Programu Ya Mikutano Ya Utumishi
Juma Toka Februari 10
Wimbo 4
Dak. 10:Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8, fanyeni maonyesho mawili tofauti kuhusu jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi wa Februari 15 na Amkeni! ya Februari 22. Katika kila tamasha, magazeti hayo mawili yanapaswa kutolewa yakiwa pamoja, hata ingawa ni moja tu ndilo linalokaziwa.
Dak. 35:“Tuhubiri na Kutoa Ushahidi Kamili.”* Itolewe na mwangalizi wa utumishi. Tia moyo wale wote wanaoweza kuwa mapainia wasaidizi mnamo Machi na Aprili. Omba wale waliopainia katika majira ya Ukumbusho mwaka uliopita watoe maelezo. Walifanyaje mipango ili kupainia? Hilo liliomba wafanye jitihada na marekebisho gani? Walipata shangwe na baraka gani? Rudilia programu za kielelezo zinazopatikana katika kisanduku kwenye ukurasa wa 4. Tangaza kwamba maombi kwa ajili ya utumishi wa painia msaidizi yatapatikana baada ya mkutano.
Wimbo 30 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Februari 17
Wimbo 48
Dak. 10:Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti. Rudilieni toleo la vichapo la Machi. Sema kuhusu pendekezo moja au mawili kwa ajili ya kutoa kitabu Ujuzi, ukitumia habari kutoka nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002. Kazia mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani.
Dak. 15:“Je, Unaweza Kutoa Nyumba Yako?” Hotuba itakayotolewa na mwangalizi wa funzo la kitabu. Tia ndani maelezo kutoka katika Kisanduku cha Maulizo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 2001 na Majibu kwa Maulizo Yenu katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 1990. Sema kuhusu hesabu ya vikundi vya mafunzo ya kitabu katika kutaniko lenu na hesabu ya wahudhuriaji kwa wastani. Omba mhubiri mmoja au wawili waeleze jinsi wao na familia zao wamefaidika kwa kuwa na funzo la kitabu katika nyumba yao. Yeyote ambaye angetaka kutoa nyumba yake anapaswa kujulisha hilo kwa mwangalizi-msimamizi.
Dak. 20:“Ni Jambo Gani Unalotanguliza?”* Fanya mipango kimbele ili mhubiri mmoja au wawili waeleze jinsi wameweza kurekebisha hali zao ili kufanya mengi zaidi katika huduma.
Wimbo 57 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Februari 24
Wimbo 74
Dak. 10:Matangazo ya kwenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Februari. Kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8, fanyeni maonyesho mawili tofauti kuhusu jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi wa Machi 1 na Amkeni! ya Machi 8. Katika kila tamasha, magazeti hayo mawili yanapaswa kutolewa yakiwa pamoja, hata ingawa ni moja tu ndilo linalokaziwa.
Dak. 15:“Msaada kwa Wakati Unaofaa.” Hotuba itakayotolewa na mzee. Kazia kwamba jitihada ya pekee inayofanywa ili kusaidia wale wasiotenda ni wonyesho wa jinsi Yehova anavyohangaikia watu wake kwa upendo.
Dak. 20:Unafaidikaje na Kitabu-Mwaka? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Kwanza, soma na ukazie mambo makuu katika “Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza.” Kisha, omba wasikilizaji wasimulie kuhusu ripoti na mambo yaliyoonwa kutoka katika kitabu-mwaka cha 2002 ambayo waliona kuwa yenye kutia moyo na yenye kuimarisha kwa njia ya pekee. Tia wote moyo wamalize kusoma kitabu-mwaka cha 2003 kitakapopatikana na kukitumia ili kusaidia wanafunzi wa Biblia wafahamiane na tengenezo la Yehova.
Wimbo 56 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Machi 3
Wimbo 14
Dak. 10:Matangazo ya kwenu. Zungumzieni kwa kifupi “Mpango Mpya Kuhusu Maktaba ya Jumba la Ufalme.” Taja yule atakayetumikia kuwa msimamizi wa maktaba ya Jumba la Ufalme.
Dak. 15:Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 20:“Iweni Timamu Katika Akili kwa Kuwa Mwisho Unakaribia.”* Mnapozungumzia fungu la 3-4, alika wahubiri fulani wasimulie miradi ya kiroho wanayofuatia sasa. Tia ndani maelezo kutoka ukurasa wa 176 wa kitabu Mwabudu Mungu.
Wimbo 127 na sala ya kumalizia.
* Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.