MAISHA YA MUKRISTO
Mungu na Kristo Watatupatia Uhuru Wakati Wenye Kuja
Ni magumu gani yenye uko unapambana nayo? Uko kichwa ya familia na uko na madaraka ya mingi? Uko unachunga watoto peke yako na uko unapiganisha ili kuwategemeza? Uko mwanafunzi, na ku masomo yenu wanafunzi wenzako wanakuchokozaka? Uko unapambana na magumu ya afya ao uzee? Kila mutu anakuwaka na magumu. Wakristo mingi wako wanapambana na magumu mingi wakati uleule. Lakini, tunajua kama hivi karibuni Yehova atatutosha mu ile magumu yote.—2Ko 4:16-18.
Kujua kama Yehova anaelewa magumu yetu, anafurahia uaminifu na uvumilivu wetu, na kama atatupatia baraka mingi wakati wenye kuja, kunatufariji sana leo. (Yer 29:11, 12) Yesu pia iko anatuhangaikia. Tuko hakika kama Yesu ataendelea ‘kuwa pamoja na sisi’ kadiri tunaendelea kufanya mambo yenye Wakristo wanapaswa kufanya. (Mt 28:20) Tunatia nguvu tumaini na azimio letu la kuvumilia magumu yenye tuko nayo sasa, wakati tunafikiri sana juu ya uhuru wenye tutapata wakati Ufalme wa Mungu utaanza kutawala dunia.—Ro 8:19-21.
MUANGALIE VIDEO UPEPO MUKALI UNAKARIBIA, ENDELEA KUMUTAZAMA YESU—BARAKA ZA UFALME ZA WAKATI WENYE KUJA, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Namna gani watu walijitenga na Mungu, na ile ilileta matokeo gani?
Ni baraka gani zenye Yehova atapatia wale wenye kuwa waaminifu kwake?
Nini njo itawezesha watu kupata zile baraka?
Ni baraka gani zenye uko unatazamia kwa hamu sana mu dunia mupya?
Wazia uko mu dunia mupya