Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Mei: Magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Toleeni watu kitabu Ujuzi na broshua Anataka; mkiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Juni: Mungu Anataka Nini Kwetu? au Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Kazeni fikira juu ya kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Julai na Agosti: Yoyote ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 inaweza kutumiwa: Jambo Gani Hutufikia Tunapokufa?; Je! Kweli Mungu Anatujali?; Je! Uamini Utatu?; Jina la Mungu Litakaloendelea Milele; Kuishi Milele Duniani Katika Furaha!; Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa; Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?; Serikali Itakayoleta Paradiso; na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote; Nos problèmes — Qui nous aidera à les résoudre ?; na Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli? zinaweza kutolewa inapofaa.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu mwingine anayechaguliwa naye atafanya uchunguzi wa akaunti za kutaniko mnamo Juni 1 au mapema zaidi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Wakati jambo hilo litakapokuwa limefanywa, fanyeni tangazo kwa kutaniko baada ya kusoma ripoti ya akaunti yenye kufuata.
◼ Kuanzia juma la Julai 30, 2001, tutajifunza Unabii wa Isaya—Nuru kwa Wanadamu Wote I katika Funzo la Kitabu.
◼ Mnara wa Mlinzi wa Juni 15, 2001, utakuwa na makala yenye kichwa “Je, Fedha Zinaweza Kukutolea Uhai Ulio Kwelikweli?” Kwa kuwa hiyo ni makala yenye kupendeza, maombi ya makutaniko yataongezwa kwa asilimia 20 kuhusu chapa hiyo.
◼ Ripoti zinaonyesha kwamba wahubiri fulani hufanya maombi ya kaseti-vidio kwa ajili ya kujiletea sifa au kwa sababu tu ya kufurahia kuwa nazo ijapokuwa hawana mashini inayotumiwa ili kuzitazama. Tunawakumbusha kwamba utoaji wa bidhaa hizo hugharimu Sosaiti fedha nyingi. Kwa hiyo, inafaa kuzifanyia ombi tu ikiwa mna chombo cha kutumia ili kuzitazama. Kama sivyo, ingekuwa kuonyesha hekima na uamuzi mzuri kutozifanyia ombi. Waandishi wa makutaniko wanaombwa wachunguze kwa uangalifu karatasi za maombi kabla ya kuzitia sahihi na kuzisafirisha, ili wahakikishe kwamba hakuna kitu kinachofanyiwa ombi bila kuhitajiwa au kwa ajili ya kujiletea sifa.—1 Kor. 14:20; Efe. 1:8; 2 Tim. 4:5a.
◼ Makutaniko ambayo katika eneo layo hukutana na wageni wanaozungumza lugha ya kigeni yanaweza kufanya ombi la vichapo katika lugha hiyo ili kuwatolea vichapo katika lugha wanayoijua. Hilo linaweza kuhusu magazeti, broshua Mungu Anataka Nini Kwetu au kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.