Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/13 uku. 1
  • Tuige Mufano wa Manabii—Hosea

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuige Mufano wa Manabii—Hosea
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2013
Huduma Yetu ya Ufalme—2013
km 11/13 uku. 1

Tuige Mufano wa Manabii​—Hosea

1. Pengine umejiuliza ulizo gani?

1 ‘Niko tayari kujitoa kwa kadiri gani ili nifanye mapenzi ya Yehova?’ Pengine unajiuliza ulizo hilo unapofikiri sana juu ya uwingi wa wema na rehema za Yehova. (Zab. 103:2-4; 116:12) Hosea alikuwa tayari kufanya mambo ambayo Yehova alimuomba afanye, hata kama alihitaji kujitoa kabisa. Namna gani tunaweza kumuiga Hosea?

2. Namna gani tunaweza kuiga mufano muzuri wa Hosea wa kuendelea kuhubiri hata katika hali ngumu?

2 Hubiri Hata Katika Nyakati Ngumu: Ujumbe wa Hosea ulihusu kwanza ufalme wa makabila kumi ya Israeli, ambamo ibada ya kweli ilikuwa imepotea. Mufalme Yeroboamu wa 2 alifanya mambo machafu machoni pa Yehova, na aliendeleza ibada ya ndama ambayo Mufalme Yeroboamu wa 1 alianzisha. (2 Fal. 14:23, 24) Wafalme waliofuata, waliendelea kuharibu hali ya kiroho ya ufalme wa makabila kumi, mupaka ufalme huo ulipoharibiwa katika mwaka wa 740 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Lakini, hata kama ibada ya uongo ilienea sana, nabii Hosea aliendelea kutumika kwa uaminifu kwa miaka 59 hivi. Je, sisi pia tumeazimia kuhubiri mwaka baada ya mwaka, hata kama watu hawapendezwe ao wanatupinga?​—2 Tim. 4:2.

3. Namna gani ndoa ya Hosea na Gomeri, bibi muasherati, inaonyesha rehema ya Yehova?

3 Tutangaze Rehema ya Yehova: Yehova alimuagiza Hosea aoe ‘muke wa uasherati.’ (Hos. 1:2) Gomeri, bibi ya Hosea, alimuzalia mutoto mumoja; lakini, inawezekana baadaye Gomeri alizaa pia watoto wawili inje ya ndoa. Hosea alikuwa tayari kumusamehe bibi yake; hilo lilionyesha rehema kubwa ya Yehova kwa Waisraeli waliotubu. (Hos. 3:1; Rom. 9:22-26) Je, tuko tayari kuacha mambo fulani tunayopenda sana ili kutangaza rehema ya Yehova kwa watu wa namna zote?​—1 Kor. 9:19-23.

4. Tunaweza kujitoa kwa kadiri gani ili kufanya mapenzi ya Yehova?

4 Watumishi fulani wa Yehova wameacha kazi zenye mushahara mukubwa ili wawe na wakati mwingi wa kuhubiri. Wengine wamebaki bila kufunga ndoa ao bila kuzaa watoto ili kuendeleza faida za Ufalme. Tunapofikiri sana juu ya hali ya Hosea, tunaweza kuwaza hivi: ‘Singeweza kufanya mambo aliyofanya.’ Hata hivyo, tunapoendelea kusamini fazili zisizostahiliwa za Yehova na kutegemea roho yake takatifu ili kupata nguvu, anaweza kututumia kwa njia ambayo hatukutazamia, kama alivyomutumia Hosea.​—Mt. 19:26; Flp. 2:13.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine