Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Februari: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!, au kitabu chochote cha zamani chenye kurasa 192 ambacho kutaniko linacho katika stoki. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Aprili na Mei: Magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Toleeni watu broshua Anataka, mkiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani.
◼ Kwa sababu ya mabadiliko ya maana yaliyofanywa juu ya maandikisho kwa ajili ya kupokea magazeti na kaseti, tunataka kuwajulisha nukta zifuatazo: Kuanzia matoleo ya Machi 1 na Machi 8, 2002, wahubiri watakuwa wakipelekea watu magazeti kwa ukawaida badala ya watu hao kujiandikisha. Tawi litahamisha mara moja maandikisho hayo katika lugha za kigeni kuwa ombi la kawaida la kutaniko. Hilo linamaanisha kwamba matoleo ya mwisho yatakayopokewa kuwa andikisho yatakuwa yale ya Februari 15 na Februari 22, 2002 (Februari 1 na Februari 8 ikiwa ni toleo la mara moja kwa mwezi). Wakati makutaniko yanapoomba magazeti katika lugha za kigeni, yanapaswa kujaza fomu M(d)-202-F Demande pour congrégation : périodiques / Ministère du Royaume. Andikisho lolote kwa ajili ya kupokea kaseti ya kusikiliza litaombwa kama inavyofanywa kuhusu maandikisho kwa ajili ya kupokea magazeti, ni kusema kwa kujaza fomu M(d)-202-F. Tafadhali, chunguzeni “Instructions pour la demande de publications” S(d)-15a-F Cn.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu mwingine atakayechaguliwa naye anapaswa kufanya uchunguzi wa akaunti za kutaniko mnamo Machi 1 au mapema zaidi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Jambo hilo litakapokuwa limefanywa, toeni tangazo kwa kutaniko baada ya kusoma ripoti ya akaunti yenye kufuata.
◼ Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wanapaswa kukagua utendaji wa mapainia wa kawaida wote. Ikiwa yeyote ana matatizo ya kufikia kiwango cha saa, wazee wanapaswa kuchukua mipango ili msaada utolewe. Ili kupata mapendekezo, rudilieni barua S-201 za kila mwaka. Ona pia fungu la 1-9 katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 1987, ukurasa wa 3.
◼ Hotuba ya pekee ya watu wote kwa ajili ya majira ya Ukumbusho mnamo 2002 itatolewa Siku ya Yenga, Aprili 14. Kichwa cha hotuba hiyo kitakuwa “Wekeni Karibu Katika Akili ile ‘Siku Yenye Kuogopesha’!” Muhtasari utatolewa. Makutaniko yatakayokuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko au kusanyiko mwisho-juma huo yatakuwa na hotuba ya pekee juma lenye kufuata. Hakuna kutaniko linalopaswa kuwa na hotuba ya pekee kabla ya Aprili 14, 2002.
◼ Amkeni! ya Machi 8, 2002, itazungumzia habari “Walimu—Tungefanyaje Bila Wao?” Kwa kuwa makala hiyo ni yenye kupendeza sana, ombi la kila kutaniko litaongezwa kwa asilimia 20.
◼ Mnara wa Mlinzi wa Machi 15, 2002, utazungumzia uongozi wa Kristo juu ya kutaniko. Kwa kuwa habari hiyo ni yenye kupendeza sana, ombi la kila kutaniko litaongezwa kwa asilimia 10.
◼ Tunataka kuvuta uangalifu wa wazee juu ya jinsi ya kutumikisha mihtasari ya hotuba za watu wote ambayo mmekwisha kutolewa: (1) Mwangalizi-msimamizi anapaswa kuweka vizuri, mahali palipo hakika, faili ya kawaida ya mihtasari yote. (2) Atatoa kwa msemaji, si nakala ile iliyotumwa na ofisi, lakini fotokopi ya muhtasari. (3) Hotuba ileile kwa kweli inaweza kutolewa na wasemaji tofauti-tofauti. (4) Tafadhali ingizeni mara moja katika faili yenu mihtasari mipya inayotumwa na tawi. (5) Jueni kwamba Sosaiti haitoi mihtasari ileile mara ya pili, isipokuwa marekebisho yamefanywa juu ya mambo yaliyo ndani ya mihtasari hiyo. Wakati huo, inafaa kuharibu muhtasari wa zamani na kutia ule mpya pa nafasi yake. Namna hiyo ya kufanya mambo itawezesha kutaniko kusikiliza hotuba zinazopangwa na Baraza Linaloongoza.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Kifaransa, Kiingereza: Kalenda ya 2002.
Otetela: Sikiliza Unabii wa Danieli!