Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Mei: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Iweni na broshua Anataka ikiwa tayari kwa ajili ya wale wanaoonyesha kupendezwa, na mjitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Juni: Mungu Anataka Nini Kwetu? Kazeni fikira juu ya kuanzisha mafunzo ya Biblia. Julai na Agosti: Yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 inaweza kutumiwa: Jambo Gani Hutufikia Tunapokufa?, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Kuishi Milele Duniani Katika Furaha!, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje? na Serikali Itakayoleta Paradiso. Broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Nos problèmes — Qui nous aidera à les résoudre? na Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli? zinaweza kutolewa inapofaa.
◼ Tunaomba waandishi waandike sikuzote “S-14” kwenye bahasha ambamo wao hutuma ombi la vichapo S-14 la kutaniko. Hakuna barua nyingine inayopaswa kuwa katika bahasha hiyo.
◼ Tunaona kuwa lazima kukumbusha wahubiri wote kwamba anwani ya Sosaiti haipaswi kutumiwa kwenye barua yoyote ya kibinafsi. Hilo latia ndani barua zote au vichapo vinavyotumwa kama barua ili kutoa ushahidi kwa watu wenye kupendezwa, kwa wale wasiokuwako nyumbani, au kwa wale wanaoishi katika nafasi zisizoweza kufikiwa kwa urahisi. Wakati unapotoa ushahidi kupitia barua, tumia anwani yako mwenyewe au anwani ya Jumba lenu la Ufalme. Tafadhali usitumie anwani ya Sosaiti.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu mwingine aliyechaguliwa naye anapaswa kufanya uchunguzi wa akaunti ya kutaniko mnamo Juni 1 au mapema zaidi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Wakati hilo litakapokuwa limefanywa, toeni tangazo kwa kutaniko baada ya kusomwa kwa ripoti ya akaunti yenye kufuata.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Kiswahili: Yesu Kristo—Yeye Ni Nani? (T-24)
◼ Vichapo vinavyopatikana tena katika stoki:
Kiswahili: Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?