Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb18 Mwezi wa 1 uku. 8
  • Kwanza Fanya Amani Pamoja na Ndugu Yako; Namna Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kwanza Fanya Amani Pamoja na Ndugu Yako; Namna Gani?
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kumaliza Kukosana Katika Roho ya Upendo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Musikwaze “Hawa Wadogo”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Muendelee ‘Kumusikiliza’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Fuatilia Amani
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
mwb18 Mwezi wa 1 uku. 8

MAISHA YA MUKRISTO

Kwanza Fanya Amani Pamoja na Ndugu Yako​—Namna Gani?

Mwanaume anaacha zawadi yake kwenye mazabahu na anaenda kufanya amani pamoja na ndugu yake

Wazia unaishi katika Galilaya wakati wa Yesu. Umeenda Yerusalemu ili kufanya Sikukuu ya Vibanda. Muji unajaa Wakristo wenye wametoka katika maeneo ya mbali. Unapenda kumutolea Yehova zawadi. Unabeba mbuzi, na unaanza kutembea katika barabara zenye kujaa watu zenye kuongoza kwenye hekalu. Wakati unafika, hekalu limejaa watu wengine wenye wanapenda kutoa zawadi. Kisha, wakati unafika ili utolee makuhani mbuzi yako. Wakati huo, unakumbuka kama ndugu yako, mwenye kuwa pengine kati ya watu ao katika muji, ana jambo fulani juu yako. Yesu anaeleza jambo lenye unapaswa kufanya. (Soma Mathayo 5:24.) Namna gani wewe na ndugu yako mwenye kuwa na jambo fulani juu yako munaweza kufanya amani kama vile Yesu anaomba? Onyesha jibu la kweli katika kila kisanduku chenye kuwa hapa chini.

UNAPASWA . . .

  • kuzungumuza na ndugu yako ikiwa tu unawaza kama ana haki ya kukasirika

  • kujaribu kumurekebisha ndugu yako ikiwa unaona kama anakasirika haraka ao ikiwa anakubali kama kosa ni lake

  • kumusikiliza ndugu yako kwa uvumilivu wakati anajieleza, na hata kama haumuelewe kabisa, umuombe musamaha kwa moyo wote kwa sababu umemukosea bila kujua

NDUGU YAKO ANAPASWA . . .

  • kuambia wengine katika kutaniko kosa lenye ulimufanyia, ili wajiunge naye

  • kukurekebisha, kurudilia kila kitu kuhusu kosa lenye ulimufanyia, na kukuomba ukubali kama kosa ni lako

  • kuelewa kama ilikuomba unyenyekevu na ujasiri ili kuja kumuona, na kukusamehe kwa moyo wote

Hata kama leo hatutoe zawadi za wanyama katika ibada yetu, Yesu alipenda kufundisha kama kuko upatano gani kati ya kufanya amani na ndugu yetu na ibada yenye tunamutolea Mungu?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine