Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb18 Mwezi wa 2 uku. 7
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri​—Tutumie Muzuri Maulizo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri​—Tutumie Muzuri Maulizo
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Timiza Daraka Lako La Mweneza​-injili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kutumia Maulizo
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
  • Bhayibele yi ko go Thušeng mo o ka fo yi Bala
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Unawaza Biblia Inaweza Kukusaidia?
    Furahia Maisha Milele!—Anza Kujifunza Biblia
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
mwb18 Mwezi wa 2 uku. 7

MAISHA YA MUKRISTO

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri Tutumie Muzuri Maulizo

SABABU GANI NI LAZIMA: Ikiwa ‘mawazo katika moyo wa mutu ni kama kilindi cha maji,’ maulizo ni kama mbeketi ya kutusaidia kushota maji hayo. (Met 20:5) Maulizo inachochea wasikilizaji wetu watoe mawazo yao. Majibu ya maulizo yenye kuchaguliwa muzuri inaleta matokeo ya muzuri. Yesu alitumia muzuri maulizo. Namna gani tunaweza kumuiga?

Yesu anauliza mwanafunzi wake moja ulizo

NAMNA YA KUFANYA:

  • Uliza maulizo ya kuchochea mutu atoe mawazo yake. Yesu alitumia maulizo mbalimbali ili kujua mawazo ya wanafunzi wake. (Mt 16:13-16; be uku. 238 fu. 3-5) Unaweza kuuliza maulizo gani ya kuchochea mutu atoe mawazo yake?

  • Uliza maulizo ya kuongoza mutu. Ili kurekebisha mawazo ya Petro, Yesu alimuuliza maulizo na kutoa majibu mbalimbali yenye ilimusaidia Petro apate jibu la kweli. (Mt 17:24-26) Unaweza kuuliza maulizo gani ya kuongoza mutu ili kumusaidia apate jibu la kweli?

  • Umupongeze musikilizaji wako. Kisha mwandishi fulani ‘kujibu kwa kutumia akili,’ Yesu alimupongeza. (Mk 12:34) Namna gani unaweza kupongeza mutu mwenye anajibia ulizo?

Ukuwe mwenye heshima. Tunapaswa kuonyesha heshima, zaidi sana kwa watu wenye kuzeeka, wale wenye hatujue, na wale wenye kuwa na mamlaka.​—1Pet 2:17.

MUANGALIE SEHEMU YA KWANZA YA VIDEO FANYA KAZI YENYE YESU ALIFANYA​—FUNDISHA, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:

  • Hata kama ni habari za kweli, sababu gani huo ni mufano mubaya wa kufundisha?

  • Sababu gani hatupaswe tu kufasiria habari?

MUANGALIE SEHEMU YA PILI YA VIDEO HIYO, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:

  • Namna gani ndugu huyo alitumia muzuri maulizo?

  • Ni mambo gani ingine tunaweza kuiga katika namna yake ya kufundisha?

Mwanaume anahangaika katika mazawo wakati hafundishiwe muzuri; mwanaume anaelewa kweli wakati anafundishiwa muzuri

Mafundisho yetu iko na matokeo gani juu ya wengine? (Lu 24:32)

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine