Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/02 uku. 2
  • Programu Ya Mikutano Ya Utumishi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu Ya Mikutano Ya Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 10/02 uku. 2

Programu Ya Mikutano Ya Utumishi

Juma Toka Oktoba 14

Wimbo 103

Dak. 10:Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Tia moyo kila mmoja atazame vidio Les Jeunes s’interrogent... Comment se faire de vrais amis ? ili kujitayarisha kwa ajili ya mazungumzo kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma la Oktoba 28. Kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8, fanyeni maonyesho mawili kuhusu jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 15 na Amkeni! ya Oktoba 22. Katika kila tamasha, onyesheni njia tofauti ya kushughulikia kizuia-mazungumzo “Tayari naijua sana kazi yenu.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 20.

Dak. 15:Mahitaji ya kutaniko.

Dak. 20:“Jinsi Waangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko Wanavyoonyesha Kupendezwa Kibinafsi.” Mazungumzo ya maulizo na majibu itakayotolewa na mwangalizi mmoja wa Funzo la Kitabu la Kutaniko. Katika maelezo ya utangulizi, eleza kwa kifupi jinsi mpango wa funzo la kitabu ulivyoanza. (jv-SW 237, fu. 4) Chukueni mipango kimbele ili wahubiri wawili au watatu watoe maelezo kuhusu jinsi ambavyo wamefaidika na kupendezwa kibinafsi kulikoonyeshwa kwao kupitia Funzo la Kitabu la Kutaniko.

Wimbo 65 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Oktoba 21

Wimbo 206

Dak. 10:Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti.

Dak. 35:“Tufaidike Kikamili na Kusanyiko la Wilaya ‘Watangazaji Wenye Bidii wa Ufalme.’” Itolewe na kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi. Baada ya utangulizi wa dakika moja, ongoza mazungumzo pamoja na wasikilizaji kuhusu programu ya kusanyiko la wilaya, ukitumia maulizo yaliyotolewa katika makala. Panga wakati wako kwa uangalifu. Maelezo mafupi yanaweza kutiwa ndani ili kukumbusha wasikilizaji mambo makuu ya kusanyiko. Inapofaa, uliza wasikilizaji jinsi ambavyo wamekuwa wakitumia yale waliyojifunza na faida ambazo wamepokea kwa kufanya hivyo.

Wimbo 194 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Oktoba 28

Wimbo 110

Dak. 8:Matangazo ya kwenu. Tia moyo wote warudilie maandishi yao kuhusu programu ya kusanyiko la pekee la mwisho ili kujitayarisha kwa ajili ya mazungumzo kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma lijalo. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Oktoba. Kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8, omba dada mmoja aonyeshe jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi wa Novemba 1 na ndugu mmoja aonyeshe jinsi ya kutoa Amkeni! ya Novemba 8. Baada ya kila onyesho, kazia kwa kifupi sehemu yenye matokeo ya utoaji.

Dak. 12:Mambo yaliyoonwa katika eneo lenu. Alika washiriki wa kutaniko wasimulie mambo yaliyoonwa waliyofurahia waliposafiri kwenda na kutoka kwenye kusanyiko la wilaya, walipokuwa kwenye kusanyiko, au walipokuwa wakitoa ushahidi wa vivi hivi kazini, shuleni, walipokuwa wakifanya ununuzi katika maduka, na kadhalika.

Dak. 25:“Itikio Lenye Shauku!” Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja. Katika fungu la 1, tolea kutaniko nafasi ili liongeze maneno mafupi kuhusu vidio Les jeunes s’interrogent... Comment se faire de vrais amis ? Kisha, anza mara moja mazungumzo pamoja na wasikilizaji kuhusu kila ulizo linalotolewa katika fungu la 2-7.

Wimbo 41 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Novemba 4

Wimbo 66

Dak. 10:Matangazo ya kwenu. Rudilia kwa kifupi mapendekezo fulani kutoka katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002 kwa ajili ya kutolea watu broshua Anataka na kitabu Ujuzi. Fanyeni onyesho la utoaji mmoja.

