UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | ZABURI 52-59
‘Umutupie Yehova Muzigo Wako’
Katika maisha yake, Daudi alipambana na majaribu mengi yenye kuumiza sana. Wakati Zaburi ya 55 iliandikiwa, alikuwa amepambana na majaribu kama vile . . .
Kutukanwa
Kuteswa
Kusumbuliwa sana na zamiri
Magumu katika familia
Magonjwa
Kusalitiwa
Hata wakati magumu yake yalionekana kuwa mazito sana, Daudi alipata namna ya kupambana nayo. Alitolea watu wenye wanaweza kujisikia kama yeye shauri hili lenye kuongozwa na roho: ‘Umutupie Yehova Muzigo Wako.’
Namna gani tunaweza kutumia andiko hili leo?
Umuambie Yehova katika sala magumu na mahangaiko yote yenye kuwa katika moyo wako
Tafuta muongozo na musaada katika Neno la Mungu na tengenezo lake
Fanya yote unaweza ili kutuliza hali yako, lakini usivunje kanuni za Biblia