Matangazo
◼ Toleo la vitabu la Mwezi wa 11: Kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Ikiwa watu wanasema kwamba hawana watoto, muwatolee broshua Endeleeni Kukesha! Mwezi wa 12: Kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi, Mkaribie Yehova ao Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Mwezi wa 1: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa mbele ya mwaka wa 1991. Makutaniko ambayo hayana kiasi cha kutosha cha vitabu kama hivyo yanaweza kutolea watu kitabu Ujuzi ao broshua Endeleeni Kukesha! Mwezi wa 2: Kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? ao Siri ya Kupata Furaha ya Familia.
◼ Kwa kuwa mwezi wa 12 una Siku za Posho tano na Siku za Yenga tano, huo utakuwa mwezi muzuri sana ili kufanya kazi ya upainia msaidizi.
◼ Vitabu vingi vyenye kutegemea Biblia vinapatikana; vitabu ambavyo vimefanywa ili kuhubiria watu walio na mitindo mbalimbali ya maisha na wale walio na imani mbalimbali za kidini. Mtumishi anayeshugulika na vitabu ana karatasi ambako vitabu hivyo vyenye kusaidia vimetajwa.
◼ Wahubiri wote wanatiwa moyo kujaza kadi ya kiganga DPA (Instructions médicales/Désignation d’une personne de confiance), ikiwa hawajafanya hivyo. Kadi hiyo inatetea haki yenu ya kukataa kutiwa damu mishipani. Wazee watatolea kila mtu msaada ikiwa inahitajiwa.—Ona nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 11, 2006.
◼ Si lazima tena wahubiri wajaze fomu ya ripoti ya funzo (S-3) kwa ajili ya kila funzo la Biblia lililoongozwa katika mwezi. Hata hivyo, wataendelea kuandika mahali panapofaa kwenye fomu ya ripoti ya mahubiri (S-4), hesabu ya mafunzo ya Biblia yaliyoongozwa kila mwezi. Kwa hiyo, fomu S-3 itatumiwa tu ili kuandikia hesabu ya watu wenye kuhuzuria mikutano.
◼ Amkeni! ya mwezi wa 11, 2007 itazungumzia habari yenye kichwa: “Je, Unaweza Kuitegemea Biblia?” Kwa kuwa habari hiyo ni ya maana sana, kila kutaniko litapokea 10% ya zaidi kuhusu gazeti hilo.
◼ Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15/11/07 utazungumzia habari yenye kichwa: “Unaweza Kuwa na Maisha Yenye Kusudi!” Kwa kuwa habari hiyo ni ya maana sana, kila kutaniko litapokea 10% ya zaidi kuhusu gazeti hilo.
◼ Mbele ya mtu kulazwa katika hospitali, inapendekezwa kwamba kila mara ajulishe mzee mmoja wa kutaniko lenu ambaye anaweza kuzungumza na ndugu wanaohusika na Halmashauri ya Uhusiano na Hospitali (Comité de liaison hospitalier). Ndugu hao watamjulisha majina ya waganga walio na nia njema ya kusaidia na ambao wanajua vizuri ugonjwa wake. Kufanya hivyo ni kwa lazima sana ikiwa mtu anafikiri kwamba atatumwa katika mji mwingine, iwe katika inchi yenu ao hata katika inchi nyingine. Ili kuheshimu utakatifu wa damu, ni jambo la hekima kwamba, mbele ya kusafiri, mtu apate jina la mganga aliye na nia njema ya kusaidia. Betheli inaweza kumsaidia kupata habari hizo, lakini kufanya mipango ya lazima ni daraka lake yeye na watu wa jamaa yake ao marafiki.