Dak. 13: Siaibikii Habari Njema. (Rom. 1:16) Kijana anamkaribia baba ili kumjulisha kwamba ana tatizo. Kijana huyo hapendi ajulikane kuwa Shahidi wa Yehova kwa sababu anaogopa kudhihakiwa na wenzake. Baba anamshukuru kijana huyo kwa kuwa mnyofu kuhusu jambo hilo. Anasimulia jinsi Petro alivyotenda wakati fulani kwa sababu ya mkazo ya wengine. (Mt. 26:69-74) Baba anatoa shauri lifuatalo: Hatupaswi kamwe kusikia haya ya kuwa Wakristo. (Mk. 8:38) Ni jambo lenye faida kujitambulisha kuwa Shahidi shuleni. Wanapojulishwa, walimu wengi wataheshimu imani zako na hawatajaribu kukuhusisha katika shughuli unazoona kuwa zisizokubalika. Huenda vijana wasio na kanuni za kiadili wasijaribu kukusukuma katika mwenendo mbaya. Wengine kati ya wanashule wenzako wataelewa kwa utayari zaidi kwa nini unachagua kutofanya urafiki wa kimapenzi, kutoshiriki katika michezo au shughuli nyinginezo za baada ya shule. Ikiwa wakati unaruhusu, baba na kijana wanazungumzia mawazo kutoka kichwa kidogo “Kujulisha Rasmi Peupe Urafiki Wako Pamoja na Mungu,” katika kitabu Vijana Huuliza, ukurasa wa 315-318. Kijana anashukuru kwa lile shauri nzuri.

Dak. 22: Jitiisheni Wenyewe kwa Mungu—Mpingeni Ibilisi. (Yak. 4:7) Akitumia maulizo yanayotolewa hapa, mzee mmoja anaongoza mazungumzo yenye uchangamfu kuhusu programu ya kusanyiko la pekee la siku moja lililofanyika mnamo mwaka wa utumishi uliopita. Alika washiriki wa kutaniko wasimulie jinsi walivyoweza kutumia yale waliyojifunza. (Sehemu zinaweza kutolewa kimbele.) Kazia sehemu zifuatazo za programu: (1) “Ujitiisho kwa Mungu Katika Ulimwengu Ulio Katika Utumwa.” Kwa nini tunapaswa kuwa macho ili kuepuka mitego ya ulimwengu? (2) “Tuonyeshe Ujitiisho wa Kimungu Tukiwa Washiriki wa Familia.” Kwa nini katika tengenezo la Yehova kuna uhitaji wa haraka wa kutia nguvu vifungo vya familia? Tunawezaje kufanya hivyo? (3) “Saidieni Wanafunzi Wapya Wasimame Imara Upande wa Yehova.” Tunawezaje kusaidia wapya washinde vizuizi vinavyojaribu imani yao? (4) “Kumpinga Ibilisi Kunamaanisha Nini?” Ni nini ufunguo wa kupinga Ibilisi kwa mafanikio? Zile silaha za kiroho zinazofafanuliwa kwenye Waefeso 6:11-18 zinawezaje kutulinda sisi? (w-SW 92 5/15 21-3) (5) “Vijana Wanaopinga Yule Mwovu kwa Mafanikio” na “Vijana Wanaofaidika na Ujitiisho wa Kimungu.” Ni nini mitego fulani-fulani ya Shetani ambayo vijana wanapaswa kujilinda wasinaswe nayo? Vijana wanabarikiwaje kwa kujitiisha kwa Yehova? (w-SW 90 8/1 13-14, fu. 15-17) (6) “Tufaidike na Ujitiisho wa Kimungu.” Eleza jinsi Wakristo wanavyoonyesha ujitiisho kwa mamlaka za kiserikali, kwa mabwana wa kazi, katika familia, na katika kutaniko la Kikristo. Ni sifa gani zitakazotusaidia kufanya hivyo?  

Wimbo 185 na sala ya kumalizia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine