Habari za Mahubiri Zenye Kufurahisha
Congo-Kinshasa: Tangu mwaka wa utumishi wa 2011 ulipoanza, tumepokea mara tatu ripoti za makutaniko zaidi ya 1,000 pa wakati. Ripoti hizo tulizopokea pa wakati ni 30% ya ripoti zote. Tafazali, tunawaomba mwendelee kukusanya haraka na kutuma ripoti za mahubiri pa wakati. Kufanya hivyo kunatia moyo.
Congo-Brazzaville: Katika mwezi wa 12, 2010, wahubiri walitolea watu magazeti zaidi ya 75,000, yaani kila muhubiri alitolea watu magazeti zaidi ya 11. Kutolea watu magazeti kunawatayarisha ili ‘wapokee upandwaji wa neno lile linaloweza kuokoa nafsi zao.’ (Yakobo 1:21).