Kujikumbusha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maulizo yafuatayo yatatumiwa wakati wa kujikumbusha kwa maulizo na majibu kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi mnamo juma toka Agosti 29, 2005. Kwa dakika 30, mwangalizi wa shule ataongoza kujikumbusha kwenye kutegemea habari iliyozungumziwa katika migawo ya majuma ya Julai 4 mpaka Agosti 29, 2005. [Taarifa: Mahali ambapo kichapo hakionyeshwi baada ya ulizo, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona kitabu Shule ya Huduma, uku. 36-37.]
SIFA ZA USEMI
1. Tunaposhiriki tumaini letu na wengine, tunawezaje kufanya ‘usawaziko wetu ujulikane kwa watu wote,’ na kwa nini jambo hilo ni la maana? (Flp. 4:5; Yak. 3:17) [be uku. 251 fu. 1-3, kisanduku]
2. Namna gani kujua wakati wa kukubali maoni ya wengine kutatusaidia tuwashughulikie kwa mafanikio? [be uku. 253 fu. 1-2]
3. Kwa nini kutumia maulizo kwa ufundi ni jambo la maana tunaposaidia wengine kusababu (kufikiri) juu ya jambo fulani? [be uku. 253 fu. 3-4]
4. Ni mambo gani yanayoweza kufikiriwa ili kufanya hotuba iwe yenye kuvutia? [be uku. 255 fu. 1-4, kisanduku; uku. 256 fu. 1, kisanduku]
5. Ni nini tunalopaswa kukumbuka ikiwa tunaamua kutumia mambo yasiyo ya kibiblia yanayothibitisha kusudi letu ili kuunga mkono sababu za Maandiko? [be uku. 256 fu. 3-5, kisanduku]
MGAWO NA. 1
6. Ni uthibitisho gani ulio wazi unaoshuhudia kwamba Yesu aliishi duniani? [w03 6/15 uku. 4-7]
7. Namna gani ‘kinywa cha wanyoofu kitawakomboa,’ na namna gani nyumba ya waadilifu “itaendelea kusimama”? (Met. 12:6, 7) [w03 1/15 uku. 30 fu. 1-3]
8. Kwa kuwa Biblia haikuandikwa kama vile orodha yenye sheria zinazotuonyesha mambo tunayoweza kufanya na mambo tusiyoweza kufanya, tunawezaje “kufahamu yale yaliyo mapenzi ya Yehova”? (Efe. 5:17) [w03 12/1 uku. 21 fu. 3–uku. 22 fu. 3]
9. Ni kanuni gani za Biblia ambazo zinapotumiwa zinaweza kusaidia mtu kupambana na umaskini au hali za kiuchumi zisizofaa? [w03 8/1 uku. 5 fu. 5-uku. 6 fu. 2]
10. Mfano wa Yehova wa kutoa bure unapaswa kuwa na uvutano gani kwetu? (Mt. 10:8) [w03 8/1 uku. 20-2]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
11. Ni nini kilichofananishwa na nguzo mbili zilizoitwa Yakini na Boazi kwenye mwingilio wa hekalu lililojengwa na Sulemani? (1 Fal. 7:15-22)
12. Je, zawadi ya majiji 20 katika nchi ya Galilaya ambayo Sulemani alimtolea Mfalme Hiramu wa Tiro ilipatana na Sheria ya Musa? (1 Fal. 9:10-13)
13. Ni somo gani tunaloweza kujifunza kutokana na kutotii kwa “mtu wa Mungu”? (1 Fal. 13:1-25)
14. Ni katika njia gani Mfalme Asa wa Yuda alionyesha moyo mkuu, na tunaweza kujifunza nini kutokana na mfano wake? (1 Fal. 15:11-13)
15. Jinsi gani tukio lenye kuhusisha Mfalme Ahabu na Nabothi linaonyesha hatari ya kujisikitikia? (1 Fal. 21:1-16)