Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb25 Mwezi wa 3 uku. 14-15
  • Tarehe 28/4–4/5

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tarehe 28/4–4/5
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2025
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2025
mwb25 Mwezi wa 3 uku. 14-15

TAREHE 28/4–4/5

MEZALI 11

Wimbo 90 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. Usiseme!

(Dak. 10)

Usiseme jambo yenye inaweza kuumiza “jirani” yako (Mez 11:9; w02 15/5 uku. 26 fu. 4)

Usiseme mambo yenye inaweza kugawanya batu (Mez 11:11; w02 15/5 uku. 27 fu. 2-3)

Usiseme mambo ya siri (Mez 11:12, 13; w02 15/5 uku. 27 fu. 5)

Mu Jumba ya Ufalme, bandugu bawili biko naongea. Mumoya kati yabo iko nasema mubaya juu ya ndugu mwingine mwenye iko nakuya pale kwenye biko.

ULIZO YA KUTAFAKARI: Namna gani maneno ya Yesu yenye kuwa mu Luka 6:45 inatusaidia tuepuke maneno yenye kuumiza?

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Mez 11:17—Juu ya nini ni muzuri kuonyesha fazili? (g20.1 uku. 11, kisanduku)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Mez 11:1-20 (th somo ya 5)

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Tafuta nafasi ya kuambia mutu jambo fulani yenye ulijifunza ku mukutano wenye umepita. (lmd somo ya 2 nukta ya 4)

5. Kuendelesha Mazungumuzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Tumia video yenye kuwa mu Byombo bya Kufundishia. (lmd somo ya 8 nukta ya 3)

6. Kufanya Banafunzi

(Dak. 4) MAHUBIRI YA MAHALI PA WATU WENGI. Ambia mutu kuhusu mupango wetu wa kujifunza Biblia na batu, na umuonyeshe namna tunafanyaka vile. (lmd somo ya 10 nukta ya 3)

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 157

7. Usiache Ulimi Wako Upoteze Amani

(Dak. 15) Mazungumuzo.

Juu hatukamilike, ni kawaida kukosea mu maneno yetu. (Yak 3:8) Lakini, kama tunafikiria matokeo ya kutumia mubaya ulimi wetu, ile itatusaidia kuepuka kusema mambo yenye tutahuzunikia kisha. Ona mifano fulani ya maneno yenye inaweza kufanya amani ipotee mu kutaniko:

  • Kujisifu kwenye hakufae. Maneno ya kujisifu inaweza kuchochea roho ya mashindano.—Mez 27:2

  • Maneno ya udanganyifu. Maneno ya udanganyifu haiko tu kuambia mutu bongo, inaweza kuwa pia kusema mambo yenye tunajua kama inaweza kupotosha mutu. Hata udanganyifu kidogo inaweza kutuharibishia sifa na kufanya batu basitutumainie.—Muh 10:1

  • Kusema bengine mubaya. Kusema bengine mubaya ni kusema juu ya bengine mu njia yenye inapotosha ukweli ao kuzungumuzia mambo yabo ya kipekee. (1Ti 5:13) Ile inaweza kuleta ugomvi na kugawanya batu

  • Maneno makali. Ile ni maneno yenye mutu anasema kwa ukali juu mutu alimukosea. (Efe 4:26) Maneno ya vile inaweza kuumiza mutu.—Mez 29:22

Picha za mu video “‘Ondoa’ Mambo Yenye Inapoteza Amani—⁠Sehemu.” 1. Emily anaikala ngambo ya pili ya Celia mu restora. Celia iko naangalia ku telefone byenye Hélène alitia ku Enternete. 2. Hélène iko namusema Celia kwa ukali ku parking ya Jumba ya Ufalme.

Muangalie VIDEO ‘Ondoa’ Mambo Yenye Inapoteza Amani—Sehemu. Kisha uliza basikilizaji:

  • Unajifunza nini kuhusu namna maneno yetu inaweza kwa urahisi kufanya amani ipotee mu kutaniko yetu?

Angalia video ‘Tafuta Amani na Uifuatilie’ juu ya kujua namna balirudishaka amani.

8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

(Dak. 30) bt sura ya 25 fu. 14-21

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo Mupya wa Mukusanyiko wa Eneo wa 2025 na Sala

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine