Mikusanyiko ya Wilaya na ya Kimataifa Inatuchochea Tumtukuze Mungu!
Mikusanyiko ya Wilaya na ya Kimataifa “Mtukuzeni Mungu,” inayofanyika mpaka sasa, imetoa ushahidi mkubwa. Matukio hayo makubwa ya kitheokrasi yametukuza jina la Yehova na yameboresha uwezo wetu wa ‘kumpa Yehova utukufu unaofaa jina lake.’ (Zab. 96:8) Kwa kweli, anastahili kutukuzwa kwa sababu ya kazi zake nzuri ajabu za uumbaji, zinazoonyesha sifa zake za kustaajabisha.—Ayu. 37:14; Ufu. 4:11.
Kwa kutumia maulizo yenye kufuata pamoja na maandishi yenu binafsi, tayarisheni na kushiriki katika kujikumbusha programu ya mkusanyiko ambako kutafanyika mnamo juma la Oktoba 20.
1. Uumbaji usio na uhai unatangazaje utukufu wa Mungu, na hilo linatofautianaje na jinsi wanadamu wanavyomsifu? (Zab. 19:1-3; “Uumbaji Unatangaza Utukufu wa Mungu”)
2. Mgeuko-umbo ulitangulia kuonyesha jambo gani ambalo sasa ni halisi, na Wakristo leo wanachochewaje na jambo hilo? (Hotuba ya msingi, “Maono Matukufu ya Kinabii Hutuchochea!”)
3. Tunawezaje kusitawisha aina ya unyenyekevu ulioonyeshwa na nabii Danieli, na tutafaidikaje kwa kufanya hivyo? (Dan. 9:2, 5; 10:11, 12; “Yehova Huwafunulia Wanyenyekevu Utukufu Wake”)
4. (a) Ni mambo gani matatu kuhusu hukumu ya Mungu tunayoweza kujifunza kutokana na unabii wa Amosi? (Amo. 1:3, 11, 13; 9:2-4, 8, 14) (b) Ni somo gani lenye kufaa ambalo Mashahidi wa Yehova leo wanaweza kujifunza kutokana na mfano wenye kuonya unaopatikana kwenye Amosi 2:12? (“Unabii wa Amosi—Ujumbe Wake kwa Ajili ya Siku Zetu”)
5. (a) Kuna hatari gani za kutumia kileo kupita kiasi, hata ikiwa mtu halewi? (b) Tatizo la kutumia kileo kupita kiasi linawezaje kurekebishwa? (Marko 9:43; Efe. 5:18; “Epuka Mtego wa Kutumia Kileo Kupita Kiasi”)
6. Unafaidikaje na kichapo kipya “Ona Nchi Nzuri”? (“‘Nchi Nzuri’—Mwonjo wa Paradiso”)
7. Ni njia gani tatu ambazo katika hizo tunaweza ‘kutoa kama vioo mrudisho wa utukufu wa Yehova’? (2 Kor. 3:18; “Tutoe Kama Vioo Mrudisho wa Utukufu wa Yehova”)
8. Ni nini kilicho chanzo cha chuki isiyo na sababu, na ni nini kinachoweza kutusaidia tudumishe uaminifu wetu ijapokuwa tunapatwa na chuki ya namna hiyo? (Zab. 109:1-3; “Wanachukiwa Bila Sababu”)
9. Ni nini maoni ya Kristo kuhusu umashuhuri, na mtu anawezaje kutambua kwamba anahitaji kusitawisha maoni hayo kwa ukamili zaidi? (Mt. 20:20-26; “Kusitawisha Maoni ya Kristo Kuhusu Umashuhuri”)
10. Ni nini kinachoweza kutusaidia tubaki wenye nguvu kiroho ijapokuwa uchovu wa kimwili? (“Kuchoka Kimwili Wala Si Kiroho”)
11. Ni nini njia fulani ambazo kupitia hizo Shetani anaendeleza uwongo, na kulingana na Maandiko, inafaa kuitikiaje majaribio ya kuharibu imani yetu? (Yoh. 10:5; “Jihadhari na ‘Sauti ya Wageni’”)
12. (a) Wazazi wanawezaje kufuata mfano wa Yesu, kama unavyoonyeshwa kwenye Marko 10:14, 16? (b) Unapendezwa na nini kuhusu kile kitabu kipya Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu? (“Watoto Wetu Ni Urithi Wenye Thamani”)
13. Vijana wanamsifuje Yehova? (1 Ti. 4: 12; “Jinsi Vijana Wanavyomsifu Yehova”)
14. Ni maonyesho gani katika drama “Kuhubiri kwa Ujasiri Licha ya Upinzani” unayokumbuka?
15. Tunawezaje kuiga mfano uliowekwa na (a) Petro na Yohana? (Mdo. 4:10) (b) Stefano? (Mdo. 7:2, 52, 53) (c) kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza? (Mdo. 9:31; drama na hotuba “Tangaza Habari Njema ‘Bila Kuacha’”)
16. (a) Tuliazimia kumtukuza Mungu katika njia gani? (b) Tunaweza kuwa na uhakika gani tunapotumikisha yale tuliyojifunza kwenye Mikusanyiko yenye kichwa “Mtukuzeni Mungu”? (Yoh. 15:9, 10, 16; “‘Endeleeni Kuzaa Matunda Mengi’ Ili Kumtukuza Yehova”)
Kwa kutafakari juu ya mafundisho bora ya kiroho yaliyotolewa kwenye mkusanyiko huu, tutachochewa kutumikisha mambo tuliyojifunza. (Flp. 4:8, 9) Hilo litatia nguvu azimio letu la ‘kufanya mambo yote kwa utukufu wa Mungu.’—1 Kor. 10:31.