Kisanduku Cha Maulizo
◼ Ni mambo gani unapaswa kufikiria ikiwa unataka tengenezo la Yehova liriti nusu ya mali yako ao mali yako yote utakapokufa?
Mutu anapokufa, hana tena uwezo wa kuamua jambo lolote juu ya mali yake. (Mhu. 9:5, 6) Kwa hiyo, watu wengi wanaandika barua ao testama inayoeleza namna mali zao zitagawanywa wakisha kufa. (2 Fal. 20:1) Barua ao testama hiyo ambayo kwa kawaida inajulikana kisheria, inaonyesha pia mutu ambaye atashugulikia mali hiyo na jinsi atakavyoigawanya. Katika inchi nyingi, ikiwa hakuna barua ao testama, ni wakubwa wa serikali ndio wataamua namna mali ya mutu aliyekufa itakavyogawanywa. Kwa hiyo, ikiwa tunataka mali yetu igawanywe kama tunavyopenda, kwa mufano, ikiwa tunataka tengenezo la Yehova liriti nusu ya mali yetu ao mali yetu yote kisha kifo chetu, lazima tuandike barua ao testama inayojulikana kisheria inayoonyesha mambo hayo; na pia tunapaswa kuchagua kwa uangalifu mutu ambaye atashugulikia mambo hayo kisha kifo chetu.
Mutu huyo ana daraka kubwa. Ikiwa feza na mali zingine ni vingi, kuvikusanya vyote na kuvigawanya kunaweza kuomba kazi nyingi na wakati mwingi. Pia, mara nyingi wakubwa wa serikali wana sheria ambazo zinapaswa kufuatwa. Kwa hiyo, si kila mutu katika kutaniko anayeweza kushugulikia mambo yaliyoandikwa katika testama. Lazima tumuchague mutu aliye na uwezo wa kufanya hivyo, mwenye kutumainika, na aliye tayari kabisa kufuata mambo yaliyoandikwa katika testama.—Soma habari yenye kichwa “Hekima na Manufaa za Kupanga Urithi wa Mali,” katika Amkeni! ya tarehe 8 mwezi wa 12, 1998.
Ikiwa Unaombwa Kushugulikia Testama: Ikiwa mutu anakuomba ushugulikie testama yake kisha kifo chake, kwanza hakikisha kwamba unajua uzito wa daraka utakalokuwa nalo na ufikirie jambo hilo katika sala ili kuona ikiwa una uwezo wa kutimiza daraka hilo. (Lu. 14:28-32) Kisha kifo chake, unapaswa kuwajulisha watu wote ambao majina yao yanatajwa katika testama hiyo kama ni wao ndio watakaofaidika na mali hizo. Kisha, unapoamua kufanya hivyo, itakuwa daraka lako kugawanya mali kufuatana na sheria na kwa kufuata kabisa mambo yaliyoandikwa katika testama. Iwe mali ya kugawanya ni mingi ao kidogo, mutu anayeshugulika na ugawaji huo hapaswi kupuuza mambo yanayoandikwa katika testama. Zawadi yoyote inayotolewa kwa shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova ni mali ya tengenezo la Yehova.—Lu. 16:10; 21:1-4.