Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/01 uku. 1
  • Jinsi ya kusadikisha wengine

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Jinsi ya kusadikisha wengine
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uwe Mwenye Kusadikisha Unapofundisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Namna Gani Tunapashwa ‘Kumujibia Kila Mutu’?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 2/01 uku. 1

Jinsi ya kusadikisha wengine

1 Mtume Paulo alijulikana kuwa mhudumu mwenye usadikisho. (Mdo. 19:26) Hata Mfalme Agripa alimwambia: “Kwa muda mfupi [ungenisadikisha] niwe Mkristo.” (Mdo. 26:28) Ni nini kilichofanya huduma ya Paulo iwe yenye kusadikisha sana? Alitafakari kutokana na Maandiko kwa njia yenye kupatana na akili, akipatanisha maneno yake na wasikilizaji wake.—Mdo. 28:23.

2 Sisi pia tunahitaji kumwiga Paulo kwa kuwa wenye usadikisho katika huduma yetu. Namna gani? Kwa kutumia ufahamu wenye kina wakati tunaposikiliza na kusema na wengine. (Mez. 16:23) Hatua tatu za maana zitatusaidia kutimiza hilo.

3 Sikiliza kwa uangalifu: Kadiri yule mtu mwingine anavyosema, sikiliza ili utambue jambo ambalo juu ya hilo mnapatana kusudi ufanye hilo kuwa msingi wa mazungumzo. Ikiwa anatokeza kipingamizi, jaribu kutambua sababu ya kutokezwa kwa kipingamizi hicho. Lingekuwa jambo lenye kusaidia kujua kwa usahihi yale ambayo anaamini, kwa nini anayaamini, na yale yaliyomsadikisha kuhusu mambo hayo. (Mez. 18:13) Kwa busara, mfanye aseme.

4 Uliza maulizo: Ikiwa mtu anaonyesha kwamba anaamini Utatu, unaweza kuuliza: “Je, umekuwa sikuzote ukiamini Utatu?” Endelea hivi: “Je, ulipata wakati wowote kujifunza kikamili yale ambayo Biblia inasema kuhusu jambo hilo?” Unaweza pia kuuliza: “Ikiwa Mungu angekuwa sehemu ya Utatu, je, hatungetazamia Biblia iseme hivyo waziwazi?” Majibu unayopata yatakusaidia utafakari na mtu huyo kuhusu yale ambayo Maandiko yanasema.

5 Tumia namna ya kutafakari yenye akili: Shahidi mmoja aliuliza mwanamke aliyeamini kwamba Yesu alikuwa Mungu: ‘Ikiwa ungekuwa mwenye kujaribu kueleza kwamba watu wawili ni sawa, ni uhusiano gani wa kifamilia unaoweza kutumia?’ Mwanamke huyo akajibu: “Ninaweza kutumia ndugu wawili.” Shahidi akaongeza: “Labda hata mapacha wenye kuwa sawasawa. Lakini katika kutufundisha tuone Mungu kuwa Baba na yeye mwenyewe kuwa Mwana, Yesu alikuwa akitoa ujumbe gani?” Mwanamke huyo akafikia uamuzi kwamba mmoja ni mwenye umri mkubwa zaidi na ana mamlaka zaidi. (Mt. 20:23; Yn. 14:28; 20:17) Akili na moyo wake vilikuwa vimeguswa na ufundi wa kusadikisha.

6 Bila shaka, si wote wanaopokea kweli, hata utoaji wetu uwe sahihi na wa akili kama nini. Lakini, kama Paulo, acheni tuwe wenye bidii katika kutafuta wale wenye mioyo minyofu katika eneo letu, tukiwasadikisha wakubali ujumbe wa Ufalme.—Mdo. 19:8.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine