Matangazo
◼ Toleo la vitabu la Mwezi wa 2, 2007: Toleeni watu kitabu Mkaribie Yehova. Ikiwa makutaniko hayana kitabu hiki, yanaweza kutolea watu kitabu Ujuzi au kitabu kingine cha zamani kinachopatikana katika stoki. Mwezi wa 3: Toleeni watu kitabu Biblia Inafundisha na mjikaze sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Mwezi wa 4 na wa 5: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mnaporudilia wale walioonyesha kupendezwa, kutia ndani wale waliohuzuria Ukumbusho na/au matukio mengine ya kitheokrasi lakini hawashirikiane sana na kutaniko, mjikaze kuwatolea kitabu Biblia Inafundisha, mkiwa na kusudi la kuanzisha mafunzo ya Biblia. Mwezi wa 6: Toleeni watu kitabu Muumba au Furaha ya Familia.
◼ Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15 mwezi wa 3, 2007 utakazia habari “Kuja kwa Kristo—Kunakuhusu Jinsi Gani?’ Kwa kuwa ulizo hili ni la maana sana, kila kutaniko litapokea 15% ya zaidi ya gazeti hilo.
◼ Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wanapaswa kuchunguza utendaji au kazi ya mapainia wote wa kawaida. Ikiwa painia yeyote ana matatizo ya kueneza saa, wazee wanapaswa kuchukua mipango ili kumsaidia. Ili kupata mapendekezo, rudilieni barua ya kila mwaka S-201.
◼ Hotuba ya pekee kwa ajili ya majira ya Ukumbusho ya 2007 itakuwa na kichwa “Unaweza Kuwa na Usalama Katika Ulimwengu Huu Wenye Kuvurugika!” Ona tangazo linalohusiana na jambo hili katika Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 10, 2006.