MAISHA YA MUKRISTO
Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri Tutumie Muzuri Maulizo
SABABU GANI NI LAZIMA: Ikiwa ‘mawazo katika moyo wa mutu ni kama kilindi cha maji,’ maulizo ni kama mbeketi ya kutusaidia kushota maji hayo. (Met 20:5) Maulizo inachochea wasikilizaji wetu watoe mawazo yao. Majibu ya maulizo yenye kuchaguliwa muzuri inaleta matokeo ya muzuri. Yesu alitumia muzuri maulizo. Namna gani tunaweza kumuiga?
NAMNA YA KUFANYA:
Uliza maulizo ya kuchochea mutu atoe mawazo yake. Yesu alitumia maulizo mbalimbali ili kujua mawazo ya wanafunzi wake. (Mt 16:13-16; be uku. 238 fu. 3-5) Unaweza kuuliza maulizo gani ya kuchochea mutu atoe mawazo yake?
Uliza maulizo ya kuongoza mutu. Ili kurekebisha mawazo ya Petro, Yesu alimuuliza maulizo na kutoa majibu mbalimbali yenye ilimusaidia Petro apate jibu la kweli. (Mt 17:24-26) Unaweza kuuliza maulizo gani ya kuongoza mutu ili kumusaidia apate jibu la kweli?
Umupongeze musikilizaji wako. Kisha mwandishi fulani ‘kujibu kwa kutumia akili,’ Yesu alimupongeza. (Mk 12:34) Namna gani unaweza kupongeza mutu mwenye anajibia ulizo?
MUANGALIE SEHEMU YA KWANZA YA VIDEO FANYA KAZI YENYE YESU ALIFANYA—FUNDISHA, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:
Hata kama ni habari za kweli, sababu gani huo ni mufano mubaya wa kufundisha?
Sababu gani hatupaswe tu kufasiria habari?
MUANGALIE SEHEMU YA PILI YA VIDEO HIYO, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:
Namna gani ndugu huyo alitumia muzuri maulizo?
Ni mambo gani ingine tunaweza kuiga katika namna yake ya kufundisha?
Mafundisho yetu iko na matokeo gani juu ya wengine? (Lu 24:32)