Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Februari: Kile kitabu kipya chenye kichwa Mkaribie Yehova kitatolewa. Machi: Toleeni watu kitabu Ujuzi. Jitihada ya pekee itafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu mwingine atakayechaguliwa naye anapaswa kufanya uchunguzi wa akaunti za kutaniko mnamo Machi 1 au mapema zaidi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Jambo hilo litakapokuwa limefanywa, toeni tangazo kwa kutaniko baada ya kusoma ripoti ya akaunti yenye kufuata. Someni barua yoyote ya shukrani kwa michango ya fedha ambayo kutaniko lilitoa kwa kazi ya ulimwenguni pote na kwa hazina nyingine yoyote inayosimamiwa na tengenezo.
◼ Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wanapaswa kukagua utendaji wa mapainia wa kawaida wote. Ikiwa yeyote ana matatizo ya kufikia kiwango cha saa, wazee wanapaswa kuchukua mipango ili msaada utolewe. Ili kupata mapendekezo, rudilieni barua S-201 za kila mwaka. Ona pia fungu la 1-9 katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 1987, ukurasa wa 3.
◼ Hotuba ya pekee ya watu wote kwa ajili ya majira ya Ukumbusho mnamo 2003 itakuwa na kichwa “Je, Saa ya Hukumu ya Babiloni Imefika?” Itatolewa Siku ya Yenga, Aprili 27. Makutaniko yatakayokuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko au kusanyiko mwisho-juma huo yatakuwa na hotuba ya pekee juma lenye kufuata. Hakuna kutaniko linalopaswa kuwa na hotuba ya pekee kabla ya Aprili 27, 2003.