Utafanya Nini Wakati wa Sikukuu?
Kwa kuwa watu wengi wanabaki nyumbani wakati wa sikukuu za taifa na za kidini, kwa kawaida, hizo ni nyakati zinazofaa ili kuhubiri. Makutaniko yanatiwa moyo kupanga mukutano kwa ajili ya mahubiri siku hiyo. Ikiwa watu wengi wa eneo hawataamuka mbio siku hiyo, ni vizuri kubadili wakati wa mukutano huo. Tangazo linaweza kufanywa kwenye Mukutano wa Utumishi ili kujulisha kutaniko kwamba mahubiri yamepangwa wakati wa sikukuu, na kutia wote moyo wahubiri siku hiyo. Kwa kweli, sikukuu zinatutolea nafasi ya kupumuzika ao kushugulikia mambo yetu ya kipekee. Lakini ni vizuri tupange kuhubiri kwa muda wa saa fulani siku hiyo. Kwa hiyo, tutapata furaha inayotokana na kushiriki katika kazi takatifu.—Mt. 11:29, 30.