Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi
Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika juma tokea tarehe 29 Mwezi wa 4, 2013. Tarehe ambayo kila jambo litazungumuziwa inaonyeshwa pia ili kusaidia watu kutafuta majibu katika vitabu wanapotayarisha masomo ya huduma ya kila juma.
1. Kama inavyoonyeshwa kwenye Marko 10:6-9, ni jambo gani la maana kuhusu ndoa ambalo Yesu alitukumbusha? [Juma tokea tarehe 4 Mwezi wa 3, w08 15/2 uku. 30 fu. 8]
2. Kumutumikia Yehova kwa nafsi yote kunamaanisha nini? (Marko 12:30) [Juma tokea tarehe 4 Mwezi wa 3, w97 15/10 uku. 13 fu. 4]
3. “Maumivu ya taabu” yanayozungumuziwa katika andiko la Marko 13:8 ni nini? [Juma tokea tarehe 11 Mwezi wa 3, w08 15/3 uku. 12 fu. 2]
4. Luka alichunguza vitabu gani alipokuwa akiandika Injili yake? (Luka 1:3) [Juma tokea tarehe 18 Mwezi wa 3, w09 15/3 uku. 32 fu. 4]
5. Kwa kuwa Shetani anatafuta “wakati unaofaa” ili kujaribu utimilifu wetu, hilo linapaswa kutuchochea kufanya nini? (Luka 4:13) [Juma tokea tarehe 25 Mwezi wa 3, w11 15/1 uku. 23 fu. 10]
6. Tunaweza kutumia namna gani maneno yaliyo kwenye andiko ya Luka 6:27, 28? [Juma tokea tarehe 25 Mwezi wa 3, w08 15/5 uku. 8 fu. 4]
7. Sababu gani Yesu alisamehe zambi za mwanamuke fulani mbele atoe uzima wake kama zabihu ya ukombozi? (Luka 7:37, 48) [Juma tokea tarehe 1 Mwezi wa 4, w10 15/8 uku. 6-7]
8. Wafuasi wa Kristo ‘wanawachukia’ watu wa jamaa zao katika maana gani? (Luka 14:26) [Juma tokea tarehe 15 Mwezi wa 4, w08 15/3 uku. 32 fu. 1; w92 15/7 uku. 9 fu. 3-5]
9. “Ishara katika jua na mwezi na nyota” zitakuwa na matokeo gani juu ya wanadamu? (Luka 21:25) [Juma tokea tarehe 22 Mwezi wa 4, w97 1/4 uku. 15 fu. 8-9]
10. Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Yesu wa kusali tunapopambana na majaribu makali sana? (Luka 22:44) [Juma tokea tarehe 29 Mwezi wa 4, w07 1/8 uku. 6 fu. 2]