PENDEKEZO JUU YA MAMBO YA KUJIFUNZA
Ujifunze kwa Undani juu Uendelee Kuwa Macho
Soma Danieli 9:1-19 juu ujue sababu gani ni jambo ya maana kujifunza kwa undani.
Chunguza habari yote. Ni mambo gani ilikuwa imetokea, na ilikuwa na matokeo gani juu ya Danieli? (Da. 5:29–6:5) Kama weye njo ulikuwa Danieli ungejisikia namna gani?
Ujifunze mambo mingi zaidi. Pengine Danieli alichunguza “vitabu vitakatifu” gani? (Da. 9:2, maelezo ya chini; w11-SW 1/1 uku. 22 fu. 2) Juu ya nini Danieli alitubu zambi zake na za taifa ya Israeli? (Law. 26:39-42; 1 Fa. 8:46-50; dp-SW uku. 182-184) Sala ya Danieli inaonyesha namna gani kama alikuwa najifunza Neno ya Mungu kwa undani?—Da. 9:11-13.
Unajifunza nini? Ujiulize hivi:
‘Ninaweza kufanya nini juu mambo yenye iko napitikana mu dunia isinikengeushe?’ (Mik. 7:7)
‘Kama Danieli, nitapata faida gani kama ninajifunza Neno ya Mungu kwa undani?’ (w04-SW 1/8 uku. 12 fu. 17)
‘Ninaweza kujifunza habari gani zenye zitanisaidia ‘niendelee kukesha’?’ (Mt. 24:42, 44; w12 15/8 uku. 5 fu. 7-8)