Sisi Wote Tunaweza Kushiriki Katika Kazi ya Kufanya Wanafunzi Wapya
1 Mwanafunzi mpya si matokeo ya kazi ya mtu mmoja tu. Yehova anaweza kutumia “wafanyakazi wenzi” wake wote ili kusaidia wanafunzi wa Biblia wakomae kiroho. (1 Kor. 3:6-9) Kila mmoja wetu anasaidia wapya si kwa maelezo yetu tu yenye kutoka moyoni tunayotoa kwenye mikutano ya Kikristo, lakini pia kupitia mwenendo wetu mzuri unaoonyesha waziwazi jinsi roho ya Mungu inavyotenda katika maisha yetu. (Yoh. 13:35; Gal. 5:22, 23; Efe. 4:22, 23) Ni mambo gani zaidi tunayoweza kufanya ili kusaidia wapya?
2 Katika Kutaniko: Sisi wote tunaweza kuonyesha kuwa tunapendezwa na wale wanaoanza kuhuzuria mikutano, kwa kuchukua hatua ya kwanza ili kuwasalimia kwa furaha na kuzungumza nao mbele na kisha mikutano. Baada ya kufika kwenye Jumba la Ufalme kwa mara ya kwanza, mwanaume mmoja alisema hivi: “Kwa siku moja nilikutana na watu nisiowajua kabisa wenye upendo wa kweli kuliko watu wa kanisa langu tangu utoto. Ilionekana wazi kwamba nilikuwa nimeipata ile kweli.” Alibatizwa miezi saba kisha kuhuzuria mkutano wake wa kwanza.
3 Msifu kabisa mwanafunzi wa Biblia anapoanza kufanya maendeleo ya kiroho. Je, mwanafunzi wa Biblia anavumilia upinzani? Je, anahuzuria mikutano kwa ukawaida? Je, anatoa maelezo kwenye mikutano bila kuogopa? Je, amejiandikisha kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi au ameanza kushiriki katika kazi ya kuhubiri? Umusifu kwa maendeleo ambayo amefanya. Hilo litampa nguvu na kumtia moyo.—Met. 25:11.
4 Kiongozi wa Funzo la Biblia: Wahubiri fulani wamesaidia wanafunzi wao wa Biblia ili wafahamiane na washiriki wengine wa kutaniko kwa kuomba wahubiri wenye mfano mzuri wawasindikize kwenye funzo hilo. Inapowezekana umwalike bila kukawia mwanafunzi huyo kwenye mikutano ya kutaniko. Anapoanza kuhuzuria mikutano, umujulishe kwa wengine. Je, anafanya nguvu ili kushindana na tabia mbaya, kama vile kuvuta tumbako? Je, kuna mtu fulani katika nyumba yao anayepinga kujifunza kwake? Anaweza kufaidika kwa kuzungumza na mhubiri ambaye amepambana na kushinda tatizo kama hilo.—1 Pet. 5:9.
5 Wapya wana lazima ya kutegemezwa kiroho na kutaniko. Sisi wote tunaweza kuwasaidia wafanye maendeleo kwa kuonyesha kwamba tunapendezwa nao kwelikweli.