Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi
Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika juma tokea tarehe 29 Mwezi wa 10, 2012. Tarehe ambayo kila jambo litazungumuziwa inaonyeshwa pia ili kusaidia watu kutafuta majibu katika vitabu wanapotayarisha masomo ya huduma ya kila juma.
1. Mazabahu ambayo Ezekieli aliona katika maono inafananisha nini? (Eze. 43:13-20) [Tokea tarehe 10 Mwezi wa 9, w07 1/8 uku. 10 fu. 4]
2. Ni nini kinachofananishwa na maji ya muto ambao Ezekieli anaona katika maono? (Eze. 47: 1-5) [Tokea tarehe 17 Mwezi wa 9, w07 1/8 uku. 11 fu. 2]
3. Maneno “aliazimia moyoni mwake” yanafunua nini juu ya maagizo ya kiroho ambayo Danieli alipata alipokuwa angali kijana? (Dan. 1:8) [Tokea tarehe 24 Mwezi wa 9, dp uku. 32 fu. 4-6; uku. 36 fu. 16]
4. Ni nini kilichowakilishwa, ao kufananishwa, na ule muti murefu sana katika ndoto ya Nebukadneza? (Dan. 4: 10, 11, 20-22) [Tokea tarehe 1 Mwezi wa 10, w07 9/1 uku. 18 fu. 5]
5. Andiko la Danieli 9:17-19 linatufundisha nini kuhusiana na sala? [Tokea tarehe 8 Mwezi wa 10, w07 1/9 uku. 20 fu. 5-6]
6. Ni agano gani lililoendelea ‘kutendeshwa kwa ajili ya wengi’ mupaka mwishoni mwa juma la 70 la miaka, ao mwaka wa 36 W.W? (Dan. 9:27) [Tokea tarehe 8 Mwezi wa 10, w07 1/9 uku. 20 fu. 4]
7. Tunaweza kusema nini kutokana na malaika aliyemwambia Danieli kwamba ‘mukuu wa ufalme wa Uajemi’ alikuwa amesimama mbele yake ili kumupinga? (Dan. 10:13) [Tokea tarehe 15 Mwezi wa 10, w11 1/9 uku. 8 fu. 2-3]
8. Ni unabii gani wa Biblia kuhusu Masiya uliotimiza andiko la Danieli 11:20? [Tokea tarehe 15 Mwezi wa 10, dp uku. 232-233 fu. 5-6]
9. Kulingana na Hosea 4:11, kukunywa pombe kupita kiasi kuna hatari gani? [Tokea tarehe 22 Mwezi wa 10, w10 1/1 uku. 4-5]
10. Tunaweza kujifunza nini kutokana na andiko la Hosea 6:6? [Tokea tarehe 22 Mwezi wa 10, w07 15/9 uku. 16 fu. 8; w05 15/11 uku. 24 fu. 11-12]