Matangazo
◼ Toleo la vitabu la mwezi wa 1: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa mbele ya mwaka wa 1991 kinaweza kutolewa. Ikiwa makutaniko hayana vitabu hivyo vya zamani katika stoki, yanaweza kutumia kitabu Ujuzi au broshua Endeleeni Kukesha! Mwezi wa 2: Toleeni watu kitabu Mkaribie Yehova. Ikiwa makutaniko hayana kitabu hicho, yanaweza kutolea watu kitabu Ujuzi au kitabu kingine cha zamani kinachopatikana katika stoki. Mwezi wa 3: Toleeni watu kitabu Biblia Inafundisha na mjikaze sana kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Kuanzia mwezi wa 2, au nyuma zaidi kuanzia tarehe 4 mwezi wa 3, hotuba mpya ya watu wote itakayotolewa na waangalizi wa mzunguko itakuwa na kichwa “Ni Nani Atakayestahili Kuingia Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu?”
◼ Programu ya DVD yenye kichwa Les jeunes s’interrogent... Que vais-je faire de ma vie ? itazungumziwa katika Mkutano wa Utumishi wa mwezi wa 4. Ikiwa mna lazima ya DVD hiyo, mfanye ombi mbele ya wakati kupitia kutaniko.
◼ Makutaniko yanapaswa kuchukua mipango yenye kufaa ili kuazimisha Ukumbusho mwaka huu Siku ya Kwanza, tarehe 2 mwezi wa 4, baada ya jua kutua. Ingawa hotuba inaweza kuanza mbele, kupitishwa kwa mifano hakupaswi kuanza mpaka jua litakapokuwa limetua. Chunguzeni mahali kwenu ili kujua wakati ambapo jua linatua. Kila kutaniko litajaribu kufanya mwazimisho walo lenyewe wa Ukumbusho. Hata hivyo, labda hilo lisiwezekane sikuzote. Mahali ambapo makutaniko mengi yanatumia kwa kawaida Jumba la Ufalme lilelile, labda kutaniko moja au zaidi yanaweza kukubaliwa kutumia jengo lingine jioni hiyo. Mahali ambapo inawezekana, tunapendekeza kwamba kuwe na dakika 40 kati ya programu mbalimbali kusudi wote wapate faida zaidi ya kuongea na marafiki baada ya Ukumbusho. Mtafikiria pia jambo la usafirishaji na mahali pa kuegeshea magari, kutia ndani mahali pa kushushia na kukamatia watu. Baraza la wazee litaamua ni mipango gani inayoweza kuwa bora zaidi mahali pao.
◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuwa hakika kwamba wana barua ya kupendekezwa (S-202-F) ya kila painia wa kawaida katika kutaniko. Ikiwa hawana, wanapaswa kuandikia ofisi ya tawi.
◼ Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2007 itatumwa kwa makutaniko yote ya Congo-Kinshasa bila kutumia fomu ya ombi la vitabu (S-14-F). Mtapokea hesabu sawa na ile ya Huduma Yetu ya Ufalme tunayowatumia. Hata hivyo, ikiwa kutaniko lenu limekwisha kutuma ombi (S-14-F) kama inavyoonyeshwa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 8, 2006 kwenye Matangazo, Idara ya Usafirishaji itashugulikia ombi hilo.