa: Upotovu wa Kiadili Unaweza Kumfanya Mtu Adharauliwe
Apr. 3 usomaji wa Biblia: Yoshua 21-24
Wimbo Na. 144 [*Yoeli 1–Amosi 7]
Na. 1: Yoshua—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si-SW kur. 45-6 maf. 21-4)
Na. 2: Yoshua 21:43–22:8
Na. 3: td-SW 12B Je! Petro Ndiye Lile “Tungamo-Mwamba”?
Na. 4: Timotheo (Timothée)—Kichwa: #Imani Bila Unafiki Humtukuza Mungu
Apr. 10 usomaji wa Biblia: Waamuzi 1-4
Wimbo Na. 43 [*Amosi 8–Mika 5]
Na. 1: Waamuzi—Utanguluzi (si-SW kur. 46-7 maf. 1-7)
Na. 2: Waamuzi 3:1-11
Na. 3: td-SW 41A Sayansi Iliyothibitishwa Yaunga Mkono Simulizi la Biblia la Uumbaji
Na. 4: Tito (Tite)—Kichwa: #Tumikia Akina Ndugu kwa Moyo Wote
Apr. 17 usomaji wa Biblia: Waamuzi 5-7
Wimbo Na. 193 [*Mika 6–Sefania 1]
Na. 1: Jifunze Kutokana na Maagizo ya Yesu kwa Wale 70 (w98-SW 3/1 kur. 30-1)
Na. 2: Waamuzi 5:24-31
Na. 3: td-SW 41B Je! Kila Siku ya Uumbaji Ilikuwa Kipindi cha Wakati cha Saa 24?
Na. 4: Tobia (Na. 2)—Kichwa: Maadui wa Mungu Hawatafaulu
Apr. 24 kujikumbusha kwa kuandika. Malizeni Kumbukumbu 4–Waamuzi 7
Wimbo Na. 91 [*Sefania 2–Zekaria 7]
Mei 1 usomaji wa Biblia: Waamuzi 8-10
Wimbo Na. 38 [*Zekaria 8–Malaki 4]
Na. 1: Heshimu Adhama ya Binafsi ya Wengine (w98-SW 4/1 kur. 28-31)
Na. 2: Waamuzi 9:7-21
Na. 3: td-SW 24A Je! Yesu Alikufa juu ya Msalaba?
Na. 4: Trifimo (Trophimus)—Kichwa: #Toa Utegemezo kwa Wale Wanaoongoza
Mei 8 usomaji wa Biblia: Waamuzi 11-14
Wimbo Na. 82 [*Mathayo 1-8]
Na. 1: Barnaba, Yule “Mwana wa Faraja” (w98-SW 4/15 kur. 20-3)
Na. 2: Waamuzi 13:2-10, 24
Na. 3: td-SW 24B Je! Wakristo Wanapaswa Kuabudu Msalaba?
Na. 4: Trifaina (Tryphène)—Kichwa: Thamini Wanawake Wanaofanya Kazi Ngumu Katika Bwana
Mei 15 usomaji wa Biblia: Waamuzi 15-18
Wimbo Na. 26 [*Mathayo 9-14]
Na. 1: Usalama wa Ulimwengu Bila Majeshi (w98-SW 4/15 kur. 28-30)
Na. 2: Waamuzi 17:1-13
Na. 3: td-SW 13A Ni Nini Sababu ya Kifo?
Na. 4: Tikiko (Tychique)—Kichwa: #Uwe Mkristo Mwaminifu na Mwenye Kutumainiwa
Mei 22 usomaji wa Biblia: Waamuzi 19-21
Wimbo Na. 42 [*Mathayo 15-21]
Na. 1: Waamuzi—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si-SW uku. 50 maf. 26-8)
Na. 2: Waamuzi 19:11-21
Na. 3: td-SW 13B Je! Wafu Wanaweza Kukuumiza?
Na. 4: Uria (Urie) (Na. 1)—Kichwa: Uwe Mwenye Kujitoa Kikamili Katika Utumishi Wako kwa Mungu
Mei 29 usomaji wa Biblia: Ruthi 1-4
Wimbo Na. 120 [*Mathayo 22-26]
Na. 1: Ruthi—Utangulizi na Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si-SW kur. 51-3 maf. 1-3, 9-10)
Na. 2: Ruthi 3:1-13
Na. 3: td-SW 13C Je! Wanadamu Wanaweza Kuongea na Washiriki Wao wa Familia Waliokufa?
Na. 4: Uriya (Ouriya) (Na. 2)—Kichwa: Ogopa Mungu wa Kweli, Si Mwanadamu
Juni 5 usomaji wa Biblia: 1 Samweli 1-3
Wimbo Na. 191 [*Mathayo 27–Marko 4]
Na. 1: 1 Samweli—Utangulizi (si-SW kur. 53-4 maf. 1-6)
Na. 2: 1 Samweli 1:9-20
Na. 3: td-SW 10A Je! Ibilisi Ni Mtu Halisi?
Na. 4: Uza (Ouzza) (Na. 2)—Kichwa: #Nia Nzuri Hazitetei Ukosefu wa Utii
Juni 12 usomaji wa Biblia: 1 Samweli 4-7
Wimbo Na. 85 [*Marko 5-9]
Na. 1: Yehova Ni Nani? (w98-SW 5/1 kur. 5-7)
Na. 2: 1 Samweli 4:9-18
Na. 3: td-SW 10B Ibilisi Ndiye Mtawala Asiyeonekana wa Ulimwengu
Na. 4: Uziya (Ouzziya) (Na. 3)—Kichwa: #Heshimu kwa Unyenyekevu Utaratibu wa Kitheokrasi
Juni 19 usomaji wa Biblia: 1 Samweli 8-11
Wimbo Na. 160 [*Marko 10-14]
Na. 1: Uaminifu-Maadili Huthawabishwa (w98-SW 5/1 kur. 30-1)
Na. 2: 1 Samweli 8:4-20
Na. 3: td-SW 10C Kile Ambacho Biblia Inasema Kuhusu Malaika Walioshuka
Na. 4: Vashti—Kichwa: Uwe Mwenye Kiasi na Utembee na Mungu
Juni 26 usomaji wa Biblia: 1 Samweli 12-14
Wimbo Na. 172 [*Marko 15–Luka 3]
Na. 1: Je! Mali Zaweza Kukufanya Uwe Mwenye Furaha? (w98-SW 5/15 kur. 4-6)
Na. 2: 1 Samweli 14:1-14
Na. 3: td-SW 5A Dunia Iliumbwa ili Iwe Paradiso
Na. 4: Zakayo (Zachée)—Kichwa: #Epuka Mtego wa Pupa
Julai 3 usomaji wa Biblia: 1 Samweli 15-17
Wimbo Na. 8 [*Luka 4-8]
Na. 1: Eunike na Loisi—Waelimishaji Walio Vielelezo Bora (w98-SW 5/15 kur. 7-9)
Na. 2: 1 Samweli 16:4-13
Na. 3: td-SW 5B Uhai Duniani Hautakoma Kamwe
Na. 4: Zadoki (Zadoc) (Na. 1)—Kichwa: #Uwe Mtumishi Mwaminifu
Julai 10 usomaji wa Biblia: 1 Samweli 18-20
Wimbo Na. 156 [*Luka 9-12]
Na. 1: Fikia Moyo kwa Ushawishi (w98-SW 5/15 kur. 21-3)
Na. 2: 1 Samweli 19:1-13
Na. 3: td-SW 18A Je! Unaweza Kutambua Manabii Wasio wa Kweli?
Na. 4: Zeba (Zébah)—Kichwa: Wapingaji wa Watu wa Mungu Watahukumiwa
Julai 17 usomaji wa Biblia: 1 Samweli 21-24
Wimbo Na. 33 [*Luka 13-19]
Na. 1: Chukua Daraka Lako la Kifamilia (w98-SW 6/1 kur. 20-3)
Na. 2: 1 Samweli 24:2-15
Na. 3: td-SW 15A Uponyeshaji wa Kiroho Ni wa Maana Kadiri Gani?
Na. 4: Zekaria (Na. 12)—Kichwa: Yehova Hatasahau Watumishi Wake Waaminifu
Julai 24 usomaji wa Biblia: 1 Samweli 25-27
Wimbo Na. 60 [*Luka 20-24]
Na. 1: Haki ya Kweli—Wakati Gani na Jinsi Gani? (w98-SW 6/15 kur. 26-9)
Na. 2: 1 Samweli 25:23-33
Na. 3: td-SW 15B Ufalme wa Mungu—Njia ya Kuleta Maponyo ya Kimwili Yenye Kudumu
Na. 4: Zekaria (Na. 20)—Kichwa: #Tutiane Moyo Katika Kazi ya Mungu
Julai 31 usomaji wa Biblia: 1 Samweli 28-31
Wimbo Na. 170 [*Yohana 1-6]
Na. 1: 1 Samweli—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si-SW kur. 57-8 maf. 27-35)
Na. 2: 1 Samweli 31:1-13
Na. 3: td-SW 15C Uponyeshaji wa Imani wa Ki-Siku-Hizi Hautoki kwa Mungu
Na. 4: Zekaria (Na. 31)—Kichwa: Amini Yote Mungu Anayosema
Agosti 7 usomaji wa Biblia: 2 Samweli 1-4
Wimbo Na. 22 [*Yohana 7-11]
Na. 1: 2 Samweli—Utangulizi (si-SW uku. 59 maf. 1-5)
Na. 2: 2 Samweli 2:1-11
Na. 3: td-SW 15D Je! Kusema kwa Lugha Ni Ushuhuda Hakika wa Kuwa na Kibali cha Mungu?
Na. 4: Zedekia (Tsidqiya) (Na. 1)—Kichwa: Fanya Angalisho na Manabii wa Uwongo
Agosti 14 usomaji wa Biblia: 2 Samweli 5-8
Wimbo Na. 174 [*Yohana 12-18]
Na. 1: “Jikakamueni Wenyewe Kisulubu” (w98-SW 6/15 kur. 30-1)
Na. 2: 2 Samweli 7:4-16
Na. 3: td-SW 20A Ni Nani Anayekwenda Mbinguni?
Na. 4: Zedekia (Tsidqiya) (Na. 4)—Kichwa: #Tiini Sikuzote Amri za Yehova
Agosti 21 usomaji wa Biblia: 2 Samweli 9-12
Wimbo Na. 107 [*Yohana 19–Matendo 4]
Na. 1: Iweni Jirani Wema (w98-SW 7/1 kur. 30-1)
Na. 2: 2 Samweli 11:2-15
Na. 3: td-SW 8A Helo Si Mahali pa Mateso
Na. 4: Zerubabeli (Zorobabel)—Kichwa: #Kabiliana na Upinzani kwa Ujasiri
Agosti 28 kujikumbusha kwa kuandika. Malizeni Waamuzi 8–2 Samweli 12
Wimbo Na. 177 [*Matendo 5-10]
Sept. 4 usomaji wa Biblia: 2 Samweli 13-15
Wimbo Na. 183 [*Matendo 11-16]
Na. 1: Wapeni Watoto Wenu Mwanzo Mzuri Katika Maisha (w98-SW 7/15 kur. 4-6)
Na. 2: 2 Samweli 13:20-33
Na. 3: td-SW 8B Moto Ni Alama ya Angamizo
Na. 4: Ziba—Kichwa: Ujanja na Uchongezi Hutia Mashakani Nia ya Kufanya Kazi Nzuri
Sept. 11 usomaji wa Biblia: 2 Samweli 16-18
Wimbo Na. 129 [*Matendo 17-22]
Na. 1: Maoni ya Mkristo Kuhusu Desturi za Mazishi (w98-SW 7/15 kur. 20-4)
Na. 2: 2 Samweli 16:5-14
Na. 3: td-SW 8C Simulizi la Tajiri na Lazaro Halitoi Ushuhuda wa Kuwako kwa Mateso ya Milele
Na. 4: Zimri (Na. 2)—Kichwa: #Yehova Haachilii Ukosefu wa Adili
Sept. 18 usomaji wa Biblia: 2 Samweli 19-21
Wimbo Na. 19 [*Matendo 23–Waroma 1]
Na. 1: Je! Waweza Kuamini Dhamiri Yako? (w98-SW 9/1 kur. 4-7)
Na. 2: 2 Samweli 20:1, 2, 14-22
Na. 3: td-SW 31A Maoni ya Kikristo Kuhusu Sikukuu
Na. 4: Zimri (Na. 3)—Kichwa: Tamaa ya Makubwa Isiyozuiwa Inaweza Kuwa na Matokeo Yenye Kuleta Msiba
Sept. 25 usomaji wa Biblia: 2 Samweli 22-24
Wimbo Na. 98 [*Waroma 2-9]
Na. 1: 2 Samweli—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si-SW uku. 63 maf. 28-31)
Na. 2: 2 Samweli 23:8-17
Na. 3: td-SW 23A Matumizi ya Mifano Hayamtukuzi Mungu
Na. 4: Sipora (Zipporah)—Kichwa: Onyesha Hofu na Heshima Wakati Unaponyosha Mambo
Okt. 2 usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 1-2
Wimbo Na. 36 [*Waroma 10–1 Wakorintho 3]
Na. 1: 1 Wafalme—Utangulizi (si-SW kur. 64-5 maf. 1-5)
Na. 2: 1 Wafalme 2:1-11
Na. 3: td-SW 23B Matokeo ya Ibada ya Mifano
Na. 4: Zofari (Zophar)—Kichwa: Uchambuzi Mkali Ni Ukosefu wa Upendo
Okt. 9 usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 3-6
Wimbo Na. 106 [*1 Wakorintho 4-13]
Na. 1: Tanguliza Mambo Yanayopasa Kutangulizwa (w98-SW 9/1 kur. 19-21)
Na. 2: 1 Wafalme 4:21-34
Na. 3: td-SW 23C Yehova Peke Yake Ndiye Anayepasa Kuabudiwa
Na. 4: td-SW 21A #Njia ya Mchanganyiko wa Imani Mbalimbali Si Njia ya Mungu
Okt. 16 usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 7-8
Wimbo Na. 76 [*1 Wakorintho 14–2 Wakorintho 7]
Na. 1: Kutoa Ushahidi Mbele ya Waheshimiwa (w98-SW 9/1 kur. 30-1)
Na. 2: 1 Wafalme 7:1-14
Na. 3: td-SW 21B Je! Dini Zote Ni Nzuri?
Na. 4: td-SW 43A Wakristo Wanapaswa Kutumia Jina la Binafsi la Mungu
Okt. 23 usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 9-11
Wimbo Na. 97 [*2 Wakorintho 8–Wagalatia 4]
Na. 1: Maoni ya Kikristo Kuhusu Mahari (Mali kwa Ajili ya Ndoa) (w98-SW 9/15 kur. 24-7)
Na. 2: 1 Wafalme 11:1-13
Na. 3: td-SW 43B Kweli Kuhusu Kuwako kwa Mungu
Na. 4: td-SW 43C #Kuzitambua Sifa za Mungu
Okt. 30 usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 12-14
Wimbo Na. 113 [*Wagalatia 5–Wafilipi 2]
Na. 1: Je! Mungu Ni Halisi Kwako? (w98-SW 9/15 kur. 21-3)
Na. 2: 1 Wafalme 13:1-10
Na. 3: td-SW 43D Watu Wote Hawamtukii Mungu Yuleyule
Na. 4: td-SW 19A Je! Mashahidi wa Yehova Ni Dini Mpya?
Nov. 6 usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 15-17
Wimbo Na. 123 [*Wafilipi 3–1 Wathesalonike 5]
Na. 1: Zidi Kufanya Maendeleo ya Kiroho! (w98-SW 10/1 kur. 28-31)
Na. 2: 1 Wafalme 15:9-24
Na. 3: td-SW 44A Yesu Kristo—Mwana wa Mungu na Mfalme Aliyewekwa Rasmi
Na. 4: td-SW 44B Kwa Nini Imani Katika Yesu Ni ya Maana Sana kwa Ajili ya Wokovu
Nov. 13 usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 18-20
Wimbo Na. 159 [*2 Wathesalonike 1–2 Timotheo 3]
Na. 1: Tatueni Matatizo kwa Amani (w98-SW 11/1 kur. 4-7)
Na. 2: 1 Wafalme 20:1, 13-22
Na. 3: td-SW 44C Je! Imani Pekee Katika Yesu Inatosha ili Kuokolewa?
Na. 4: td-SW 34A #Baraka Ambazo Ufalme wa Mungu Utaleta
Nov. 20 usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 21-22
Wimbo Na. 179 [*2 Timotheo 4–Waebrania 7]
Na. 1: 1 Wafalme—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si-SW kur. 68-9 maf. 23-6)
Na. 2: 1 Wafalme 22:29-40
Na. 3: td-SW 34B Utawala wa Ufalme Waanza Wakati Maadui wa Kristo Wangali Wanatenda
Na. 4: td-SW 34C Ufalme wa Mungu Hauji Kupitia Jitihada za Mwanadamu
Nov. 27 usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 1-3
Wimbo Na. 148 [*Waebrania 8–Yakobo 2]
Na. 1: 2 Wafalme—Utangulizi (si-SW uku. 69 maf. 1-4)
Na. 2: 2 Wafalme 2:15-25
Na. 3: td-SW 30A Kile Ambacho “Mwisho wa Ulimwengu” Unamaanisha
Na. 4: td-SW 30B #Zidi Kuwa Macho ili Kuona Alama ya Siku za Mwisho
Des. 4 usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 4-6
Wimbo Na. 109 [*Yakobo 3–2 Petro 3]
Na. 1: Fanya Angalisho na Usimoni (w98-SW 11/15 uku. 28)
Na. 2: 2 Wafalme 5:20-27
Na. 3: td-SW 36A Uhai Udumuo Milele Si Ndoto
Na. 4: td-SW 36B Ni Nani Anayekwenda Mbinguni?
Des. 11 usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 7-9
Wimbo Na. 117 [*1 Yohana 1–Ufunuo 1]
Na. 1: Kanuni za Biblia za Kufuata Wakati wa Kukopesha au Kukopa Fedha (w98-SW 11/15 kur. 24-7)
Na. 2: 2 Wafalme 7:1, 2, 6, 7, 16-20
Na. 3: td-SW 36C Hakuna Mpaka kwa Hesabu ya Wale Watakaopokea Uhai Udumuo Milele Duniani
Na. 4: td-SW 26A #Lazima Muungano wa Ndoa Uheshimike
Des. 18 usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 10-12
Wimbo Na. 181 [*Ufunuo 2-12]
Na. 1: Masimulizi ya Kweli ya Kuzaliwa kwa Yesu (w98-SW 12/15 kur. 5-9)
Na. 2: 2 Wafalme 11:1-3, 9-16
Na. 3: td-SW 26B Wakristo Wanapaswa Kuheshimu Kanuni ya Ukichwa
Na. 4: td-SW 26C Daraka la Wazazi kwa Watoto
Des. 25 kujikumbusha kwa kuandika. Malizeni 2 Samweli 13–2 Wafalme 12
Wimbo Na. 217 [*Ufunuo 13-22]