Programu ya mikutano ya utumishi
TAARIFA: Kuanzia toleo hili la Huduma Yetu ya Ufalme, Programu ya Mikutano ya Utumishi itatia ndani muhtasari kwa ajili ya Mkutano wa Utumishi wa kwanza wa mwezi wenye kufuata. Rekebisho hilo ni lenye kufanywa ili litumiwe ikiwa usafirishaji wa Huduma Yetu ya Ufalme unachelewa kwa sababu ya mpango mpya wa usafirishaji.
Juma toka desemba 6
Wimbo 207
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Toa maelezo kuhusu ripoti ya utumishi wa shambani ya Agosti katika nchi na katika kutaniko lenu.
Dak. 15: “Igeni Yehova kwa Kutokuwa na Upendeleo.” Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, na uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu. Fasiria maana ya kutokuwa na upendeleo, jinsi Yehova anavyoonyesha sifa hiyo, na jinsi tunavyoweza kuionyesha katika huduma yetu.—Ona Étude perspicace, Buku 1, uku. 1175, fu. 8 hadi uku. 1176, maf. 1-3.
Dak. 20: “Je! Hatukusikia Hilo Hapo Mbele?” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Alika wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi kurudilia mambo kulivyowasaidia kuelewa na kuthamini kweli kikamili zaidi.—Ona Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1995, kur. 21-2, na Agosti 15, 1993, kur. 13-14, maf. 10-12.
Wimbo 218 na sala ya kumalizia
Juma toka desemba 13
Wimbo 168
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti. Toa madokezo kuhusu jinsi ya kuitikia kwa busara salamu za sikukuu. Ikiwa kutaniko linazo nakala za vitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi au Mwalimu Mkuu katika stoki, onyesha jinsi hivyo vinaweza kutumiwa ifaavyo katika huduma wakati wa sikukuu za Krismasi.
Dak. 15: “Shule ya Huduma ya Kitheokrasi Mnamo 2000.” Hotuba inayofanywa na mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Rudilia mabadiliko yafuatayo katika programu ya mwaka huu mpya. Mgawo Na. 3 utakuwa na msingi juu ya “Vichwa vya Biblia vya Mazungumzo” kama vinavyopatikana katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Mgawo Na. 4 utaendelea kuzungumzia watu wa kibiblia kutoka katika kitabu Étude perspicace des Écritures, na mnamo miezi mitatu ya mwisho wa mwaka, mgawo huo utakuwa na msingi juu ya “Vichwa vya Biblia vya Mazungumzo.” Mahali ambapo alama ya namba (#) inapatikana baada ya mgawo huo, ni vizuri zaidi ndugu autoe. Tia moyo wote waendelee na usomaji wao wa Biblia wa kila juma na kuwa wenye bidii katika kutimiza migawo ya shule.
Dak. 20: “Utasema Nini kwa Mtu Anayeamini Kwamba Hakuna Mungu?” Maulizo na majibu. Rudilia sababu mbalimbali zilizofanya wengi wapoteze imani katika Mungu. Pendekeza njia fulani ambazo kwa hizo tunaweza kuwakaribia, tukiwasaidia waone kwa nini ni jambo lenye kupatana na akili nzuri kukubali kuwako kwa Mungu. Fanyeni onyesho moja au mawili mafupi. Ili kupata habari zaidi, ona kitabu Kutoa Sababu, kurasa 218-224, na Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, sura 14.
Wimbo 220 na sala ya kumalizia
Juma toka desemba 20
Wimbo 219
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Omba wahubiri waeleze mambo mafupi yenye kufaa yaliyoonwa ambayo walifurahia karibuni katika utumishi wa shambani.
Dak. 15: Kujibu Vizuia-Mazungumzo Vinavyoweza Kutokea. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji na maonyesho. Soma “Maelezo” kwenye kurasa 15-16 za kitabu Kutoa Sababu. Chagua vizuia-mazungumzo viwili au vitatu kutoka kurasa 16-20, au utumie vingine vinavyojitokeza kwa kawaida katika eneo lenu. Rudilia majibu fulani-fulani yanayopendekezwa, na uchanganue kwa nini hayo yanaweza kuwa yenye matokeo kwenu. Fanyeni kwa kifupi maonyesho ya majibu fulani-fulani kati ya hayo. Alika wasikilizaji waeleze majibu waliyotumia kwa matokeo.
Dak. 20: Je! Ninaweza Kukubali Kazi Inayohusisha Tengenezo la Kidini? Hotuba inayotolewa na mzee, ikiwa na msingi juu ya Mnara wa Mlinzi wa Aprili 15, 1999, kurasa 28-30. Watu fulani wamekubali kazi kama hizo na baadaye wakatambua kwamba yale waliyokuwa wakifanya hayakupatana na kanuni za Biblia. Rudilia maulizo tunayohitaji kufikiria wakati wa kufanya uamuzi kuhusu kufanya kazi ya kimwili iliyo na uhusiano fulani na dini. Tia moyo wote wafuatie mwendo utakaohakikisha msimamo mzuri mbele ya Yehova.—2 Kor. 6:3, 4, 14-18.
Wimbo 109 na sala ya kumalizia.
Juma toka desemba 27
Wimbo 166
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ikiwa kutaniko lenu litabadili saa za mikutano za mwaka ujao, toa kitia-moyo chenye wema usihi wote waendelee kuhudhuria mikutano kikawaida pa saa hizo mpya. Julisheni mabadiliko yoyote kwa wanafunzi wa Biblia na wengine wenye kupendezwa, na pia anzeni kutumia vikaratasi vya mwaliko ambavyo vinaonyesha programu mpya. Kumbusha wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Desemba.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 20: Kutolea Watu Vitabu vya Zamani na Broshua Mnamo Januari. Hotuba na maonyesho. Onyesha vitabu viwili au vitatu vya zamani vyenye kurasa 192, vilivyotangazwa kabla ya 1986, vilivyo katika stoki ya kutaniko, na utie moyo wahubiri wapeleke baadhi yavyo katika huduma ya shambani. (Ikiwa hakuna hata kimoja kinachopatikana, zungumzia uwezekano mwingine wa toleo la Januari.) Fasiria kwa nini vichapo hivyo vya zamani vingali vyenye matokeo katika kusitawisha kupendezwa na Biblia. Katika kila kitabu, onyesha vichwa vya mazungumzo na picha zinazoweza kutumiwa ifaavyo ili kuanzisha mazungumzo. Fanyeni onyesho moja au mawili ya ule utoaji mbalimbali. Onyesha jinsi ya kutumia broshua Roho za Wafu na Mashahidi wa Yehova Katika Karne ya 20 ikiwa hizo zinapatikana. Mahali ambapo kupendezwa kunapatikana, broshua Anataka inaweza kutumiwa ili kuanzisha funzo.
Wimbo 224 na sala ya kumalizia.
Juma toka januari 3
TAARIFA: Makutaniko hayapaswi kujongeza Mkutano wao wa Utumishi wa juma la Januari 3 kwenye siku ya mbele zaidi ya tarehe hiyo isipokuwa kuna ziara ya mwangalizi wa mzunguko.
Wimbo 10
Dak. 8: Matangazo ya kwenu.
Dak. 17: Jueni Jinsi ya Kutoa Jibu. (Kol. 4:6) Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Kitabu Kutoa Sababu ni msaada mzuri ajabu katika kutayarisha kushiriki kweli ya Biblia pamoja na wengine. Wakati mwenye-nyumba anapotokeza kipingamizi kwa moja ya imani zetu, labda tunaweza kutumia sehemu “Mtu Akisema—” mwishoni mwa habari yenye kuzungumzia imani hiyo. Zungumzieni maelezo kuhusu Biblia, ambayo yanaonekana kwenye kurasa 46-9, na pia fikirieni kwa uangalifu kwa nini majibu yanayopendekezwa yanaweza kuonekana kuwa yenye matokeo.
Dak. 20: “ ‘Watendaji wa Neno la Mungu’—Mkusanyiko wa Wilaya 2000 wa Mashahidi wa Yehova.” Mwandishi anazungumzia makala katika nyongeza kwa maulizo na majibu. Kwanza, soma barua ya Desemba 15, 1999, kwa ajili ya migawo ya mkusanyiko. Tumia maandiko yanayotajwa ili kuonyesha kwa nini sisi sote tunahitaji kufuata kwa ukaribu mwongozo wa Sosaiti. Kazia umaana kwa kila mmoja kupanga mbele ya wakati tarehe zilizo wazi za mapumziko ili kuhudhuria kila siku ya mkusanyiko, kutia ndani Siku ya Tano. Pongeza akina ndugu kwa kushirikiana na mipango ya Sosaiti.
Wimbo 56 na sala ya kumalizia.