Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/02 uku. 7
  • Matangazo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 3/02 uku. 7

Matangazo

◼ Toleo la vichapo la Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Wahubiri wanaweza kujulisha wenye nyumba kwamba wanaweza kutoa mchango ili kutegemeza kazi ya ulimwenguni pote ikiwa wanataka kufanya hivyo. Mahali ambapo kupendezwa kunaonyeshwa, toleeni watu broshua Anataka, mkifanya jitihada ya pekee ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Juni: Mungu Anataka Nini Kwetu? au Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Ikiwa wenye nyumba wana vichapo hivyo, watoleeni broshua yenye kufaa ambayo kutaniko linayo katika stoki.

◼ Wahubiri wanaotaka kutumikia wakiwa mapainia wasaidizi mnamo Aprili wanapaswa kuchukua mipango yao sasa na kutoa ombi mapema. Hilo litasaidia wazee wafanye mipango ya lazima kwa ajili ya utumishi wa shambani na kuwa na magazeti ya kutosha na vichapo vingine vikiwa tayari. Majina ya wale wote wanaokubaliwa kuwa mapainia wasaidizi yanapaswa kutangazwa kwa kutaniko kila mwezi.

◼ Ukumbusho utafanywa Siku ya Nne, Machi 28, 2002. Ikiwa kwa kawaida kutaniko lenu lina mikutano Siku ya Nne, hiyo inapaswa kuwekwa kwenye siku nyingine ya juma ikiwa Jumba la Ufalme halitumiwi na kutaniko lingine. Ikiwa hilo haliwezekani na kwamba linakuwa na uvutano mbaya juu ya Mkutano wenu wa Utumishi, sehemu zinazohusu kipekee kutaniko lenu zinaweza kuingizwa katika Mkutano wa Utumishi mwingine.

◼ Ofisi ya tawi haitoi vichapo vinavyoombwa kwenye maombi ya vichapo ya wahubiri binafsi. Mwangalizi-msimamizi anapaswa kuchukua mipango ili tangazo lifanywe kabla ya ombi la vichapo la kutaniko kutumwa kwenye tawi kusudi wote wanaotaka kupata vichapo vya kibinafsi waweze kumjulisha ndugu anayeshughulika na vichapo. Tafadhali kumbukeni ni vichapo gani vinavyofanyiwa ombi la pekee.

◼ Wakati mwangalizi-msimamizi anapopokea Taarifa ya Ofisi ya Tawi kila mwezi, anapaswa kuhakikisha kwamba kutaniko linasomewa maneno yote ya shukrani yenye kuonyesha kwamba michango imepokewa kwa ajili ya Hazina ya Sosaiti ya Majumba ya Ufalme na kazi ya ulimwenguni pote; maneno hayo yanapaswa kusomwa pamoja na ripoti ya akaunti.

◼ Iweni waangalifu kuhusu mipango ya udanganyi ambayo imekuwa ikizunguka kwenye Internet na katika barua ili kuomba fedha kwa ajili ya ndugu zetu kana kwamba kwa ajili ya kusaidia wale waliopatwa na misiba. Wakati wowote hali zinapoomba kuunda halmashauri ya misaada ili kutoa msaada wa kimwili kwa Mashahidi wa Yehova, ndugu wenye madaraka watajulishwa.

◼ Watafiti na watu wengine wamekutana na ndugu fulani-fulani, wakitafuta habari kuhusu Mashahidi wa Yehova na tengenezo letu. Wameomba fomu za ukaguzi zijazwe, zikitoa majibu kwa maulizo yenye kuhusiana na imani zetu na mafundisho yetu. Ikiwa watu kama hao wanakaribia mhubiri wa kutaniko, mhubiri huyo anapaswa kuwapa jina la mwangalizi-msimamizi. Wazee wanaweza kushughulika na maulizo kama hayo na kutoa jibu lenye kufaa na lenye kutegemea barua iliyotumwa kwa mabaraza yote ya wazee, barua ya Aprili 25, 2001.

◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:

Kifaransa, Kiingereza: Kuyachunguza Maandiko Kila Siku 2002.

◼ Vidio-Kaseti Mpya Zinazopatikana:

Lugha ya Ishara ya Kiamerika: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi​—vidio ya 2.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine