Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/02 uku. 1
  • Watu Wenye Furaha Zaidi Duniani

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Watu Wenye Furaha Zaidi Duniani
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wenye Furaha Ni Wale Wenye Kumutumikia “Mungu Mwenye Furaha”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Unaweza Kuwa na Furaha ya Kweli
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 2/02 uku. 1

Watu Wenye Furaha Zaidi Duniani

1 “Heri watu wenye BWANA [Yehova, NW] kuwa Mungu wao”! (Zab. 144:​15) Maneno hayo yanafafanua Mashahidi wa Yehova kuwa watu wenye furaha zaidi duniani. Hakuna furaha iliyo kubwa zaidi kupita ile inayotokana na kutumikia Mungu pekee wa kweli na aliye hai, Yehova. Kwa kuwa yeye ndiye “Mungu mwenye furaha,” wale wanaomwabudu huonyesha furaha yake. (1 Tim. 1:​11) Ni nini sehemu fulani za ibada yetu zinazotufanya tuwe wenye furaha sana?

2 Sababu za Kuwa Wenye Furaha: Yesu alituhakikishia kwamba furaha inatokana na “kuona uhitaji [wetu] wa kiroho.” (Mt. 5:3) Kuendelea kujifunza Biblia na kuhudhuria mikutano yetu yote ya Kikristo kunatosheleza uhitaji huo. Kujifunza kweli ya Neno la Mungu kumetuweka huru kutoka katika uwongo na makosa ya kidini. (Yn. 8:​32) Maandiko yametufundisha pia njia bora zaidi ya kuishi. (Isa. 48:​17) Kwa sababu ya hilo, tunafurahia ushirika mzuri wa Kikristo katika muungano wetu wenye furaha wa ndugu.​—1 Thes. 2:​19, 20; 1 Pet. 2:​17.

3 Tunapata kutosheka kutokana na kutii viwango vya kiadili vya juu vya Mungu, kwa kuwa tunajua kwamba jambo hilo linatulinda na linamfurahisha Yehova. (Mez. 27:​11) Mweneza-habari wa gazeti moja alisema: “Ijapokuwa viwango vyao vyenye kushikilia mambo sana, Mashahidi wa Yehova hawaonekani kuwa wasio na furaha. [. . . ] Vijana na wale wenye umri mkubwa zaidi [kati yao] wanaonekana kwa namna isiyo ya kawaida kuwa wenye furaha na wenye usawaziko.” Tunawezaje kusaidia wengine washiriki maisha yetu yenye furaha?

4 Saidieni Wengine Wapate Furaha: Ulimwengu unajaa ukosefu wa furaha, na watu kwa kawaida wana mtazamo wenye giza kuhusu wakati ujao. Lakini, sisi tuna mtazamo wenye kung’aa, tukijua kwamba siku moja huzuni yote itapita. (Ufu. 21:​3, 4) Kwa hiyo, tunashiriki kwa bidii katika huduma, tukitafuta watu wenye mioyo minyofu ili tushiriki nao tumaini letu na imani zetu kuhusu Yehova.​—Eze. 9:4.

5 Dada mmoja painia alisema: “Hakuna jambo linalofanya mtu atosheke zaidi kuliko kusaidia wengine wapate kumjua Yehova na kweli yake.” Acheni tufanye yote tuwezayo ili kusaidia wengine wengi wakubali mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Kumtumikia Yehova na kujitoa ili kusaidia wengine wamtumikie yeye kunatokeza furaha iliyo kubwa kupita zote.​—Mdo. 20:35.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine