Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Aprili na Mei: Toleeni watu nakala za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mnapofanya ziara za kurudia kwa watu wanaopendezwa, ambazo zinaweza kutia ndani wale wanaohudhuria Ukumbusho na/au matukio mengine ya kitheokrasi lakini ambao hawashirikiani na kutaniko kwa njia yenye kutenda, kazeni fikira juu ya kuwaachia kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli. Kila jitihada inapaswa kufanywa ili kuanzisha funzo la Biblia la nyumbani, zaidi sana ikiwa watu fulani wamekwisha kujifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka. Juni: Toleeni watu kitabu Ujuzi au broshua Anataka. Ikiwa wenye nyumba tayari wana vichapo hivyo, tumieni broshua nyingine inayofaa ambayo kutaniko linayo katika stoki. Julai na Agosti: Yoyote ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 inaweza kutumiwa: Jambo Gani Hutufikia Tunapokufa?; Je! Uamini Utatu?; Jina la Mungu Litakalodumu Milele; Je! Kweli Mungu Anatujali?; Kuishi Milele Duniani Katika Furaha!; Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa; Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?; Serikali Itakayoleta Paradiso; na “Tazama! Mimi Nafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.”
◼ Kuanzia Aprili, kadi za vitambulisho kwa ajili ya mkusanyiko wa wilaya wa 2003 zitatumwa mara moja pamoja na vichapo. Haitakuwa lazima kuzifanyia ombi. Kwa msingi wa ukubwa wa kila kutaniko, kadi zitatumwa zikiwa mafurushi ya kadi 25 kila furushi.
◼ Ni jambo la lazima kwa Sosaiti kuendelea kuwa na maandishi ya kisasa kuhusu anwani na namba za simu za waangalizi-wasimamizi na waandishi wote. Ikiwa kuna badiliko wakati wowote, Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko inapaswa kujaza na kutuma fomu Changement d’adresse du surveillant-président/secrétaire (S-29-F) kwa Sosaiti bila kukawia. Hilo linatia ndani mabadiliko yoyote katika namba ya siri ya mahali.
◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuendelea kuwa na kiasi cha kutosha cha fomu Demande d’admission au service de pionnier permanent (S-205-F), na Demande d’admission au service de pionnier auxiliaire (S-205b-F). Hizo zinaweza kuombwa kwenye fomu Demande de publications (S-14-F). Iweni na kiasi cha angalau mwaka mmoja. Rudilieni fomu zote kwa ajili ya utumishi wa painia wa kawaida ili kuhakikisha kwamba zimejazwa vizuri. Ikiwa wale wanaojaza fomu hawawezi kukumbuka tarehe kamili ya ubatizo wao, wanapaswa kukadiria tarehe hiyo na kulinda maandishi yake.
◼ Wakati wowote ambapo mipango ya kibinafsi ya kusafiri inatia ndani kuhudhuria mikutano ya kutaniko, kusanyiko la mzunguko, au mkusanyiko wa wilaya katika nchi nyingine, ombi lenu la habari kuhusu tarehe, wakati, na mahali linapaswa kuelekezwa kwa ofisi ya tawi inayosimamia kazi katika nchi hiyo. Anwani za ofisi za tawi zinaorodheshwa kwenye ukurasa wa mwisho wa Kitabu-Mwaka cha sasa.
◼ Ikiwa kuna gereza katika eneo la kutaniko fulani, kabla ya kupanga mikutano, wazee watajulisha tawi ili kupata mwelekezo.
◼ Kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kimetayarishwa katika karibu lugha zote za kienyeji za eneo letu. Makutaniko yanayosema lugha ambayo katika hiyo kitabu hicho hakikutafsiriwa yatatumia kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi katika lugha nyingine ya jimbo inayojulikana na sehemu kubwa ya washiriki wa kutaniko na ambayo katika hiyo kichapo hicho kinapatikana. Leo, kile kitabu kipya cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kimetafsiriwa au kinatafsiriwa katika Kifaransa, Kiluba, Kiswahili, Lingala, Monokutuba, Otetela, na Tshiluba.