Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/07 uku. 1
  • Tunawatangazia Wengine Tumaini Letu la Ufalme

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tunawatangazia Wengine Tumaini Letu la Ufalme
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Utie Nguvu Tumaini Yako ya Kikristo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Tunaweza Kupata Wapi Tumaini ya Kweli
    Amuka!—2004
  • Furahia Tumaini Yenye Haikatishe Tamaa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Tuhubiri Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2007
km 11/07 uku. 1

Tunawatangazia Wengine Tumaini Letu la Ufalme

1 Katika siku hizi za mwisho zenye hatari, watu wengi ulimwenguni hawana tumaini. (Efe. 2:12) Wengine kwa kukosa hekima wametia tumaini lao katika mali za kimwili, katika watawala, katika sayansi ya sasa na katika mambo mengine. Sisi ni wenye furaha kabisa kwa kuwa tuna tumaini la kweli kuhusu wakati ujao, tumaini lililo “nanga ya nafsi, likiwa hakika na imara.”—Ebr. 6:19.

2 Wakati wa utawala wa Ufalme wa Mungu, dunia itakuwa paradiso. Wapendwa wetu waliokufa watafufuliwa. (Mdo. 24:15) Umaskini, ukosefu wa haki, magonjwa, uzee na kifo vitakwisha. (Zab. 9:18; Mt. 12:20, 21; Ufu. 21:3, 4) Hizo ni ahadi fulani za Yehova zitakazotimizwa karibuni. Kati ya mambo hayo tunayotazamia, ni jambo gani unalongojea kwa hamu nyingi?  

3 Tangaza Habari Njema: Hatupaswi kubaki na tumaini la Ufalme bila kulijulisha wengine. Upendo kwa Yehova na kwa jirani unatuchochea kumwiga Yesu na “kuwatangazia maskini habari njema, . . . kuhubiri kuachiliwa huru kwa mateka na kupata kuona tena kwa vipofu, kuacha waliopondeka waende zao wakiwa wameachiliwa huru.” (Luka 4:18) Mtume Paulo alihubiri habari njema kwenye soko na mahali popote ambapo watu walipatikana. Alishugulika sana na kazi ya kuhubiri. (Mdo. 18:5) Kufuata mfano wake kwa kuhubiri kwa bidii kutazuia “mahangaiko ya mfumo huu wa mambo na nguvu za utajiri” visilegeze tumaini letu la Kikristo.—Marko 4:19.

4 Tumaini letu la Ufalme halilegei tunapokutana na watu wasiopendezwa na ujumbe wa Ufalme, na wale wenye kupendezwa nao kidogo tu ao na wale wanaotupinga waziwazi. ‘Tunashika imara tangazo la hadharani la tumaini letu bila kuyumba-yumba.’ (Ebr. 10:23) Hatuionei “aibu habari njema.” (Rom. 1:16) Labda uhakika wetu ulio wazi na uvumilivu wetu vitachochea mwishowe wengine wasikilize.

5 Ijapokuwa ni jambo lenye kufaa kuzungumzia hali za ulimwengu zinazoendelea kuharibika, ambazo zinatimiza unabii wa Biblia, sisi hatutakazia hali hizo katika mahubiri yetu. Lakini kazi yetu ya kuhubiri inakazia tumaini letu la Ufalme, yaani habari njema ya Ufalme wa Mungu. Na tuhubiri habari njema hii kwa uhakika na kwa bidii “ili kuwa na uhakikisho kamili wa tumaini mpaka mwisho.”—Ebr. 6:11.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine