Matangazo
◼ Mwezi wa 9 na wa 10: Tutawatolea watu magazeti Munara wa Mulinzi na Amuka!
◼ Juma tokea tarehe 9 Mwezi wa 9, mbele ya kuanza mukutano, mwandishi wa kutaniko atatoa tangazo fupi kuhusu daraka la kila muhubiri la kutoa ripoti yake S-4, na daraka la mwandishi la kutuma ripoti ya kutaniko lote kwa kutumia SMS kama ilivyoagizwa katika barua ya tarehe 5 Mwezi wa 4, 2013, atafanya hivyo pia mwishoni mwa juma.
◼ Hotuba ya pekee ya watu wote kwa ajili ya kipindi cha Ukumbusho cha mwaka wa 2014 itatolewa katika juma tokea tarehe 21 Mwezi wa 4. Kichwa cha hotuba hiyo kitajulishwa baadaye. Makutaniko yatakayotembelewa na mwangalizi wa muzunguko juma hilo ao ambayo yatakuwa na mukusanyiko yatapanga hotuba ya pekee juma linalofuata. Hakuna kutaniko linaloruhusiwa kutoa hotuba hiyo ya pekee mbele ya tarehe 21 Mwezi wa 4.